Tanzania ukisoma hadi chuo ni kama laana mtaani

Tanzania ukisoma hadi chuo ni kama laana mtaani

msomi duni

Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
90
Reaction score
301
Nisikuchoshe usinichoshe, bila kumsifu mama wala chama hata kama una masters, degree au diploma of honor Yani GPA ya nne ma straight A's huku mtaani ni laana tu kwanza unakuwa case study pili hupati michongo maana kila mtu anaona unaenda kumuovertake kwenye ugali wake ukienda kujiajiri ndio balaa tupu maana mkononi mtaji una elfu hamsini, unabaki kubishana tu vijiweni kati ya chama na pacome nani mkali utaishia kujua ofisi zote za kubeti na kama haitoshi utamsifu mama utakuwa chawa utapauka kama viatu vya mwalimu wa shule ya msingi.

Ndio maana tunaanza kuoneana wivu hadi tunaanza kutamani uchawi... Na ndio sisi tunaunga mkono kila hoja ya wapinzani ila tunakula ChiChieM na kussuport kikokotoo, mwisho nawashauri wadogo zangu kama hauna ndugu maofisini tena wenye vyeo usiwasumbue wazazi kukulipia ada bora ufanye mtaji uanze kuuza hata viatu au mawigi utanishukuru baadae.​
 
Pole sana inaonekana unapitia mazito, Elimu yako weka pembeni jikite katika kutatua changamoto za Jamii inayokuzunguke kama:

Chakula. Kipindi hiki ni cha mavuno nafaka bei cheee huku mjini bado ghali ingia humu kwa mtaji wowote utauona mwanga.
 
Pole sana inaonekana unapitia mazito, Elimu yako weka pembeni jikite katika kutatua changamoto za Jamii inayokuzunguke kama ;

Chakula. Kipindi hiki ni cha mavuno nafaka bei cheee huku mjini bado ghali ingia humu kwa mtaji wowote utauona mwanga.
Kaka elfu 50 naingia humo pesa ya kununua Io nafaka plus nauli ya kusafirisha plus vibali ni shughuli pevu labda nisubiri odd za wikiendi mkeka utiki
 
Nisikuchoshe usinichoshe, bila kumsifu mama wala chama hata kama una masters, degree au diploma of honor Yani GPA ya nne ma straight A's huku mtaani ni laana tu kwanza unakuwa case study pili hupati michongo maana kila mtu anaona unaenda kumuovertake kwenye ugali wake ukienda kujiajiri ndio balaa tupu maana mkononi mtaji una elfu hamsini, unabaki kubishana tu vijiweni kati ya chama na pacome nani mkali utaishia kujua ofisi zote za kubeti na kama haitoshi utamsifu mama utakuwa chawa utapauka kama viatu vya mwalimu wa shule ya msingi.

Ndio maana tunaanza kuoneana wivu hadi tunaanza kutamani uchawi... Na ndio sisi tunaunga mkono kila hoja ya wapinzani ila tunakula ChiChieM na kussuport kikokotoo, mwisho nawashauri wadogo zangu kama hauna ndugu maofisini tena wenye vyeo usiwasumbue wazazi kukulipia ada bora ufanye mtaji uanze kuuza hata viatu au mawigi utanishukuru baadae​
Hahaaaa mkuu Mbona Kama unashawishi hv 😀?
 
Jikusanye kuza mtaji hata kwa kuomba mbona shule umesomeshwa tafuta hata 500k tuu ingia Dodoma huku ni njaa njoo uza nafaka utapiga hela mpaka uikimbie..
500k ni nyingi wazazi washatua mzigo kitambo na Dodoma naijua vizuri maana nimesoma huko kuna gharama sana ya maisha acha nijipange nitajaribu hii wenda ikawa breakthrough yangu
 
Hali mtaani ni mbaya, elimu ina umuhimu wake ilikuwa ni ufunguo wa maisha ila kwa sasa ile funguo imepotea, watu wenye hali ngumu kiuchumi ni wasomi na wanazidi kuongezeka kila mwaka.
😂😂 iyo ya kusema elimu ni Ufunguo wa maisha hiyo ni dhana ya kipindi icho cha zamani ambapo hakukua na wasomi Kwaiyo ilikua mtu ukiingia tu darasani ukitoboa vizuri bas we kazi tayari unayo na umeshatoboa kimaisha lakini sio kwa sasa mzee
 
😂😂 iyo ya kusema elimu ni Ufunguo wa maisha hiyo ni dhana ya kipindi icho cha zamani ambapo hakukua na wasomi Kwaiyo ilikua mtu ukiingia tu darasani ukitoboa vizuri bas we kazi tayari unayo na umeshatoboa kimaisha lakini sio kwa sasa mzee
Kwa sasa hali ni tete, hata msomi wa zaman na wasasa wana utofauti mkubwa sana.
 
😂😂 iyo ya kusema elimu ni Ufunguo wa maisha hiyo ni dhana ya kipindi icho cha zamani ambapo hakukua na wasomi Kwaiyo ilikua mtu ukiingia tu darasani ukitoboa vizuri bas we kazi tayari unayo na umeshatoboa kimaisha lakini sio kwa sasa mzee
Wanatoboa ndugu yangu uchawi connection hata waliomaliza 2023 wengine wana ajira tena nyadhifa muhimu
 
Ndio ukubwa nishapoa
dunia ya sasa waliobea mafanikio yako ni mzazi au walezi wanaokusomesha, baada ya kukulipia ada mpaka unahitimu.

inabidi tena wakupe na mtaji ili uweze kujiajiri, tofauti na hapo labda upate kismati tu.

Umesomea udaktari mpaka ukahitimu, alafu unaambiwa ujiajiri!, je una mtaji wa kuanzisha hospitali?

Umesomea education mpaka ukahitimu, alafu unaambiwa ujiajiri! Je una mtaji wa kufungua shule?
 
Back
Top Bottom