Tanzania ya "viwanda" imeishia wapi?

Tanzania ya "viwanda" imeishia wapi?

Acha viwanda, Lukuvi ali-trend na single ya kurasimisha kila kipande cha ardhi nchi hii, mawakala mahiri wa janja janja wakachaguliwa kwenye zoezi la upimaji maeneo kadhaa hapa Dar kwa shs 150000/200000..... Pamoja na mawakala wa ardhi kukusanya pesa kwa watu kwa ahadi ya kurasimisha na kutoa hati, hakuna kinachoendelea na ofisi wamefunga, Serikali za mitaa hawana majibu zaidi ya kunyoshea kidole wizara ya ardhi. Viwanda ilikuwa ndoto ya JPM ambayo haikutimia, na sidhani kama itakuja kutimia.... Labda Bagamoyo inayopigiwa upatu kwa sasa!!? [emoji848]
Je una amini ni sahihi kuongoza taifa kwa ndoto ya mtu? Kwanini tusiwe na "ndoto/plan ya taifa"?

Leo hii huyo magufuli hayupo na ndoto yake pia haipo! Je why tusiwe na ndoto ya taifa ili mtu akifa ndoto ibaki?
 
Sera ya taifa haipo Bali sera ya rais,almaarufu maono ya raisi,ndo maana hata somo la historia ya taifa limefutwa maana ilikuwa sera ya Magufuri,na hata hili la Viwanda ilikuwa sera ya Magufuri

Kwa Sasa rais Samia bado sera zake hazijawa wazi japo ameanza na kutembelea nchi majirani kwa lengo ka kukuza diplomasia na pia kuja na tozo nyingi lengo likiwa kukamua watz ili aendeshee serikali yake na watz kwa ujumla.
 
Sera ya taifa haipo Bali sera ya rais.

Na hapa ndio tatizo lilipo.

JK alituamisha kwenye kilimo alipo kuja magu akaja na wimbo wa viwanda..

Tumepoteza miaka 6 tukiimba viwanda sasa tumerudi square 1.
 
Je una amini ni sahihi kuongoza taifa kwa ndoto ya mtu? Kwanini tusiwe na "ndoto/plan ya taifa"?

Leo hii huyo magufuli hayupo na ndoto yake pia haipo! Je why tusiwe na ndoto ya taifa ili mtu akifa ndoto ibaki?
Hata kabla ya Magufuli mambo yalikuwa hayaendi vile inavyopaswa. Tuliomba sana tupate mbeba maono tukapata na kwa hakika alituonyesha njia japo kwa mkono wa chuma. Sasa hayupo tumerudi kwenye arifu A.

Misingi ya kuendesha nchi inapaswa kujengwa na kuwekewa uzio ili pale watawala wanapobadilika misingi iliyojengwa iwe endelevu... Kwa bahati mbaya hapa kwetu, hatutaki kujenga nchi zaidi sana ni kujijenga kwa mtu mmoja mmoja au kikundi katika mfumo wa kibepari.
 
Nakumbuka miaka ya mwazo ya mwendazake wimbo wa viwanda uliimbwa sana na tukaambiwa mtu ukiwa vyerehani vinne basi unakiwanda.

Wakaenda mbele zaidi na kusema kila mkoa unaviwanda zaidi ya 100 (hapa figure siikumbuki vizuri ila ilikua kubwa). Na tukaambiwa mpaka mwaka jana Tz kuna viwanda zaidi ya 8400!

Sasa najiuliza je viwanda siku hizi vimeishia wapi? Mbona wanasiasa hawaimbi tena wimbo wa viwanda?
Achana na Njozi za mchana za yule mgonjwa wa Mirembe!
 
Nakumbuka miaka ya mwazo ya mwendazake wimbo wa viwanda uliimbwa sana na tukaambiwa mtu ukiwa vyerehani vinne basi unakiwanda.

Wakaenda mbele zaidi na kusema kila mkoa unaviwanda zaidi ya 100 (hapa figure siikumbuki vizuri ila ilikua kubwa). Na tukaambiwa mpaka mwaka jana Tz kuna viwanda zaidi ya 8400!

Sasa najiuliza je viwanda siku hizi vimeishia wapi? Mbona wanasiasa hawaimbi tena wimbo wa viwanda?

Ule utapeli wa Tanzania ya viwanda uliisha toka enzi za dhalimu akiwa hai.

Cc:jingalao
 
Tanzania ya viwanda ilikuwa na bado inabaki kama lengo jema la kukuza uchumi wetu kwa kupunguza imports na ikiwezekana kukuza exports.

Ili tufikie hapo, serikali (ofisi ya AG, hazina, wizara za uwekezaji na wizara ya viwanda) zingetengeneza financial instruments/soft financial leverage ili mkakati huo uwe halisi.

Bahati mbaya, waziri yule aliedai vyerehani 4 au machine za tofali ni kiwanda alikosa maono na mkakati mahsusi wa kufikia lengo.

Imagine nchi ndogo kama Sri Lanka yenye aneo la mraba 65,000 sqkm wanauza products za pamba (finished well designed cloths) kwenda soko la USA na EU.

Sri Lanka wanauza consumable tea ikiwamo Dilma moja ya brand 10 bora za chai duniani.

