Habari zenu,
Nina mtoto wa kike ambaye kesho, tarehe 13/06/24, anafikisha miaka 11 kamili (Happy birthday in advance my daughter).
Mtoto alizaliwa vizuri ingawa alikunywa maji machafu baada ya kuchelewa kuzaliwa kwa masaa kadhaa. Hii inaweza kuwa ilitokana na mama yake kuwa na msongo wa mawazo (depression) au la, japo haikuonekana kwa wakati huo. Aliendelea vizuri tu, lakini alipofikisha miezi 6 au 9, mama yake alipoingia ndani alimkuta mtoto macho yakiwa kama makengeza. Mama jirani alimwambia macho yatakaa sawa, lakini baada ya wiki moja aliamua kumpeleka hospitali ambapo aliambiwa mtoto alitaka kupata degedege, ila macho yangekaa sawa.
Maisha yaliendelea, lakini mtoto alichelewa kuongea. Tulipata maoni mbalimbali kwamba tatizo lilikuwa ulimi kuwa umeungana kwa chini, hivyo tukampeleka akafanyiwa upasuaji mdogo na akaanza kuongea vizuri. Akiwa na miaka 3, alianza shule ya awali (baby class) na kisha darasa la 1 Montessori pale Msimbazi. Maendeleo hayakuwa mazuri, hivyo nikamuhamishia shule moja Kinondoni na akawa anafanya vizuri.
Hata hivyo, nilipata changamoto za kifedha na ikabidi nimhamishie shule ya English Medium Oysterbay. Alianza vizuri lakini darasa la 4 matokeo yakawa mabaya sana. Mungu mwema alifaulu na sasa yupo shule nyingine, lakini bado matokeo ni mabaya. Pia kuna tabia za ajabu alizonazo licha ya zingine alizokuwa nazo awali.
Anapenda kula maganda ya karanga, anapenda harufu mbaya kama ya kitu kilichooza, na chumvi. Anafanya mambo yasiyoendana na umri wake, na wakati mwingine analia bila sababu au anasema ameona kifo chake. Muhimbili kwenye afya ya akili, daktari wa watoto alisema ni suala la malezi, lakini daktari wa watu wazima alisema kuna shida kidogo pamoja na majibu ya vipimo. Kuna dawa alipewa lakini zilimchanganya kidogo tukaziacha.
Kuna mganga alisema wanamchukua msukule na nimuulize ndoto gani anaota usiku. Alisema anaota anaruka au anakula nyama. Mganga alisema nimpeleke amtibie, lakini sheikh mmoja alisema ana majini na inabidi yatolewe mapema, akanitajia pesa nyingi.
Basi hadi sasa nipo njia panda. Kwa anayejua njia za kumsaidia binti yangu naomba msaada.
Samahani kwa kuwachosha, kusummarize bado ni shida kwangu licha ya kufundishwa darasani. Ila hapa pia nimeandika vingine na kuacha vingine. Nitaviweka inapobidi.
Asanteni.
Nina mtoto wa kike ambaye kesho, tarehe 13/06/24, anafikisha miaka 11 kamili (Happy birthday in advance my daughter).
Mtoto alizaliwa vizuri ingawa alikunywa maji machafu baada ya kuchelewa kuzaliwa kwa masaa kadhaa. Hii inaweza kuwa ilitokana na mama yake kuwa na msongo wa mawazo (depression) au la, japo haikuonekana kwa wakati huo. Aliendelea vizuri tu, lakini alipofikisha miezi 6 au 9, mama yake alipoingia ndani alimkuta mtoto macho yakiwa kama makengeza. Mama jirani alimwambia macho yatakaa sawa, lakini baada ya wiki moja aliamua kumpeleka hospitali ambapo aliambiwa mtoto alitaka kupata degedege, ila macho yangekaa sawa.
Maisha yaliendelea, lakini mtoto alichelewa kuongea. Tulipata maoni mbalimbali kwamba tatizo lilikuwa ulimi kuwa umeungana kwa chini, hivyo tukampeleka akafanyiwa upasuaji mdogo na akaanza kuongea vizuri. Akiwa na miaka 3, alianza shule ya awali (baby class) na kisha darasa la 1 Montessori pale Msimbazi. Maendeleo hayakuwa mazuri, hivyo nikamuhamishia shule moja Kinondoni na akawa anafanya vizuri.
Hata hivyo, nilipata changamoto za kifedha na ikabidi nimhamishie shule ya English Medium Oysterbay. Alianza vizuri lakini darasa la 4 matokeo yakawa mabaya sana. Mungu mwema alifaulu na sasa yupo shule nyingine, lakini bado matokeo ni mabaya. Pia kuna tabia za ajabu alizonazo licha ya zingine alizokuwa nazo awali.
Anapenda kula maganda ya karanga, anapenda harufu mbaya kama ya kitu kilichooza, na chumvi. Anafanya mambo yasiyoendana na umri wake, na wakati mwingine analia bila sababu au anasema ameona kifo chake. Muhimbili kwenye afya ya akili, daktari wa watoto alisema ni suala la malezi, lakini daktari wa watu wazima alisema kuna shida kidogo pamoja na majibu ya vipimo. Kuna dawa alipewa lakini zilimchanganya kidogo tukaziacha.
Kuna mganga alisema wanamchukua msukule na nimuulize ndoto gani anaota usiku. Alisema anaota anaruka au anakula nyama. Mganga alisema nimpeleke amtibie, lakini sheikh mmoja alisema ana majini na inabidi yatolewe mapema, akanitajia pesa nyingi.
Basi hadi sasa nipo njia panda. Kwa anayejua njia za kumsaidia binti yangu naomba msaada.
Samahani kwa kuwachosha, kusummarize bado ni shida kwangu licha ya kufundishwa darasani. Ila hapa pia nimeandika vingine na kuacha vingine. Nitaviweka inapobidi.
Asanteni.