Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Lakini kwa upande mwingine utakuta na yeye kuna madhaifu yako anayabeba! Hivyo jitahidini tu kuvumiliana!
 
Kaka wapo watu sampuli hii..nilikuwa na uncle wangu(sasa marehemu) askari magereza hapo wizarani(mambo ya ndani) alikuwa na utarati/masharti?/maagano?/ratiba? ni mwisho..na alikuwa hachagui mke,mtoto,mjomba,mfanyakazi,walinzi wote lazima kutii..ukimsalimia bila kukaa mguu sawa ni case,ukikaa kwenye kochi ukaegemea nyuma ni case,ndala za bafuni zikipishana ni case,kula wote ni saa moja jioni,kulala wote saa 3 ..ole ole wako uwashe taa usiku na usiwe na sababu za maana utamtambua..
Hii nadhani ni ndoa "bandia"!
<br />
<br />
 

tafuta maana ya logname yangu, utapata jibu
 
Reactions: BAK
We unataka muishi bila kukwaruzana? kukwaruzana ni sehemu ya ndoa na saa zingine mikwaruzano huwa chachu ya kuzidisha mapenzi yenu
 
kuwa mwanume wa vitendo sometimes inasaidia though si simamii violence kama diplomacy inashindwa use other methods of negotiation kama kumpeleka mbele ya wazee, kwasababu ninaimani amefunzwa kwao
 

Nimeshukuru kwa sababu umenisaidia kujua kuwa kumbe tuko wengi. Mimi nina zaidi ya miaka kumi kwenye ndoa na mke wangu hana cha masters wala mtoto wa masters. Afadhali wako anaahidi kubadilika na anajitahidi kubadilika kwa muda mfupi (miezi miwili) kisha anarudi kwenye ile vicious cyle. Lakini kizuri nilichokiona kwenye maelezo yako ni kuwa anaomba msamaha kila mara anapojua kuwa amekukosea. Hili ni jambo zuri kwani inaonesha huwa anakumbuka makubaliano yenu na anajua kuwa amekuudhi.

Kuna wengine huwa hata hilo wazo la kubadilika hawataki kukubali na wanachukulia kuwa unadhani kuwa wanaupungufu. Wengine wanafikia kudhani kuwa umepata mwingine huko nje na unataka kumbadili yeye tabia afanane na yule uliyempata huko nje. Na ukianza huo mjadala wa kubadilika ndio unakuwa chanzo cha ugomvi. Nilichogundua baada ya kuwa "philosopher" kwenye ndoa ni kuwa mwanamke huwa yupo kwenye mission ya kumbadilisha mwanaume afanane na tabia anazopenda yeye na wakati huohuo huwa anajitahidi kubakia na tabia zake zilezile. Ukihitaji mifano zaidi nitakumwagia kwani iko mingi tu.

Siamini kama huyo wako huwa anasahau makubaliano mnayofikia ya kubadilika ila nadhani bado yuko kwenye mission. Solution: keep on reminding her every time she breaks your agreements. Usiwe unalundika matukio ya violations halafu baada ya muda unakuja na orodha ya incidences ambazo amevunja makubaliano yenu.
 
Mwana Kwetu, umeandika mengi na umepata michango mingi kutoka kwa wanaJF. Umeona wengi wamekwambia mkeo ni mke mzuri wanatamani wangekuwa naye japo kuwa kwako unaona ana vijitabia vinavyokukela. Cha msingi wewe usilazimishe abadilike gafla kama upendavyo, na wewe pia yawezekana una vitabia vinavyomuuzi lakini havisemi, hivyo kubalance na yeye anapuuziaa yale unayomwambia.Nenda naye taratibu mkuu atabadilika kuwa +ve na endelea kumshirikisha Mungu pia.

Unalalamika kwa hivyo vitabia vidogo na unasema ulishamfukuza kwa tabia ambazo hajaziacha, Mwana kwetu hujapata wanawake pasua kichwa ungemuona huyo wako ni lulu. Nakushauri na wewe uanze kumkubali mkeo kwa mafanikio yake ya kiofisi na hayo mengine anayofanya vizuri hata hapo nyumbani. Anapata credits nyingi kutoka kwa watu wengine (maofisini) lakini kwa mumewe hajakubalika vyema, hiyo siyo sawa. Hebu mkubali na wewe umwonyeshe mkeo kuwa anaweza huone kama hivyo vitabia havitaisha. Ongea naye kwa utaratibu huyo ni mtu mzima mwenzako na mkeo. Mkiwa mmetulia muonyeshe hizo appreciations kwa yale aliyoyafanya vyema. Atajisikia Vizuru na ni rahisi sana yeye kujirekebisha na kuacha hivyo vitabia vinavyo kuudhi. Nakwambia haya kama mwanandoa pia, wake zetu wanapenda na wanafurahi kama tukiwapa compliments pale zinapostahili, ninaitumia hii technique kwa shemeji yako na mambo ni yanaenda vizuri.

