Tanzia: Mfanyabiashara wa madini na mpenzi wa Lulu afariki dunia

Tanzia: Mfanyabiashara wa madini na mpenzi wa Lulu afariki dunia

americana

Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
84
Reaction score
37
Anajulikana kwa jina la Seky, alikuwa muajiriwa tanzanite one.

Kafariki leo inasemekana alikalia stuli ya kioo ikapasuka na kumjeruhi mgongoni.

==========

View attachment 244096
Marehemu Lusekelo Samson Mwandenga (Seky) enzi za uhai wake, (RIP)..

Familia ya marehemu Lusekelo Samson Mwandenga 'Seky' imeweka wazi chanzo cha kifo cha marehemu baada ya kuzagaa habari mitandaoni kuhusu chanzo cha kifo chake.

Familia hiyo imeeleza kuwa marehemu aliumizwa na kiti cha kioo akiwa kambeba mtoto wake nyumbani kwake kisha akapelekwa hospitali na baadaye kufariki dunia akiwa hospitali.

Enzi za uhai wake, marehemu alikuwa mdau mkubwa wa Bongo Movies na Bongo Fleva, hivyo msiba wake umegusa tasnia hiyo.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Secky mahali pema peponi. AMEN.


Chanzo: GPL

===========

Wakati huohuo, mfalme wa mitandao yote ya jamii, W. Malecela a.k.a Le Mutuz (54), ametoa le tamkozi kuhusu kifo cha mfanyabiashara kama ifuatavyo;

" Live at my Office downtown Dar Tancot House 2nd FL kazi kama kawa maana Mwanaume ni kazi kwanza ninasikitika sana kutangaza kifo cha gafla cha rafiki yangu wa karibu sana Super Bilionea Seky.

I am speechless Wiki mbili nzima zilizopita mara kwa mara tumekutana Mliman City na Tripple 7 Club mara ya mwisho tulikuwa wote Jumamosi iliyopita mke wake alikuwa anaumwa sana tukaenda wote Baraka Plaza tuka kaa masaa mengi kumsubiria mke wake na leo asubuhi saa tatu.

Tumeongea sana kwenye simu kuhusu viwanjani leo akaniahidi kunipigia back in One Hour twende wapi leo 1 hour ago nimepigiwa Simu kuwa amefariki ghafla Ohh my God bado I am speechless.

Ninamuombea sana mke wake na watoto katika hiki kipindi kigumu sana kwao this one really hurts Binadam tunapita tu hapa Duniani we are just weak creatures of God.

I cry for U Seky a great human being Mungu amuweke mahali pema peponi, please people lets pray for my friand Aimeen le Mutuz"

Pia tujikumbushe mahusiano ya Lulu na Seky yalipoanza, habari juu ya mahusiano yao iliwekwa JF Tarehe 1/4/2014.

Lulu 'Elizabeth Michael', aingia kwenye bifu zito na Miss Tanzania 2012, baada ya kumpora bwana wake
 
Stuli ya kioo? Wap? Nyumbani au?

Alikuwa kwenye hali gan hadi hiyo stuli ivunjike na kumchana hadi umauti?

Kuna taratibu za kulipana insuarence kweli in case mtu amecollapse kwenye hivi vitu virefu? Na haya ma-tiles yanayoteleza kwenye hizi malls ukiteleza ukavunjika kuna ka utaratibu ka kulipwa kweli?

Hatari sana!

Sent from JamiiForums
 
LULU.PNG
 
Maskini Lulu sijui kweli halafu leo siku yake ya kuzaliwa
 
Anajulikana kwa jina la Seky, alikuwa muajiriwa tanzanite one. Kafariki leo inasemekana alikalia stuli ya kioo ikapasuka na kumjeruhi mgongoni.

asante kwa taarifa ya msiba lkn nasikitika kwamba ( title ) ya habari hii imekaa kinafki kwani ingetosha tu kutuambia tukio la umauti wake, jina lake, labda na wasifu wake au kazi yake, lkn c kutuambai aliyekuwa mpenzi au hawara wa ----- tena kwenye title ya taarifa.
huko ni kumdhalilisha marehemu
 
kila mwenza wa lulu anafariki "ghafla" tena kwa kuanguka
 
Hapo lazima ujiulize mara mbili, halafu wote vifo vya ghafla. Seki alikua anafanya Tanzanite one, ana mke na watoto hatareeee
sasa, kama ana mke na watoto, itakuwaje kwenye mirathi ya icho kijacho? hivi wanawake kwanini huwa mnavamia waume za watu?ona sasa.
 
Jamani msimseme vibaya marehemu. Huyo alikuwa mume wa mtu na mkewe ni mwandishi mwajiriwa wa Wizara ya Habari na Utamaduni. Tuchunge ndimi zetu, wafiwa wasingependa kusikia aibu za ndugu yao katika wakati huu wa majonzi.

Ndugu yangu naona unajaribu kuzuia mafuriko kwa mkono... sa hivi hiyo ndio imebaki habari ya midomoni kwa watu...

Mke atalia na mengi kwa wakati huu
 
Back
Top Bottom