Tanzania ukiajiriwa Serikalini ni raha kuzidi kujiajiri kwa kipato sawa na mshahara wa aliyeajiriwa

Ni kweli nakubali lakn kujiajiri kunaleta stress asikuambie mtu, mimi nilijifanya kukataa kwenda naona mambo yanakuwa magumu zaidi najuta kila siku naumiza akili.
mtu mvivu, asiye mbunifu, unayeridhika na kidogo, usiyefikiria mambo makubwa, ajira ya serikali inaweza ikawa nzuri. Lakini kwa wachapa kazi, wabunifu na mtu mwenye mawazo makubwa kimaendeleo, kujiajiri is the best ever! Nilisikia mzazi mmoja akisema mtoto huyu namwombea Mungu tu aajiriwe hasa serikalini maana hataweza kujiajiri kwa maana ni mzembe!
 
Kuna watu nawajua tangia nipo shule ya msingi wanaondoka majumbani saa 12 asubuhi kwenda kuuza dukani mpaka saa 2 usiku.
Mimi kwa experience yangu ya maisha naona wafanyabiashara wengi maisha nyumbani mazuri, wakati tupo wadogo ukiingia tu sebuleni kwa mfanyabiashara una notice utofauti na kwenu au nyumba za waajiriwa, nyumba za wafanyabiashara huwa zina vitu excess yani sebuleni kuna accessories ambazo muajiriwa ngumu kuwa nazo, nje usafiri wa kutosha alafu mara nyingi nyumba huwa wamejenga wao sio kupanga. Watoto wapo private schools

Tuseme tu ukweli wafanya biashara wengi japo wanaweza kuishi na stress sana ila maisha yao ndio hasa maisha ya mtanzania wa kipato cha kati, watumishi wengi (sio wote) sebuleni utakuta Tv nchi 32-43 , fridge na radio, sofa set moja na nje gari sana sana moja,wachache wana mbili basi, lakini nyumba za wafanya biashara madude mengi, huko nje gari nne na kuendelea
 
Ni ndoto za wazazi wengi kutaka tuajiriwe serikali hata mimi nilipata wakati mgumu nilipogoma kwenda kwenye ajira za serikali kwa kubweteka na mishe zangu lakini najuta, kuna waajiriwa pia wanafanya mishe zao pia.
 
Huu ukweli wanaukwepa..
 
Mkuu, wafanyabiashara wenye assets kama Ardhi nk hawawezi kupata mkopo kiurahisi ? Tuchukulie mfanyabiashara wa kipato cha kawaida anayeingiza faida milioni 3 kila mwezi, huyu atapata ugumu kupewa mikopo ?
 
Mkuu wa wilaya gani kampa bakora mwalimu[emoji23], walimu wanaonewa sana
 
Wengine humu mnasema biashara sio ngumu wakati mmekuta alishakufungulia baba yako kafanya kukuachia urithi. Umekuta foundation imekaa vizuri we kazi kusugua kisigino tu Mtupishe
Sasa jitahidi newewe kuweka mazingira Mazuri ili watoto wako wapate mteremko mbeleni.

Sent from my SM-A107M using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…