Mkoa wa Moro una eneo la 72,000SqKM.
Inatupa dhana Tz tunafanya kulimo cha mwaka '47 badala ya kufanya kilimo-biashara na viwanda vikiwa sehemu ya kuchakata mazao ghafi kwa kuwa na technology ya kisasa, mtiririko wa fedha utagusa sekta kibao kama fedha (banking, insurance and pension)

Logistics kwa magari kusafirisha raw products kwenda viwandani na kutokea viwandani kwenda bandarini kwa ajili ya exports.

Ni aibu Waziri wa fedha anawaza kodi na tozo badala ya kuja na mkakati mkubwa wa kukuza uchumi mkubwa.

Iko haja ya kuwa na think tank inayojenga mazingira ya private sector kukua kwa kuzalisha zaidi basics za soko la ndani, soko la SADC , soko la GCC watu walio jangwani na then soko la magharibi.

Napata tabu kusikia hata upanuzi wa bandari ya Tanga, debe ya kurejea kwenye drawing board ya Bagamoyo port husikii akili au mkakati kukuza uzalishaji ili kukuza exports.

Kinachosikika ni containers nyingi zitakuja toka China; containers zenyewe baadhi zina toothpick, leso, chupi, soft brooms, magunia ya kusindikia korosho, mifagio ya buibui hata nyama za ng'ombe na maziwa ya kusindika.

Uwepo wa mkakati wa kifedha ili kununua technology na know-how vingekuwa msingi wa Tanzania ya viwanda inayozalisha bidhaa, ajira na kukuza exports kwa kupunguza imports inakuwa halisi.

Tanzania ya viwanda ikitimia many of us will win; ikidoda kama sasa many amongst us are losing.
Ni aibu kusikia story graduates wa masters wanaendesha bajaji; haikuwa na maana kupeleka mtoto university then aishie kuendesha bajaji mtaani, sio sawa.

Weekend njema.
Point kubwa sana
 
Obviously wapo,wewe haufahamu hilo?
Walikwepo wanawake ambao walitawala kwa mkono wa chuma, Bi Golda Meir wa Israel na Bandaranaike wa Sri-Lanka. Wengine waliojaribu kuwakaribia ni Indira Gandhi na Margaret Thatcher.
 
Tanzania ya viwanda ilikuwa na bado inabaki kama lengo jema la kukuza uchumi wetu kwa kupunguza imports na ikiwezekana kukuza exports.

Ili tufikie hapo, serikali (ofisi ya AG, hazina, wizara za uwekezaji na wizara ya viwanda) zingetengeneza financial instruments/soft financial leverage ili mkakati huo uwe halisi.

Bahati mbaya, waziri yule aliedai vyerehani 4 au machine za tofali ni kiwanda alikosa maono na mkakati mahsusi wa kufikia lengo.

Imagine nchi ndogo kama Sri Lanka yenye aneo la mraba 65,000 sqkm wanauza products za pamba (finished well designed cloths) kwenda soko la USA na EU.

Sri Lanka wanauza consumable tea ikiwamo Dilma moja ya brand 10 bora za chai duniani.

Mkoa wa Moro una eneo la 72,000SqKM.
Inatupa dhana Tz tunafanya kulimo cha mwaka '47 badala ya kufanya kilimo-biashara na viwanda vikiwa sehemu ya kuchakata mazao ghafi kwa kuwa na technology ya kisasa, mtiririko wa fedha utagusa sekta kibao kama fedha (banking, insurance and pension)

Logistics kwa magari kusafirisha raw products kwenda viwandani na kutokea viwandani kwenda bandarini kwa ajili ya exports.

Ni aibu Waziri wa fedha anawaza kodi na tozo badala ya kuja na mkakati mkubwa wa kukuza uchumi mkubwa.

Iko haja ya kuwa na think tank inayojenga mazingira ya private sector kukua kwa kuzalisha zaidi basics za soko la ndani, soko la SADC , soko la GCC watu walio jangwani na then soko la magharibi.

Napata tabu kusikia hata upanuzi wa bandari ya Tanga, debe ya kurejea kwenye drawing board ya Bagamoyo port husikii akili au mkakati kukuza uzalishaji ili kukuza exports.

Kinachosikika ni containers nyingi zitakuja toka China; containers zenyewe baadhi zina toothpick, leso, chupi, soft brooms, magunia ya kusindikia korosho, mifagio ya buibui hata nyama za ng'ombe na maziwa ya kusindika.

Uwepo wa mkakati wa kifedha ili kununua technology na know-how vingekuwa msingi wa Tanzania ya viwanda inayozalisha bidhaa, ajira na kukuza exports kwa kupunguza imports inakuwa halisi.

Tanzania ya viwanda ikitimia many of us will win; ikidoda kama sasa many amongst us are losing.
Ni aibu kusikia story graduates wa masters wanaendesha bajaji; haikuwa na maana kupeleka mtoto university then aishie kuendesha bajaji mtaani, sio sawa.

Weekend njema.
Kabla ya kujenga vipya.Vya zamani vilitokomea vipi?.Na je,tunajiaminisha vipi kwamba vikijengwa vipya havitatokomea kusikojulikana kama vya mwanzo?
 
Back
Top Bottom