Tanzania yatajwa kuwa miongoni mwa nchi 7 zinazotarajiwa kuwekewa vikwazo vya kuingia Marekani

Vikwazo vya raia wa Tz kuingia Marekani so vikwazo vya kiuchumi.
Go back and read again
 
Anayeshangilia au anayelia nadhani haisaidii hapa kumjua. La muhimu ni kuwaonya wanaosababisha nchi kuwekewa vikwazo kuwa vikiwekwa kwa ujinga na tabia zao ambazo tunawaambia siku zote kuwa hazifai basi wasubiri na sisi tuwashukie na kuwagawana.

Zimbabwe waliruhusu ufala wa Mugabe kujifanya mbabe wananchi wameteseka na wengine kufa huku yeye na mkewe Grace wakiendelea kuiba na kujilimbikizia Mali Singapore, Dubai na ulaya.

Sisi tutor tahadhari mapema kuwa hadithi za sijui mabeberu sijui nini hatuwezi kuzikubali kamwe
 
Nilijua tu una malengo ya kisiasa, sasa hiyo gia si ndo mtaingia ikulu kiulaini
Hujui kuwa walikuwepo akina January huko ikulu? Hujui kuwa walikuwepo akina nape huko ikulu? Wengne wemeingia Kwa kuokota embe kwenye mnazi ndio uone aliyomo humo kama hat miliki? Hata wale Jamaa waliongia humo Kwa matarajio ya wengi pasipo kubahatisha waliiacha, uboya wako na ushamba wako unakusumbua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kuchanganya taarifa wewe!!! Inasemekana Kuna watu ambao hawajawa nominated watawekewa vikwazo vya kutofika/kutopata Visa card ya Marekani.
Sababu zenyewe hazijawekwa wazi na Kama zimewekwa hazina athari yoyote kwa Nchi ilihali viongozi wa juu hawataguswa.
 
Inaeleweka kabisa Trump jinsi alivyo juu ya mataifa ya africa na yale ya kiislamu,trump hapendi wageni kutoka africa na hayo mataifa ya kiislamu
Ni chuki tu
 
Si amesema ana mpango kwani ameshaweka ivyo vikwazo? Halafu uko USA sio pekee tu pa kwenda, kuna sehemu nyingi tu za kula bata na kutafuta maisha..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waache watufungie,nani anataka kwenda huko
Hizo ni hasira tu baada ya sera za ushoga kukataliwa,watarudi kivingine wakikwama na ubeberu wao

Wala sio ushoga, ni mtu mmoja kukandamiza demokrasia
 
kumtukana mzungu kwakumuita majina mabaya kama mabeberu na wanyonyaji ni sawa na mfanyakazi kumtukana bosi, unatarajia nini kitatokea?

wazungu tunapaswa kuwaheshim sana coz juhudi zao ndo zimefanya tuifurahie zaidi dunia
acha watuadhibu ili tujifunze kuwaheshimu
 
Raisi wa marekani Donard Trump aweka vizuizi kwa nchi baadhi za africa pamoja na katazo kutoingia nchi marekani.

. Trump ato sababu za Tanzania kuwekewa vikwazo kusafiri Marekani https://youtu.be/btga2aNgvmY


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hana jibu zaidi atakwambia demokrasia
 
Kurzweil,
Marekani ina jadili kuwawekea Watanzania vikwazo kuingia Marekani

Serikali ya Marekani ina mpango wa kuziongeza Nchi nyingine 7 ikiwemo Tanzania kwenye orodha ya Nchi ambazo Raia wake wamewekewa zuio/vikwazo vya kuingia Nchini humo.

Nchi nyingine kwenye hizo 7 ni Nigeria, Sudan, Eritrea, Myanmar, Belarus na Kyrgyzstan ambapo Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti kwamba baadhi ya Nchi VISA zinaweza zisifungiwe kabisa bali zitakua ngumu kupatikana kwa masharti zikiwemo VISA za biashara na za matembezi.

Idara ya mambo ya ndani ilipotafutwa na Waandishi haikuwa tayari kujibu chochote kuhusu hili lakini kwa upande mwingine Maafisa kwenye Uongozi wa Rais Trump wamesema bado orodha haijakamilika kwani mpaka Jumanne jioni Ikulu ilikua bado inajadili kuongeza ama la Nchi nyingine moja au mbili ambapo pia Nchi nyingine kwenye hii orodha zitafungiwa kushiriki bahati nasibu ya Green Card.


 

Attachments

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…