Tarehe 17 March 2021, Makamu wa Rais akitangaza kifo cha aliyekuwa rais Ndugu Hayati Magufuli ulikuwa wapi?

P
Peleka unafki wako huko..dhalimu ameondoka unaleta habar za unafki hapa..kama vip kaungane nae..

Mungu alisikia kilio Cha wengi nyie Wachache mliokua mnashirikiana nae mnaleta habar sio..msitumie madaraka kutesa watu,kudhulimu watu,kuua watu...wote ni binadam mavumbini tutarudi!!
 
ok
 
Nilikua Njoss.
Mda huo tumetoka prep...
Nakuta story story. Nikatoka kwenda jidah kuangalia kwa jamaa ambao walikua na simu..
Ndio nakuta Mama anatangaza rasmi
Kumbee wee ni dogo? Yaan 2021 uko Njoss? Ni 5 au 6?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] tunabishana na wanetu wa kuwazaa humu ndani.
 
Nilikuwa nimeshaingia kulala. Mwenza wangu alikuwa sebuleni.
Akaja chumbani fasta akiniambia; dear eti JPM amekufa.!
Alishangaa kuona sikushituka, sikufurahi wala sikusikitika.
Nikaendelea kulala zangu.
 
Nilikuwa home kitandani pamoja na Wife nikiwa naperuzi Twitter, ghafla mtu kwenye group la WhatsApp akapost na kusema Chuma kimekata moto.

Nilishtuka na kutaka kujua ukweli, nikakimbilia JF nikakuta bado uzi hujapandishwa. Nikarudi tena Twitter nikakuta bado watu hawajaanza kupost.

Mara group la darasa WhatsApp mtu akauliza, mumesikia nini TBC, watu wakawa bado hawana taarifa sahihi.

Mimi nikarudi tena JF, ndipo nikakuta uzi ushapanda na nikaconfirm.

Mshtuko wangu ilikuwa ni katika kuutafuta ukweli tu baada ya hapo imekuwa Historia.
 
Ulikua na vyeti feki nini?
 
Dokta upo? Longtime kichizi
 
In Makamba Senior Voice “Wazee sasa tukasema basi…., wazuri hawafi”. Makamba na genge lake ndiyo waliratibu mauaji ya Dkt Magufuli
 
hii iliinikuta nikiwa Nairobi kwa my brother kusalimia, usiku in my bedroom nacheck movie kwa laptop, nikasema wacha niingie insta, wooh nakuta mama kizm kazi yupo live na hudhuni akatangaza kifo cha Rais, i dont know why nilipiga makelele nikafurahi sana hadi nikawagongea kuwatangazia msiba hadi wakashanga nmefurahi mbona?. i hated him yes but now i know i was wrong

but now i miss that man[emoji30] i wish asingeenda aki[emoji26], forgive me Sir if nilikua sikuheshim.
 
Hakika ilikuwa ni huzuni isiyomithilika halafu unakuta kuna wajinga wachache wanasema watu walifurahi


Ukweli unabaki kuwa kifo cha mpendwa Rais wetu JPM kilileta taharuki kubwa mno kwanzaa kwa kuwa cha ghafla mno hapa wale wanaomsoma kigogo na page nyingine za udaku msije kunijibu hapa kujifanya mlikuwa mnajua hapa nawazungumzia maelfu ya watanzania wasiomsoma huyu kigogo wala page za udaku

Pili watanzania walipatwa na mshtuko wa kufiwa na kiongozi mkuu wa nchi kitu ambacho hakijawahi kutokea tangu nchi ipate uhuru

Rekodi mpaka sasa zinaonyesha msiba wa JPM ni moja ya msiba uliotikisa Taifa ndani na nje ya mipaka kama ulivyokuwa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mfano mzuri tumeona juzi msiba wa mwinyi ulikuwa wa kawaidq sana kama wa raia mwananchi wa kawaida wa nanjilinji huko

Binafsi nilipata taarifa asubuhi sa12 baada ya kuamka na kukuta simu yangu ikiwa imepigiwa simu kibao za watu waliopokea taarifa hizo usiku wa sa5 zilipotangazwa na kukiri kwamba hawakulala walikuwa wanalia mpaka panakucha,baada ya kupokea taarifa hizo nililia sana na kuwatafuta wote walionitafuta tukalia pamoja hata TV na redio tunaogopa kuwasha baada ya hapo hata kazini sikwenda na wall hakuna alienitafuta kwamba sijaenda kazini na sio sehemu ya kazi amblyopia haiku strict no lakini nilishangaa nobody alienitafuta

Hakika msiba ulikuwa mzito

Kwa hayo machache kuna kenge zinasema eti walifurahi labda sio watanzania
 
Aisee hii siku nilipata marafiki wapya ambao mpaka leo nipo nao. Sijawahi kufurahia kifo ila hii siku nilicheza sana mziki na nilikunywa bia nyingi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…