Tanzania yaifunga Namibia 1-0 CHAN

Tanzania yaifunga Namibia 1-0 CHAN

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Katika Mataifa ya kusini mwa Africa huwa nawahofia SA wenyewe, Zambia na Angola. Hawa waliobaki kama Botswana, Namibia, Malawi ni saizi yetu. Msumbiji wana utata kidogo lakini si kivile.

=========

TANZANIA imefufua matumaini ya kwenda Robo Fainali ya michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Namibia, bao pekee la kiungo Farid Mussa Malik dakika ya 65 akimalizia pasi ya mchezaji mwenzake wa Yanga, Ditram Nchimbi katika mchezo wa Kundi D Uwanja wa Limbe, Cameroon.

Baada ya sare ya 1-1 katika mchezo uliotangulia jana jioni, sasa Guinea na Zambia zinalingana kwa pointi, nne kila timu zikifuatiwa na Tanzania yenye pointi tatu, wakati Namibia imeaga mashindano baada ya kufungwa mechi zote mbili za mwanzo.

Sasa Tanzania watatakiwa kushinda mechi yao ya mwisho ya kundi hilo dhidi ya Guinea Jumatano Uwanja wa Reunification, Douala ili kwenda Robo Fainali.

1611462968039.png
 
Ifike wakati tukubaliane team ya taifa iundwe na wachezaji wa Simba, Yanga na Azam, hao wa kuokoteza Dodoma, Ndanda na Prison watatuchelewesha.

Stars imecheza vizuri sana first half lakini tatizo ni umaliziaji. Tumekosa mtu sahihi wa kumaliza shughuli pale mbele na kama mwalim hatafanya jambo sioni tukitoboa kwenye mechi hii.
 
Japo tunawashambulia Sana,na possession ipo kwetu,ila hawa jamaa wana foot work nzuri kuliko sisi.....angalia wanavyobuild mashambulizi wanafuata principles....sisi tunapiga mbele tu
Yani nakwambia wakituotea kimoja tu ujue mchezo ndo umeishia hapo, umiliki tupo juu leo kwasababu pale katikati kuna Ndemla na Fai toto, pia Kaseke anasaidia Sana pale.

Yani tungekuwa na mtu mwenye kasi kule upande wa kulia Kama Dillunga halafu pale kwa Lyanga angekuwepo mtu Kama Iddi Nado na nafasi ya Nchimbi angesimama Bocco hawa jamaa ingekuwa tayari wesha lala mapema tu.
 
Yani nakwambia wakituotea kimoja tu ujue mchezo ndo umeishia hapo, umiliki tupo juu leo kwasababu pale katikati kuna Ndemla na Fai toto, pia Kaseke anasaidia Sana pale.

Yani tungekuwa na mtu mwenye kasi kule upande wa kulia Kama Dillunga halafu pale kwa Lyanga angekuwepo mtu Kama Iddi Nado na nafasi ya Nchimbi angesimama Bocco hawa jamaa ingekuwa tayari wesha lala mapema tu.
Kumbe!!
 
Ifike wakati tukubaliane team ya taifa iundwe na wachezaji wa Simba, Yanga na Azam, hao wa kuokoteza Dodoma, Ndanda na Prison watatuchelewesha.
Stars imecheza vizuri sana first half lakini tatizo ni umaliziaji. Tumekosa mtu sahihi wa kumaliza shughuli pale mbele na kama mwalim hatafanya jambo sioni tukitoboa kwenye mechi hii.
Kwa hiki ninacho kiona hapa naweza sema uko sahihi kabisa mkuu.
 
Umeona mkuu, yaani cross za Kapombe na Faridi zinapotea bure tu hakuna wa kufunga huyu Nchimbi na Lyanga ni wa hovyo sana hawa jamaa aisee
Mwamnyeto anapiga mipira mizuri sana ila hakuna mmaliziaji, kutokana na vimo vya washambuliaji wetu ni afadhali tupunguze hii mipira ya juu.
 
Yani nakwambia wakituotea kimoja tu ujue mchezo ndo umeishia hapo, umiliki tupo juu leo kwasababu pale katikati kuna Ndemla na Fai toto, pia Kaseke anasaidia Sana pale.

Yani tungekuwa na mtu mwenye kasi kule upande wa kulia Kama Dillunga halafu pale kwa Lyanga angekuwepo mtu Kama Iddi Nado na nafasi ya Nchimbi angesimama Bocco hawa jamaa ingekuwa tayari wesha lala mapema tu.
Hii mechi ingeisha mapema hata beki 3 angekuwa Tshabalala cos cross za huyu beki Manyama wa Namungo daah inakatisha tamaa,kunafree kick kapiga shida tupu......hii mechi Dilunga,Tshabalala,Sure boy,Idd Nado,Mkude mechi ingeisha mapema kiasi
 
Hii mechi ingeisha mapema hata beki 3 angekuwa Tshabalala cos cross za huyu beki Manyama wa Namungo daah inakatisha tamaa,kunafree kick kapiga shida tupu......hii mechi Dilunga,Tshabalala,Sure boy,Idd Nado,Mkude mechi ingeisha mapema kiasi
Kabisa mkuu, alafu hivi Yassin yuko wapi kwanini asipewe nafasi labda ataleta kitu tofauti na huyu Manyama huyu.

Kifupi huku upande wa kushoto kumekufa kabisa
 
Ifike wakati tukubaliane team ya taifa iundwe na wachezaji wa Simba, Yanga na Azam, hao wa kuokoteza Dodoma, Ndanda na Prison watatuchelewesha.
Stars imecheza vizuri sana first half lakini tatizo ni umaliziaji. Tumekosa mtu sahihi wa kumaliza shughuli pale mbele na kama mwalim hatafanya jambo sioni tukitoboa kwenye mechi hii.
Haya tumchezeshe striker gani wa Azam Simba na Yanga tutajieni Basi???? Huko Simba akina kagere mugalu miquson wote wageni

Huko Yanga tumchukue saido ?sarpong? Au yacouba? Au tuisila

Huyo nchimbi anatokea wap so huko Yanga mbn mnapenda kutafuta escape goat kwa wachezaji wa timu za Kati

Simba Yanga Azam si walifungwa na Burundi taifa hao
 
Kabisa mkuu, alafu hivi Yassin yuko wapi kwanini asipewe nafasi labda ataleta kitu tofauti na huyu Manyama huyu.

Kifupi huku upande wa kushoto kumekufa kabisa
Nadhani yupo sub,labda atapata nafasi
 
Back
Top Bottom