Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Huwezi kumbadili mtu tabia, unachoweza ni kumshauri tu, asipobadilika kubali matokeo. Ndio misalaba ya ndoa!
Nakushauri ubadilike wewe kulingana na tabia zake, uzizoee. Otherwise utajisumbua bure.
Masters inamsaidia kazini, nyumbani haifanyi kazi ndo maana kuna wasomi wazuri tu wanazidiwa akili na househelp ambaye hajamaliza darasa la saba
 

Kweli mkuu,

Kwa watu ambao tumeishi kwenye ndoa kwa muda mrefu (zaidi ya muongo mmoja), huwezi kutushawishi kwamba hapa mwanamke ana kosa lolote. Nashawishika kuamini kwamba huyo dada ni mvumilivu na mwenye hekima sana.

Inawezekanaje mnaishi na mtu kwenye ndoa kwa amri ya jeshi na kufukuzana + kuwekeana kumbukumbu kwenye mafaili????

Bado sijamwelewa huyu kaka na sina hakika kama yeye mwenyewe anajielewa. Ila akikusikiliza basi atakuwa amepiga hatua kubwa katia direction ya kuokoa ndoa yake!!
 
 
<br />
<br />
Xcellent! Mia mia. Husisubutu kumpa michango ya hoja zote humu, kunaambazo zitaongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulitatua, na ndo'nyingi. "Ondoka na Ngano kwaajili ya ma2mizi yako, makapi yaache humuhumu"
 

Bora hukuwa Mwalimu maana inaelekea ungependa kutunga mitihani ya multiple choice ambayo hata ngedere anaweza kupata 100% pamoja na kuwa hakuwahi kuingia darasani hata siku moja.
 
yah mkuu unaonekana mtu wa prinspo sana by the way nilitaka kuuliza mtu ambaye sijaoa naweza kumshauri au kuwashauri wana ndoa?
 
jaribu yafuatayo

- kumwambia asante mkeo kwa yale mema anayokufanyia
- kumpongeza pale anapotekeleza yale mliyokubaliana
- kutosisitiza mapungufu ya mkeo bali kukoleza yale ambayo unakubaliana naye
- kutojaribu kumlinganisha mkeo na wanawake wengine
(sidhani kama utaona vyemâ mkeo akianza kukulinganisha na wanaume wengine)

kama walivyokueleza baadhi ya wachangiaji huyo mkeo ni lulu inabidi uienzi
kama ambayo anayokuenzi wewe (maelezo yako yanaonyesha kwamba mkeo anakuenzi vilivyo).

miaka 12 ya ndo si mchezo kwa maisha ya sasa nami nawapongeza sana.
 
ndoa ni ya wawili na maombi tu ndio ufunguo wa kila kitu. Hakuna ndoa iliyo na furaha tu na ikose downs. Kaa na mkeo usimwache. Ombea mkeo kila siku. Wengi tumepitia ugumu kama wewe katika ndoa na tuna ndoa zenye furaha kwa uvumilivu na upendo.
 
Nimeona Mwana Kwetu ni mtu mwema tu ila 'kosa' lake ni kutojua mambo ya ndoa nyengine huko hivyo kukosa benchmark.

Kwa vile hana makundi wala magurupu, haya yanayoelezwa kuwa mke huyo ni lulu hayaelewi kwa vile hajui wwnziwe wanaishi na nini. Naamini pia kuwa haamini kwenye kulinganisha na watu wengine vile vile. Anachotaka ni kesi yake kuwa isolated na kuhukumiwa hivyo. Mke hatimizi wajibu wala kutekeleza majukumu, afanyeje? (sio Jibu la kosa Hilo dogo)

Pia napata picha kuwa ni mtu wa principles kwa sana, kuwa wakishakubaliana principle fulani lazima itekelezwe. Mwanamke hawezi principles na hilo Mwana Kwetu linamtatiza

Ningekushauri Mwana Kwetu ulegeze masharti kidogo, for your sake. Kuishi kwa principles ni nzuri kwako Kama wewe tu ndie utakaetakiwa kuzitekeleza, anapolazimika mwengine pia ni ngumu. Huwa anakuahidi kutekeleza kwa sababu anakupenda hataki ukereke na yeye, ila kutekeleza hizo principles considering hajalelewa au kujikuza nazo ni ngumu.

