TANZIA: Ephraim Kibonde afiwa na Mke wake Sara Kibonde


Pole sana Kaka yangu na Kiongozi wangu wa Kitaaluma pia Ephraim Kibonde kwa Kuondokewa na Mpendwa Mke wako Sarah. Binafsi naungana nawe katika Kipindi hiki Kigumu na namwomba Mwenyezi Mungu akutie nguvu, akupe rehema na uvumilivu pia. Kikubwa tumshukuru Mwenyezi Mungu na tumuombee sana Mpendwa wetu Sarah ili apokelewe vyema huko aendako.

Nimepokea taarifa hii kwa mshtuko mkubwa mno, najua maumivu uliyonayo Kaka ila jikaze na yote tumshukuru Maulana.
 
Mkuu kama kuna uwezekano wa kuja kutoka huko mbali hudhuria huu msiba
 
Pole sana Ephraim,nakumbuka takribani miezi 4 imepita sasa tangu siku ile tuliopishana na wewe pale Hindu mandal nje ukiwa umemshikilia mke wako ukielekea kwenye gari,Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…