Tarehe/siku nzuri kwa mimba kuweza kutungwa


Jan 14.feb 15,march 14
 
Kama umeolewa ningekushauri mshirikiane kwa karibu sana na mume wako. Sio lazima mara zote tatizo liwe kwa mwanamke, kuna nyakati wanaume pia wanaweza kuwa ni/na tatizo katika mchakato mzima wa kurutubisha (fertilize) yai.

Tayari tuna mtoto
 
Reactions: SMU
Ma dou dou safi sana,nakupenda bure jinsi unavyokuwa mwepesi kujibu hoja. Leo leo unapata jibu halafu unaanza mchakato haraka haraka.
 
Madokta wameshaacha mgomo, nenda tu ukawaone moja kwa moja na mume wako mwende nae!, usitanie tatizo kwa kutaka matibabu ya bure hapa!

Mi nadhani humu tunapata ushauri na muda mwingi ni matibabu halisi na sio kwamba watu huwa wakitaka msaada humu huwa hawana pesa za hospital ila kuna wakati mtu anakuwa ameshapita sehemu nyingi tatizo limeshindikana na kwa kuwa hii ni sehemu inayopitiwa na watu wengi waweza kuta kuna mtu alikuwa ana tatizo hili akalipatia ufumbuzi au kuna wataalamu wamo humu pia muda mwingine kama taaluma haikuhusu bora husichangie kuliko kuweka dharau kuwa na lugha ya staha.
 
Jan 14.feb 15,march 14

hizo ni tarehe za kuanzia ama kuishia?
kama ni za kuanzia basi tarehe yako ya kupata mimba itaanza kesho 31 March mpaka 5 April,
Zingatio
a) mnakula vizuri, mnaliwazana na kutoa tress zote huku mkijipa hope kuwa sasa mambo yatakuwa swafi
mwandalie mzee vyakula kama Karanga, mihogo mibichi na vitu vinavyofanana na vivyo

b) Hakuna haja ya kupiga round nyingi zisizo na mpango akishapiga ya kwanza mnatafuta muda wa kupumzika ili mzigo utakao kuja tena uwe na uzito kama ule wa kwanza (Mbegu zinapokuwa nyingi ndivyo chance nayo inakuwa kubwa)

c) Msionenane aibu, NI PM KWA MAELEZO ZAIDI
 
Kama unapata siku zako kama kawaida mshirikishe mwenzio ili kufahamu tatizo liko wapi, unaweza kuta tatizo liko kwake. Mara nyingi watu humwangalia mwanamke kama chanzo cha kutoshika mimba na kusahau kwamba mimba ni matokeo ya watu wawili, ikibidi mwone Daktari ili uwezo wa mbegu zenu uhakikiwe.
 
Reactions: SMU
Tayari tuna mtoto

Najua. Ila kuwa na mtoto mmoja, wawili au zaidi haiguarantee kupata mwengine kwa sababu matatizo yanaweza kuanza muda wowote (eg baada ya mtoto wa kwanza, pili etc) katika maisha iwe kwako au kwa mumeo.

Sisi kwetu tulizaliwa watatu - inagwa najua wazazi walitaka kupata watoto zaidi (kwa miaka hiyo watoto watu walikuwa ni wachache!) lakini hilo halikuwezekana kwa sababu mama yetu alipata tatizo la uzazi baada tu ya mtoto wa tatu.

Ingekuwa hoja ya kwamba kwa sababu tayari mmepata mtoto mmoja then hakuna uwezekano wa mmoja wenu kupata tatizo la uzazi tena then hata hii issue ulioileta hapa isingekuwepo!
 
Ma dou dou kama unapata siku zako kama kawaida basi vuta subira utapata mtoto fresh tu hauna tatizo,zingatia ushauri mzuri uliopewa na baadhi ya wadau humu,kuleni vyakula vyenye virutubisho vingi kwa ajili ya sperm nying na zenye kasi kwa m/me,pia hepukeni mikwaluzano kabisa ktk kipindi hichi cha kusaka mutoto halafu msile gemu kila siku fanyeni kwa zile siku ambazo mnahisi mimba inaweza ikatunga.
 

Dipopuvera
 
hiyo sindano uliyochoma,sometimes inachelewesha kupata mimba.kuna dada namfahamu alichoma hiyo sindano,alikuja kupata uja uzito kwa mara ya 2 baada ya miaka 12
 
Mpenzi wako atakuwa mgumba jaribu kubadili mme uone kama haujadaka.
 
Mshirikishe muumbaji yeye ndo dokta wa Ukweli,sali na fuata ushauri wa madaktari ila punguza stress wakati wa chakula
 
ushauri mzuri ni kuwaona madaktari nadhani utapata msaadaa zaidi
 
Dipopuvera

Dada haya hapa ni maelezo ya sindano uliyotumia kwa kifupi
Depo-Provera
Depo-Provera ni dawa ya uzazi wa mpango kwa njia ya sindano, (kuzuia mimba). Depo-Provera, wakati mwingine pia hutumika kwa ajili ya matibabu ya matatizo mbalimbali ya masuala ya uzazi.
Ina homoni iitwayo medroxyprogesterone ambayo inajulikana kama progestagen,
sindano hii ni kinga dhidi ya mimba kwa kuzuia ovulation (Kutotoka kwa yai katika ovary) . Sindano hii pia hukinga dhidi ya mimba kwa muda wa miezi mitatu kuanzia siku ile ulipochomwa.
Wakati wa kumaliza kwa dozi ya sindano hii ya kuzuia mimba, itachukua muda kabla ovulation na hedhi kuanza tena. Hii ina maana kwamba pia inachukua muda pia kupata mimba. Ni kati ya mwanamke na mwanamke, lakini mara nyingi itakuwa ovulation ianze miezi sita hadi nane baada ya chanjo ya mwisho. kwa hiyo inakubidi uwe na subira. ila ni vizuri kufanya mapenzi na mumeo siku ya 12-17 toka siku unapata hedhi, hii itakuwa rahisi kushika mimba, kwa ni wakati yai linatoka kwenye ovary )ovulation period), na kama mlipumzika kwa mda huo bila mapenzi basi hata mumeo takuwa ametengeneza mbegu za kutosha kukupa mimba. ukiona bado hushiki mimba nenda wewe na mumeo wote mkapime, tatizo la weza pia kuwa kwa mumeo. siku njema na kila la kheri!!!
 

Asante
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…