Anakuheshimu anzia hapo. Miezi miwili ya amani kisha unamkumbusha tena asisahau, mnaendelea tena. Pia unaweza kujaribu njia mpya ya kufikisha ujumbe kwake. Mkumbushe pia kuwa wewe ukichukia, inawaathiri watoto hivyo ajitahidi kwa ajili Yao ili wawe na furaha ( kwa mwanamke ni rahisi kuongeza juhudi kwa ajili ya watoto)
 
Mleta mada nimesoma maoni yako mengi hapa na bila kuelezwa ukweli hutapata utatuzi wa suala lako,pia nimezingatia maelezo haya ni ya upande mmoja(labda nae aje kama mke flani hapa na kutoa upande wake).
1.Mawazo yako kuhusu ndoa sio sahihi,
2.Kama mumeishi hivi miaka 12 namsifu mkeo,
3.Huwezi mpangia mkeo kazi/majukumu mnaweza KUPANGA PAMOJA,
4.Kitendo cha kuandika sehemu kitu halafu mkiongea eti unaenda kuleta ushahidi huyu sio MUAJIRIWA WAKO,
5.Hii njia yako umeshaona HAIFAI hebu jaribu kuwa rafiki wa mkeo,
6.Akikosea cheka kidogo na achia hapo-masimango hapana,
7.Ulichompangia afanye yeye kama hajafanya fanya wewe na usikizungumzie-mezea.

Siku zingine mtoe mazingira ya nyumbani,muulize kuhusu kazi yake,muulize kuhusu changamoto anazozikabili,mnunulie zawadi, mletee maua na kadi,wahi nyumbani umpikie mara mojamoja.
 
haya matatizo na dhani wanawake wengi wanayo sijui huwa wanafanya kama hawajui vile au ni kiburi au ni udhaifu wao kweli tujue tunakaa na weza wetu walio wadhaifu sana hasa katika kurudia rudia mliokubaliana yasitendeke au msifanyiane
 
Kaka kama mmevalishana pete usichoke! Nenda naye hivyo hivyo BUT for me kosa KUBWA ni USALITI! Kama hilo nalo huwa analitenda haina haja ya kumvumilia. Unajua anaweza akawa mwepesi sana kuomba msamaha lakini pia angalia na usalama wa maisha yako pia, hasa kwa makosa yanayoweza kusababisha matatizo katika uhai wako!
 
Kitendo cha kuimwaga privacy zako humu ni kosa namba moja ambalo mkeo akijua tayari ni prob. Una masters umeconduct researches nyingi mno za prob solving ktk jamii si tu ktk family including yours. Ushauri...tumia kisomo chako kutatua mambo yako kwa asilimia 80..na 20% waachie JF. Ushauri: women are from venus and men are from mars. Paul mtume alituasa kuwa...enyi wanaume muishi na wake zenu kwa akili maana ni chombo dhaifu...mind you..Paul hakufafanua endapo tusipoishi nao kwa akili itakuaje...nadhani itakuwa kama mnavyoishi. Msome mtu wako dislikes zake zote then ucop nazo..kwani kutaka kuombwa msamaha kila siku anafeel mtumwa. Na wewe usipende kujali issues ndongox2 potezea tu zote ajione mshindi wakati unatafuta sln ya kudumu. Mlioana bila kusomana tabia na hilo wanalo wasomi wengi kwamba maadam wote tumesoma basi mambo yatakuwa mswano economically na socially...si kweli kwani tabia mbaya ama nzuri haijengwi na kisomo bali hujengwa na Mungu. Bwana asipoilinda ama kuijenga nyumba waijengao/wailindao wafanya kazi/wakesha bure. Unasali lkn au hata Mungu mlishampiga chini kwa kuamini masters? Jishusheni mkwezwe...masters is nothing ktk mapenzi...mahusiano
 

Unavuruga wewe mwenyewe!!Inaelekea una uboss fulani kwenye mahusiano yenu.Jirekebishe kama unataka kusahihisha tabia hizo kwa mkeo.

Wewe unapomkosea "anakufukuza"?....na unampigia magoti nani ili akusamehe? Wanaume wenye uboss kwenye ndoa hakuna rangi wanaacha kuona... na mwanamke hataondoka ng'ooo!
 
Hii ni miongoni mwa threads ambazo naamini watu wakiondoa maneno na vijembe vya hapa na pale inawez akuwa na msaada mkubwa sana kwa wengi wetu.

a. Je elimu ni muhimu sana kwa mafanikio ya ndoa?
b. Je mtu anaweza kubadilika tabia yake?
c. Je, mwanamme anaweza kumwamulia mwanamke (hata mkewe) kitu na kutaka afanye?
d. Je, katika ndoa nani ana kauli ya mwisho na kwa nini? Inakuwaje kama kauli ya mwisho inaonekana haina mantiki?
e. Je, kumpenda mtu kuna maana gani hasa? Kupenda anapokuwa na tabia nzuri tu za kupendeza na akiwa na kasoro ambazo unajua ni za kudumu upendo nao huisha?

