KERO TARURA Tabora iangalieni Barabara ya Madaraka, ni mbovu na inazidi kuharibika

KERO TARURA Tabora iangalieni Barabara ya Madaraka, ni mbovu na inazidi kuharibika

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
Hivi huu Mkoa wa Tabora viongozi wa Wakala ya Barabara za Mjini na Vijijini TARURA wapo kweli?

Maana Barabara ya Madaraka iliyopo Mtaa wa Madaraka Manispaa ya Tabora imeharibika na inazidi kuharibika kila siku, kuna mashimo lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.

Nimeshuhudia zaidi ya mara nne watu wakinusurika kugongana wakati wakikwepa hayo mashimo kwenye ile barabara hivyo lazima hatua zichukuliwe.

Mvua kwa sasa ni kubwa na yale mashimo yaliyopo kwenye barabara hiyo yanaendelea kujaa maji na kuchimbika zaidi hawa TARURA watimize wajibu wao.

20241207_095122.jpg

20241207_095050(0).jpg

20241207_095051.jpg

20241207_095031.jpg

20241207_095124.jpg
 
Wakati huo mbunge wao mwakasaka yuko daslam na familia yake wanakula maisha.CCM NI LAANA
 
Dah yaan hapo ni mjin kabisa barabara ipo ivo jmn ebu oneni Aibu viongoz wetu jmn
 
Huko Tabora diwani Chadema, Mbunge Chadema, Rais Chadema. Basi hatuleti barabara mkale mlikopeleka mboga
 
Back
Top Bottom