Kilichobaki sasa ni kila mmoja kuchukua tahadhari binafsi ili kujikinga dhidi ya Covid-19 na siyo kutegemea serikali peke yake ikusaidie kuchukua tahadhari.
Hii ni vita halisi, na kila mmoja wakati huu anaishiriki.
Hii serikali imeshalemewa tayari, tahadhari walishindwa kuchukua tangu awali hivyo saiv watu wanapukutika tuu.
Bunge limegeuka kuwa machinjioni. Hivi mpaka afe Ndugai ndo hawa wakawekwe karantini? Ulafi wa posho na kiburi cha kutaka kumaliza shughuli as per ratiba KUTAWAMALIZA wote
Naanza kupata wasiwasi na wale wote walioshiriki kikao cha kupokea ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) pale chamwino dodoma hasa mawaziri na viongozi wengine wakubwa wa nchi...
Kwa maslahi ya afya zao ni vyema wakaanza kuchukua hatua mapema...
COVID-19 is real guys. Apumzike kwa Amani bwana Balozi.
Aisee hii hatari.
Nimesikitika sana kuona neno mchapa kazi ndani ya hiyo notice kutoka Ikulu.
Sasa ni wakati wa kusifia kazi za marehemu kweli?
Hali ngumu iliyopo nchini bado tunatumia maneno ya mazoea?