TANZIA TANZIA: Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani afariki dunia

TANZIA TANZIA: Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani afariki dunia

*Sehemu ya Maelezo ya Jaji Ramadhani Mwaka 2010 kuhusu CV yake*

Nimezaliwa Desemba 28, mwaka 1945 Zanzibar mjini nikiwa ni mtoto wa pili kati ya watoto wanane, wa kike wanne na wanaume wanne. Ni Mkristo wa dhehebu la Anglikana.-

Nimesoma shule mbalimbali za msingi Mpwapwa mkoani Dodoma 1952 -1953 nikaenda Town School-Tabora nikasoma darasa la tatu hadi la nne mwaka 1954-1956 na darasa la sita na saba nilisoma Kazel Hill sasa inatwa Shule ya Msingi Itetemia mwaka 1957-1958. Na darasa la nane tu mwaka 1959 nikarudi kusoma Mpwawa.

Mwaka 1960-1965 nilijiunga na Tabora School kwa ajili ya masomo ya kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwakuwa nilifaulu nilichaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1966, na nilisoma shahada yangu ya Sheria na ilipofika Machi 1970 nilihitimu masomo.

Na mwishoni mwa Machi mwaka huo huo wa 1970 nikajiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), niliingia jeshini kama mwanasheria raia mpaka kipindi cha mafunzo ya kijeshi nikaenda kwenye mafunzo na kisha nikarudi kuitumikia JWTZ.

Ilipofika mwaka 1971 nikapewa kamisheni kambi ya Mgulani nikawa Luteni (nyota mbili). Nikaendelea na jeshi hadi mwaka 1977, nikahamishiwa Brigedi ya Faru-Tabora nikiwa na cheo cha Meja.

Sasa mwaka 1978, wewe mwandishi ulikuwa hujazaliwa, ndiyo mzee Aboud Jumbe Mwinyi, wakati huo akiwa ni rais akaniita Zanzibar na kuniteua kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar na kipindi hicho Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Damian Lubuva.

Aidha Oktoba 1978 niliteuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar. Na ilipofika Machi 1979 nilirudishwa JWTZ na baada ya muda mfupi nikapelekwa kwenye vita ya Uganda , nikiwa na cheo cha Luteni Kanali na kwenye vita hiyo nilikuwa naendesha mahakama za kijeshi.

Vita ilipokwisha nikarudi Zanzibar. Januari 8 mwaka 1980 nikaapishwa kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar, wakati huo nikiwa na cheo cha Luteni Kanali. Nikaendelea na Ujaji Mkuu Zanzibar hadi Septemba 1989 alipoapishwa Jaji Mkuu Zanzibar Hamid Mahamod Hamid.

Hata hivyo Juni 23 mwaka 1989 niliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania hadi mapema wiki hii nilivyoteuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Nilipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani hapa Bara ndiyo sababu ya kuacha ujaji Mkuu Zanzibar.
Januari 1993 niliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na niliendelea na nafasi hiyo hadi Januari 2003 na Oktoba 2002 niliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ambapo kipindi changu cha miaka mitano katika tume ZEC kinamalizika Oktoba mwaka huu.

Novemba 2001, niliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki nafasi ambayo natakiwa nimalize kipindi changu cha miaka sita Novemba mwaka huu.

Nina mke mmoja ambaye Mungu ametujalia tumebahatika kupata watoto wanne, wawili ni wasichana na wawili ni wavulana.

Mtoto wangu wa kwanza anaitwa Francis (30) huyu ni mwanasheria na anafanyakazi ya uwakili Manchester, Uingereza, Brigeth, huyu ana shahada ya Uandishi wa Habari na anafanyakazi ICAP hapa nchini, Marina ni mfamasia, yuko Liverpool, Uingereza na Mathew naye ni mfamasia, anafanya kazi Liverpool."
 
Sasa nimeelewa kwa nini bwana yule yuko nyumbani kwao kwa likizo
... kuwa nyumbani kwa likizo sio tatizo ni jambo jema sana; tatizo ni jinsi anavyotelekeza wengine wakati wao (the top ones) wameamua kujichimbia kusikojulikana!

Tunaambiwa kama huna cha kufanya mjini usitoke lakini hawatoi suluhisho kwa mfano wafanyakazi wafanyeje! Na keshokutwa ni Mei Mosi nitashangaa kama chama cha wafanyakazi hakitazungumzia hili tena kwa lugha ya kueleweka!
 
Huu mlolongo wa vyeo bado sijauelewa.
From brigedia to jaji mkuu to mchungaji.

Mwenye kunielewasha nitashukuru.

Sent using Jamii Forums mobile app
Alijiunga jeshini akiwa na taaluma ya sheria,huko akapanda hadi kufikia ngazi za juu jeshini,baadae akahamishiwa idara ya mahakama,huko nako akapanda had I kufikia kuwa Jaji.

Akiwa ni muumini wa kanisa la Anglikana,alichukua mafunzo ya Theolojia ambapo baada ya kustaa utumishi wa Umma akateuliwa na kanisa lake kuwa Mchungaji huko Zanzibar.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salaam za rambirambi kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma Kufuatia kifo cha Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mhe. Augustino Ramadhani aliyefariki dunia leo katika hospitali ya Agha Khan jijini Dar es salaam.

Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani amefariki dunia leo saa 2:05 Asubuhi katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Rais Magufuli amempigia simu Jaji Mkuu wa Tanzania na kumpa pole baada ya kupata taarifa ya kifo cha Jaji Mkuu huyo Mstaafu.

“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Jaji Mkuu Mstafu Augustino Ramadhani, napenda kutoa pole kwako, familia ya marehemu, waheshimiwa Majaji wote pamoja na watumishi wa Mahakama ya Tanzania”, alisema Rais Magufuli.

Marehemu Jaji Augustino Ramadhani aliteuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania mwaka 2007 mpaka mwaka 2010 alipostaafu.

Miongoni mwa nyadhifa nyingine alizowahi kushika ni pamoja na kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu mwaka 2010 lakini pia mwaka 2014 aliteuliwa kuwa Rais wa Mahakama hiyo, wadhifa alioushika kwa kipindi cha miaka miwili mpaka mwaka 2016 alipomaliza muda wake.

Marehemu Jaji Ramadhani pia aliwahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoundwa na Rais wa Awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Julai 4, 2012.

Mipango ya mazishi itajulikana baadaye.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, JINA BWANA LIHIMIDIWE.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom