Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Huwezi kumbadili mtu tabia, unachoweza ni kumshauri tu, asipobadilika kubali matokeo. Ndio misalaba ya ndoa!
Nakushauri ubadilike wewe kulingana na tabia zake, uzizoee. Otherwise utajisumbua bure.
Masters inamsaidia kazini, nyumbani haifanyi kazi ndo maana kuna wasomi wazuri tu wanazidiwa akili na househelp ambaye hajamaliza darasa la saba
 

...12yrs of marriage, kwakweli nyie ni ndege mfananao,....na kwa kila mapungufu ya mkeo, nawe yako yanamkera vile vile...ila, kwakuwa mnafanana, si rahisi kwako kuona mapungufu yako.




...acha tu bak, yaani we acha tu...lakini kwa mtazamo wangu, huyu bwana anakabiliwa na mid life crisis ambayo
kama kawaida, 'mnyonge' wake ndiye atayekuwa victim wa kumalizia hasira zake. In this case, mkewe maskini ndiye
anayebebeshwa mizigo ya lawama kwa mapungufu yake mwenyewe mwana kwetu.

...kama walivyo alcoholics, chain smokers, sex addicts na drug addicts, hatoweza kujinusuru na kuangamia kwake ila tu atapojikubalisha yeye ana matatizo/mapungufu pia.

...yeye ndiye dereva wa mawazo yake, na hakuna mwingine anayepaswa kulaumiwa ila yeye mwenyewe. kinyume na hapo, nasikitika sana kumsoma mwenzetu mwana kwetu akielekea kwenye shimo...

mwana kwetu, inaniuma sana,...inaniuma sana bro...
mwana kwetu, badilika kabla hujafikia the point of no return.
mrudie mwenyezi mungu, umemuacha sana mwenyezi mungu,
umepoteza muelekeo, umepoteza njia, nyota na nuru yako inafifia...
moyo na roho yako vinazingirwa na giza,...giza ambalo ni ibada tu itayokuokoa.

Kweli mkuu,

Kwa watu ambao tumeishi kwenye ndoa kwa muda mrefu (zaidi ya muongo mmoja), huwezi kutushawishi kwamba hapa mwanamke ana kosa lolote. Nashawishika kuamini kwamba huyo dada ni mvumilivu na mwenye hekima sana.

Inawezekanaje mnaishi na mtu kwenye ndoa kwa amri ya jeshi na kufukuzana + kuwekeana kumbukumbu kwenye mafaili????

Bado sijamwelewa huyu kaka na sina hakika kama yeye mwenyewe anajielewa. Ila akikusikiliza basi atakuwa amepiga hatua kubwa katia direction ya kuokoa ndoa yake!!
 
NIMEELEWA KWA NINI WA TANZANIA TUNA FAIL MITIHANI RAHISI. THREAD YANGU ILITAKA TU JIBU LA SWALI AMBALO LILIHITAJI "NDIYO AU HAPANA" Kama ningeamua kutoa MARKS hapa wachangiaji wote mnge score ZERO kwa sababu hamkulielewa swali ama kutokana na uvivu wa kufikiri au kwa kujidai wajuaji sana.[/QUOTE]

Hahahahahahah......Umenifurahisha sana!!
 
Mkeo usimwonyeshe huu uzi tafadhali. Unaweza ukamtia kiburi next time mkigombana akasema &quot;wewe mkorofi hata JF wamesema!&quot;<br />
<br />
SO puliizi huu ushauri uwe siri yako tekeleza vya kutekeleza vya kuacha viache.<br />
<br />
Hizi comment zina msaada kwako si kwake.
<br />
<br />
Xcellent! Mia mia. Husisubutu kumpa michango ya hoja zote humu, kunaambazo zitaongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulitatua, na ndo'nyingi. "Ondoka na Ngano kwaajili ya ma2mizi yako, makapi yaache humuhumu"
 
NIMEELEWA KWA NINI WA TANZANIA TUNA FAIL MITIHANI RAHISI. THREAD YANGU ILITAKA TU JIBU LA SWALI AMBALO LILIHITAJI "NDIYO AU HAPANA" Kama ningeamua kutoa MARKS hapa wachangiaji wote mnge score ZERO kwa sababu hamkulielewa swali ama kutokana na uvivu wa kufikiri au kwa kujidai wajuaji sana.

Bora hukuwa Mwalimu maana inaelekea ungependa kutunga mitihani ya multiple choice ambayo hata ngedere anaweza kupata 100% pamoja na kuwa hakuwahi kuingia darasani hata siku moja.
 
yah mkuu unaonekana mtu wa prinspo sana by the way nilitaka kuuliza mtu ambaye sijaoa naweza kumshauri au kuwashauri wana ndoa?
 
jaribu yafuatayo

- kumwambia asante mkeo kwa yale mema anayokufanyia
- kumpongeza pale anapotekeleza yale mliyokubaliana
- kutosisitiza mapungufu ya mkeo bali kukoleza yale ambayo unakubaliana naye
- kutojaribu kumlinganisha mkeo na wanawake wengine
(sidhani kama utaona vyemâ mkeo akianza kukulinganisha na wanaume wengine)

kama walivyokueleza baadhi ya wachangiaji huyo mkeo ni lulu inabidi uienzi
kama ambayo anayokuenzi wewe (maelezo yako yanaonyesha kwamba mkeo anakuenzi vilivyo).

miaka 12 ya ndo si mchezo kwa maisha ya sasa nami nawapongeza sana.
 
ndoa ni ya wawili na maombi tu ndio ufunguo wa kila kitu. Hakuna ndoa iliyo na furaha tu na ikose downs. Kaa na mkeo usimwache. Ombea mkeo kila siku. Wengi tumepitia ugumu kama wewe katika ndoa na tuna ndoa zenye furaha kwa uvumilivu na upendo.
 
Nimeona Mwana Kwetu ni mtu mwema tu ila 'kosa' lake ni kutojua mambo ya ndoa nyengine huko hivyo kukosa benchmark.

Kwa vile hana makundi wala magurupu, haya yanayoelezwa kuwa mke huyo ni lulu hayaelewi kwa vile hajui wwnziwe wanaishi na nini. Naamini pia kuwa haamini kwenye kulinganisha na watu wengine vile vile. Anachotaka ni kesi yake kuwa isolated na kuhukumiwa hivyo. Mke hatimizi wajibu wala kutekeleza majukumu, afanyeje? (sio Jibu la kosa Hilo dogo)

Pia napata picha kuwa ni mtu wa principles kwa sana, kuwa wakishakubaliana principle fulani lazima itekelezwe. Mwanamke hawezi principles na hilo Mwana Kwetu linamtatiza

Ningekushauri Mwana Kwetu ulegeze masharti kidogo, for your sake. Kuishi kwa principles ni nzuri kwako Kama wewe tu ndie utakaetakiwa kuzitekeleza, anapolazimika mwengine pia ni ngumu. Huwa anakuahidi kutekeleza kwa sababu anakupenda hataki ukereke na yeye, ila kutekeleza hizo principles considering hajalelewa au kujikuza nazo ni ngumu.

Anakuheshimu anzia hapo. Miezi miwili ya amani kisha unamkumbusha tena asisahau, mnaendelea tena. Pia unaweza kujaribu njia mpya ya kufikisha ujumbe kwake. Mkumbushe pia kuwa wewe ukichukia, inawaathiri watoto hivyo ajitahidi kwa ajili Yao ili wawe na furaha ( kwa mwanamke ni rahisi kuongeza juhudi kwa ajili ya watoto)
 
Mleta mada nimesoma maoni yako mengi hapa na bila kuelezwa ukweli hutapata utatuzi wa suala lako,pia nimezingatia maelezo haya ni ya upande mmoja(labda nae aje kama mke flani hapa na kutoa upande wake).
1.Mawazo yako kuhusu ndoa sio sahihi,
2.Kama mumeishi hivi miaka 12 namsifu mkeo,
3.Huwezi mpangia mkeo kazi/majukumu mnaweza KUPANGA PAMOJA,
4.Kitendo cha kuandika sehemu kitu halafu mkiongea eti unaenda kuleta ushahidi huyu sio MUAJIRIWA WAKO,
5.Hii njia yako umeshaona HAIFAI hebu jaribu kuwa rafiki wa mkeo,
6.Akikosea cheka kidogo na achia hapo-masimango hapana,
7.Ulichompangia afanye yeye kama hajafanya fanya wewe na usikizungumzie-mezea.

Siku zingine mtoe mazingira ya nyumbani,muulize kuhusu kazi yake,muulize kuhusu changamoto anazozikabili,mnunulie zawadi, mletee maua na kadi,wahi nyumbani umpikie mara mojamoja.
 
haya matatizo na dhani wanawake wengi wanayo sijui huwa wanafanya kama hawajui vile au ni kiburi au ni udhaifu wao kweli tujue tunakaa na weza wetu walio wadhaifu sana hasa katika kurudia rudia mliokubaliana yasitendeke au msifanyiane
 
Kaka kama mmevalishana pete usichoke! Nenda naye hivyo hivyo BUT for me kosa KUBWA ni USALITI! Kama hilo nalo huwa analitenda haina haja ya kumvumilia. Unajua anaweza akawa mwepesi sana kuomba msamaha lakini pia angalia na usalama wa maisha yako pia, hasa kwa makosa yanayoweza kusababisha matatizo katika uhai wako!
 
Kitendo cha kuimwaga privacy zako humu ni kosa namba moja ambalo mkeo akijua tayari ni prob. Una masters umeconduct researches nyingi mno za prob solving ktk jamii si tu ktk family including yours. Ushauri...tumia kisomo chako kutatua mambo yako kwa asilimia 80..na 20% waachie JF. Ushauri: women are from venus and men are from mars. Paul mtume alituasa kuwa...enyi wanaume muishi na wake zenu kwa akili maana ni chombo dhaifu...mind you..Paul hakufafanua endapo tusipoishi nao kwa akili itakuaje...nadhani itakuwa kama mnavyoishi. Msome mtu wako dislikes zake zote then ucop nazo..kwani kutaka kuombwa msamaha kila siku anafeel mtumwa. Na wewe usipende kujali issues ndongox2 potezea tu zote ajione mshindi wakati unatafuta sln ya kudumu. Mlioana bila kusomana tabia na hilo wanalo wasomi wengi kwamba maadam wote tumesoma basi mambo yatakuwa mswano economically na socially...si kweli kwani tabia mbaya ama nzuri haijengwi na kisomo bali hujengwa na Mungu. Bwana asipoilinda ama kuijenga nyumba waijengao/wailindao wafanya kazi/wakesha bure. Unasali lkn au hata Mungu mlishampiga chini kwa kuamini masters? Jishusheni mkwezwe...masters is nothing ktk mapenzi...mahusiano
 
Nilishamfukuza huyu wife mara mbili na hayuko tayari kuondoka na kuliko aende kwao ataenda kwa mama yangu kumpigia magoti ili anishawishi nimrudishe . Akiwa kwa mama humwomba mama anipigie simu kuniomba msamaha na anaweza akakaa kwa mama hata siku tatu na huwa inabidi nimheshimu mama yangu basi namkubalia.

Unavuruga wewe mwenyewe!!Inaelekea una uboss fulani kwenye mahusiano yenu.Jirekebishe kama unataka kusahihisha tabia hizo kwa mkeo.

Wewe unapomkosea "anakufukuza"?....na unampigia magoti nani ili akusamehe? Wanaume wenye uboss kwenye ndoa hakuna rangi wanaacha kuona... na mwanamke hataondoka ng'ooo!
 