Kama kakosea usiwe unawaka sana, upende kumsikiliza na mkiwa kwenye furaha muulize kwa nini kafanya hilo kosa na umwambie ni jinsi gani unavyohuzunishwa na makosa kama hayo aliyofanya. Anapokusimulia mambo ya ofisi kwake uwe unamsilikiliza na hata kama ulikuwa hutaki kusikiliza hizo story. Anakwambia hayo mambo kwa sababu wewe ndiye mume wake na kama anahitaji msaada mpe, kwa kufanya hivyo utashangaa mambo yanavyokwenda vema.


Usipende pia kukumbushia makosa ya nyuma, kama ulimsamehe basi yapite anza chapter mpya na msonge mbele. Ndoa ina changamoto zake kaka hilo halihepukiki na zinatofautiana uzito/ukubwa. Nyie ni watu wawili tofauti japo Mmeunganishwa kuwa mwili mmoja, hivyo kubali kuwa kufikiri kwako na kwake ni tofauti. Hata mapacha wanaofanan pia hutofautiana kitabia sembuse nyie ambao si wa baba/mma mmoja? Vumilia mwana kwetu, hivyo ni vijimambo vidogo tu, mkeo ni mwili wako mkubali alivyo.
 
Mwana kwetu

Huyu mwanamke kwanza umeshamshtaki kwa wazee wake (wazazi) na hata kwa ndugu zako (mama yako) so umeonyesha yeye ni mtu asiyefaa hana uwezo au ni dhaifu... Mtu ukisham-devalue kiasi hicho kw watu wake wote anakosa raha ya maisha

Ushauri:
1. Usipeleke shauri lolote linalohusu ndoa yenu kwa mtu yoyote zaidi ya nyinyi wawili
2. Lower your expectation usitegemee kwamba atafanya mambo makubwa kama unavyotaka
3. Akifanya chochote dogo appreciate sana..na uonyesha kuwa that is more than enough...
4. mwisho: men angalia je wewe unahusika vipi?
 

Ushauri huu ni wa kiutu uzima na unaonyesha ukomavu wa hali ya juu ;mkuu nakushukuru na mawaidha yako na mengine mengi nitayafanyia kazi kwa kina kwani mimi ni msikivu na pia napenda wazo la upande wa pili ndo maana nimelileta hili hapa jamvini nashukuru sana
 
MWANAKWETUUU..."NYOKA HAFUNDISHWI KONAAAA"

Au mara hii umesahau hiyo signature yako uloweka hapo chiniii..umesahau kunako biblia mwanamke alidanganywa na nyoka??...umesahau kuwa nyoka na akili zake bado alimzidi ujanja mwanamke na kumdanganya kitu alichokatazwa na mungu...kula tunda la mti wa katiii???...NAAMINI NIMEKUKUMBUSHA

UMESEMA KUWA MKEO NA WEWE WOTE NI WASOMI WA AT LEAST MASTERS????...

...ILA HAMJASOMEA MASTERS YA KUKUMBUKA NA KUTEKELEZA MAJUKUMU MADOGO MADOGO YANAYOHATARISHA UWEPO WA NDOA YENU NA KUEPUSHA MIKWARUZANOOOO...

OKKK...NIMEKUMBUKAAA...HIYO MASTERZ HAIPO DUNIANI....SOO MNATAKIWA MURUDI SHULE.."UNIVERSITY OF HARDKNOCKS WANAITOA HIYO MASTERS....HATA HAPA TANZANIA IPO"ELIMU MTAANI DOT COM"...HAPO UTAPATA ELIMU ZOOOTE ZISIZOTOLEWA CHUO CHOCHOTE RASMI DUNIANILASTLY...MAHUSIANO NI ZAIDI YA ELIMU ZA CHUO KIKUU..NDIO MAANA MAMA PROF. TIBAIJUKA KUNAKO MAHUSIANO ANACHEMKA MBAYA KULIKO DADA FATMA YULE BINTI WA MZEE KONDO ALIYEACHISHWA SHULE DARSA LA 3 NA KUOLEWA NA MZEE BASHIR KULE PANGANI TANGA....

TAFAKARI....ISHI NA MKEO/WANAWAKE KWA AKILI.
 
google translate imegoma banaa,sikui kama bakita wataweza. dokeza hata mkoa basi yakhe!
<b><span style="font-family: comic sans ms"><font size="4"><font color="#800080">tafuta maana ya logname yangu, utapata jibu</font></font></span></b>
<br />
<br />
 

Mkuu Tata nashukuru umeniongezea experience na pia kunipa strategy ya nini cha kufanya ili nisikwazike. Kusema kwamba wako kwenye mission ni kweli kwani hata rafiki yangu jirani huwa ana experience ya namna hiyo kwenye marriage yake na tunatofautiana handling procedures kwani haziwezi ku work kwa kila ndoa. Mimi kwenye hii thread kutokana na michango yenu najaribu ku derive formula ili nichukulie hizi tabia positive na nijue kutumia udhaifu wa wife kwa manufaa kuliki violence.
 


AMEN

Babu DC
 


Nakubaliana na wewe 100%
 
Mwongezee asilimia 2 binti wa kazi utaona mabadiliko mara moja.

Inabidi nijipange kwani kumfukuza nitakuwa pia nimetesa watoto wangu ambao obvious hiyo adhabu haiwahusu. Ila pia nitakuwa nafanya tu basi na yeye atakuwa na kazi gani kwani asilimia 98 ya kazi zote anafanya binti wa kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…