Jibu langu kwa ufupi kwa ndugu yangu hapa ni kuwa:

a. Umeshajua kuwa mkeo habadiliki na hahawi unavyotarajia basi uamuzi wa kwanza ni kukubali ukweli huo. USIWEKE NAYE MAAGANO! Agano uliloweka naye wakati wa ndoa ndio hilo lilnamfunga! Sijui ulikula kiapo gani lakini kama ulikula kile cha "till death do us part" na chenye "for better or for worse" basi kweli ndiyo the "worse" mpende na mzidishie upendo

b. Acha kumlaumu na kumkumbusha mapungufu yake. Believe me it will change her. Hakuna mtu anayependa kusimuliwa mapungufu yake au kila akishindwa "unaona hata wakati ule... " au "jamani msomi wewe hata hili unashindwa?".. n.k!

mengine nayaachilia hapa.
 


Sasa anakung'ang;ania nini kama wewe ndio uko na attitude mbaya hivi kumhusu?
Kwa uzoefu tu, wanawake hung'ang;ania ndoa kwa sababu zifuatazo:
1. Pamoja na matatizo kwenye ndoa, unakuta mume bado ana mapenzi makubwa sana na mkewe hata kama kuna ukorofi ( sijakusoma nikasikia una sifa hii)
2.Mwanaume hataki mke aondoke hata kama mwanamke keshachoka na hii hutokana na kukwepa gharama za kuachana ( wewe unamfukuza kienyeji hivyo humkatalii kuondoka)
3. Mwanamke hana pa kwenda kwa maana anakutegemea kuliko alivyowategemea wazazi wake ( huyu wa kwako ana kazi nzuri, kipato, wazazi wenye uwezo)
4. Watoto ( hujasema kama anawang'ang'ania watoto)
Sasa wewe una nini hadi umuone mkeo hafai hadi ulete maneno ya ndoa yenu hapa?
 

Mtoa mada kwanza kabisa nashukuru na kukupongeza kwa mada yako ambayo kusema ukweli kwa wengi wetu imetufungua akili kwa kiasi kikubwa. Nafikiri tatizo unalolirefer kwa mkeo au wanawake liko pia kwa wanaume. Kuna wanaume ambao wana tabia kama uliyoisimulia hapo kuwa mkeo anayo. So kwanza nikuweke sawa tu kuwa si wanawake pekee wanaoweza kuwa na tabia kama hiyo bali pia wapo wanaume.

Pili hapo kwenye rangi kidogo sijakuelewa vizuri, umesema ukimwuliza anakuwa mbishi and no apology but at the same time ni mwepesi sana wa kukiri kossa na kuomba msamaha....kidogo inanichanganya.
But all in all kumbuka kuwa kwenye ndoa kuna sacrifaces, kuchukuliana na kuvumiliana. Umeshaujua udhaifu wa mwenzi wako kwa muda mrefu sasa ilikupasa uwe umeshajiadjust katika kuyakubali mapungufu yake na kujitengenezea kaji"bullet proof" kako ili kuepusha migongano ya mara kwa mara na si kumlazimisha au kung'ang'ania mkeo abadilike. Ilimradi hayo mapungufu yake haya'hatarishi' usalama wa afya ya ndoa yenu mfano kama anacheat, unamfumania unamkanya na kisha anarudia, hilo ni kosa nitakuelewa but kama anachelewesha chakula; anachelewa akienda kwa mashoga zake au anapenda sana kwenda saluni- hivyo ni vitu vidogo ambavyo ni kujipanga tu namna ya kumuaccomodate kwani ndo kilema chake but not kumlazimisha abadilike kwa kuwa hutokuwa unamtendea haki kumfanya aishi vile unavyotaka wewe kwa kusacrifice hata vitu ambavyo kwake vinampa furaha and yet they are not that harmful to your marriage.

But kumbuka pia kuwa ukiona kwako kunaungua, basi jua kwa mwingine kunawezakuwa kunateketea kabisa. kila mtu akiweka hapa mapungufu ya spouse wake hapa nadhani tunawezajikuta wanaJF wote tunakutana makanisani kutoa sadaka za kushukuru kwa kuwapata wenzi tulio nao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…