Hii ni miongoni mwa threads ambazo naamini watu wakiondoa maneno na vijembe vya hapa na pale inawez akuwa na msaada mkubwa sana kwa wengi wetu.

a. Je elimu ni muhimu sana kwa mafanikio ya ndoa?
b. Je mtu anaweza kubadilika tabia yake?
c. Je, mwanamme anaweza kumwamulia mwanamke (hata mkewe) kitu na kutaka afanye?
d. Je, katika ndoa nani ana kauli ya mwisho na kwa nini? Inakuwaje kama kauli ya mwisho inaonekana haina mantiki?
e. Je, kumpenda mtu kuna maana gani hasa? Kupenda anapokuwa na tabia nzuri tu za kupendeza na akiwa na kasoro ambazo unajua ni za kudumu upendo nao huisha?

Jibu langu kwa ufupi kwa ndugu yangu hapa ni kuwa:

a. Umeshajua kuwa mkeo habadiliki na hahawi unavyotarajia basi uamuzi wa kwanza ni kukubali ukweli huo. USIWEKE NAYE MAAGANO! Agano uliloweka naye wakati wa ndoa ndio hilo lilnamfunga! Sijui ulikula kiapo gani lakini kama ulikula kile cha "till death do us part" na chenye "for better or for worse" basi kweli ndiyo the "worse" mpende na mzidishie upendo

b. Acha kumlaumu na kumkumbusha mapungufu yake. Believe me it will change her. Hakuna mtu anayependa kusimuliwa mapungufu yake au kila akishindwa "unaona hata wakati ule... " au "jamani msomi wewe hata hili unashindwa?".. n.k!

mengine nayaachilia hapa.
 
Mnaochangia mmeoa au mnachangia tu kwa uzoefu wa kusoma kwenye vitabu vya udaku.? Kuanzia wadhamini nimewaeleza na walishachoka kumweleza na wakasema hatuwezi kuongea na sikio la kufa. wazazi wake walishamwambia na kumwonya na kumfunda mara ya pili na wakaniomba nirudi kukaa naye akileta shida niwaambie tena . Hii ndo ni mojawapo ya sababu kuwa hathubutu kabisa kwenda kwao nikimfukuza. NINGEKUWA MI NINA MATATIZO HAWA MASHAHIDI WOTE INCLUDING WAZAZI WAKE TENA WENYE UWEZO WASINGEMWONYA NA KUMWEKA KIKAO.


Sasa anakung'ang;ania nini kama wewe ndio uko na attitude mbaya hivi kumhusu?
Kwa uzoefu tu, wanawake hung'ang;ania ndoa kwa sababu zifuatazo:
1. Pamoja na matatizo kwenye ndoa, unakuta mume bado ana mapenzi makubwa sana na mkewe hata kama kuna ukorofi ( sijakusoma nikasikia una sifa hii)
2.Mwanaume hataki mke aondoke hata kama mwanamke keshachoka na hii hutokana na kukwepa gharama za kuachana ( wewe unamfukuza kienyeji hivyo humkatalii kuondoka)
3. Mwanamke hana pa kwenda kwa maana anakutegemea kuliko alivyowategemea wazazi wake ( huyu wa kwako ana kazi nzuri, kipato, wazazi wenye uwezo)
4. Watoto ( hujasema kama anawang'ang'ania watoto)
Sasa wewe una nini hadi umuone mkeo hafai hadi ulete maneno ya ndoa yenu hapa?
 
Katika kipindi cha miaka 12 ktk ndoa yangu nimegundua tatizo kubwa sana la mke wangu ambalo kwa ufupi ni chanzo kikubwa cha migogoro ktk ndoa yetu. Nimegundua kuwa wife wangu ni vigumu ku keep maagano au makubaliano consistently bila kuvunja. Kwa mfano mnakuta mmekubaliana kwamba tabia au mambo fulani ndani ya ndoa hupendi au yanaleta kero na ugomvi hivyo mke wangu anakubali kabisa kwamba nitaacha sitarudia tena kwani najua nakuudhi" Vivyo hivyo na mimi mume nakubaliana na wife kwamba zile tabia zangu ambazo ni kero kwake nitaacha for good. Huwa nakuwa mwaminifu na nimeacha silika zinazomfanya mke wangu achukie na kukosa amani for her sake.

