Tatizo la Gonjwa la Sukari (Diabets Mellitis): Fahamu chanzo, aina na ushauri wa tiba ya tatizo hili

Ndicho nilichoandika mkuu,kuwa 1DM huwapata watoto,vijana lakini nimemjibu mrs milas kuwa hutokana na kurithi(genes),virusi, maziwa ya ng'ombe na baadhi ya madawa kama alivochangia carcinoma
Asante mkuu kuna aliyesema Type 1 hutokana na ulaju mmbovu ndiyo maana.
 
Wakuu habar za jioni, naomba msaada iwapo kuna tiba mbadala ya kisukar.
Nina ndugu yangu anaugua alipoenda kupima hospital akaambiwa ni kisukari kipo katika hatua za mwanzo.
Naomba msaada wenu kabla hakijafika hatua nyingine, asanten sana.
 
Chukua magome ya mti wa mzambarau kiasi cha 1kg. Chemsha kwenye maji lita 10 kwa moto wa kuni au gesi(namaanisha moto mkali ichemke haraka na kwa kasi) kwa dk 15. Epua chuja ihifadhi hiyo dawa. Anywe glass ya kahawa kutwa mara 3 mpaka dawa iishe. Wakati akiendelea na tiba awe anapima mara kwa mara.
Pia aonane na Dr apewe utaratibu wa vyakula anavyotakiwa kula na anavyotakiwa aviepuke.

Pia afanye mazoezi apunguze uzito na kama ana kitambi afanye bidii kukipunguza.

Pole kwa kuuguliwa mkuu
 
 
Yeye ameomba tiba mbadala,nimemuelekeza wewe unasema ni kama ya babu wa loliondo.
 
Asante sana mkuu nitaifanyia kazi hii tiba
 
Asante sana mkuu nashukuru nitaifanyia kazi
 
Wakuu habar za jioni, naomba msaada iwapo kuna tiba mbadala ya kisukar.
Nina ndugu yangu anaugua alipoenda kupima hospital akaambiwa ni kisukari kipo katika hatua za mwanzo.
Naomba msaada wenu kabla hakijafika hatua nyingine, asanten sana.
Alipopima ilikuwa kiasi gani?
 
Kufanya mazoezi na kubadili ulaji wa chakula ndiyo mikado mbadala kuu
Asante sana kwa ushauri, naomba unishauri kwenye ulaji hapo ale vyakula vya aina gani na vipi aviepuke
 
Asante sana kwa ushauri, naomba unishauri kwenye ulaji hapo ale vyakula vya aina gani na vipi aviepuke
Kupunguza vyakula vya wanga yaani wali, ugali, mihogo, viazi, majimbi au viazi vitamu na kula zaidi matunda na mboga mboga. kama ni wali na maharage anaweza kuweka kwenye sahani vijiko viwili/vitatu vya wali na kujazia na maharage, au kabachi pia akumbuke kunywa maji angalu lita mbili kwa siku.
 
Ilikuwa 17
Hiyo siyo mbaya sana...kuna mtu aliwahi kusema jirani na hosp ya CCBRT kuna kliniki ya sukari ambapo wanatoa ushauri na kukuelekeza namna ya kubalance hivyo hivyo vyakula vya kawaida na kuishusha sukari bila sawa...
 
Asante sana kwa ushauri, naomba unishauri kwenye ulaji hapo ale vyakula vya aina gani na vipi aviepuke
Apunguze au aache kabisa ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na chumvi nyingi....aachane kabisa na soda aina zoteee...asijifariji kwa sijui zero...awe mtu wa kutumia chakula kiasi kidogo ila mara kwa mara...mazoezi siyo lazima yale ya gym...anaweza kutembea tu kwa nusu saa
 
Shukrani ubarikiwe kwa msaada wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…