Mimi nilidhamiria na nimefanikiwa kuacha kabisa vitabia ambavyo ni kero na chanzo cha migogoro na wife kwani sipendi niwe chanzo cha kumfanya wife uncomfortable.

Cha ajabu ni kwamba yeye wife amekuwa na vicious cycle ya kuvunja maagano na maazimio kwa kurudia rudia mambo ambayo ni kero kwangu. Pamoja na kwamba sote ni wasomi kwa level ya Masters inanipa shida kumwelewa ni kwa bahati mbaya au ni kwa makusudi anafanya anapoamua kurudia rudia tabia zinazo nikera. Ukimwuliza kwa nini umevunja makubaliano huwa mbishi na no apology na kuna uwezekano wa escalation ya ugomvi. Hii inanipa shida sana kwani huwa nataka tukikubaliana basi I keep promise kama ninavyomfanyia lakini never.
Uwezo wake wa ku maintain ahadi hauzidi miezi miwili hata kama last time ugomvi ulikuwa mkubwa kiasi gani.

Kinachonishangaza zaidi ni kwamba huyu wife kazini kwake kote alikiofanya kazi anasifiwa kwa kufanya vizuri iwe yuko na bosi mwanamke au mwanaume. Najiuliza kichwa hichohicho kinashindwaje kufanya hivyo hivyo nyumbani kisifiwe na husband?
Huyu wife ni mwepesi wa kukiri kosa na kuomba msamaha ila ndo hivyo anarudia tena.
Naomba kuwauliza mlioko kwenye ndoa je tatizo hili ni la wanawake wote au ni mke wangu tu analo? Na je solution yake nini kwani nimetumia uwezo wangu wote kumwelewesha anavyosababisha ugomvi kwenye marriage bado anaonekana kusahau wiki chache baada ya ugomvi? .

Mtoa mada kwanza kabisa nashukuru na kukupongeza kwa mada yako ambayo kusema ukweli kwa wengi wetu imetufungua akili kwa kiasi kikubwa. Nafikiri tatizo unalolirefer kwa mkeo au wanawake liko pia kwa wanaume. Kuna wanaume ambao wana tabia kama uliyoisimulia hapo kuwa mkeo anayo. So kwanza nikuweke sawa tu kuwa si wanawake pekee wanaoweza kuwa na tabia kama hiyo bali pia wapo wanaume.

Pili hapo kwenye rangi kidogo sijakuelewa vizuri, umesema ukimwuliza anakuwa mbishi and no apology but at the same time ni mwepesi sana wa kukiri kossa na kuomba msamaha....kidogo inanichanganya.
But all in all kumbuka kuwa kwenye ndoa kuna sacrifaces, kuchukuliana na kuvumiliana. Umeshaujua udhaifu wa mwenzi wako kwa muda mrefu sasa ilikupasa uwe umeshajiadjust katika kuyakubali mapungufu yake na kujitengenezea kaji"bullet proof" kako ili kuepusha migongano ya mara kwa mara na si kumlazimisha au kung'ang'ania mkeo abadilike. Ilimradi hayo mapungufu yake haya'hatarishi' usalama wa afya ya ndoa yenu mfano kama anacheat, unamfumania unamkanya na kisha anarudia, hilo ni kosa nitakuelewa but kama anachelewesha chakula; anachelewa akienda kwa mashoga zake au anapenda sana kwenda saluni- hivyo ni vitu vidogo ambavyo ni kujipanga tu namna ya kumuaccomodate kwani ndo kilema chake but not kumlazimisha abadilike kwa kuwa hutokuwa unamtendea haki kumfanya aishi vile unavyotaka wewe kwa kusacrifice hata vitu ambavyo kwake vinampa furaha and yet they are not that harmful to your marriage.

But kumbuka pia kuwa ukiona kwako kunaungua, basi jua kwa mwingine kunawezakuwa kunateketea kabisa. kila mtu akiweka hapa mapungufu ya spouse wake hapa nadhani tunawezajikuta wanaJF wote tunakutana makanisani kutoa sadaka za kushukuru kwa kuwapata wenzi tulio nao.
 
Back
Top Bottom