Tatizo la kuota vinyama ukeni

uludodi

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2014
Posts
576
Reaction score
915
Nina ndugu yangu ni mwanamke na ni mjamzito tatizo lake vimeota vinyama ndani ya uke.

Bado hajaenda hospital kupima mimi nimeamua kuleta kwanza humu mnipe ushauri kabla ili nimwelekeze aanzie wapi?

je kuna dawa ya kutibu anaweza kununua au ni lazima hospital
NB.vimeota ndani ya uke.
Nitashukuru kwa michango yenu JF doctor.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aende kwa gynecology haraka iwezekanyo.
Ni vipi hadi sasa hajamuambia daktari wake siku anazo hudhuria clinic ya wajawazito?
 
Havina mda mlefu na mda wa kwenda krinik bado alichotaka kujua kama vinatibika kabla hajaenda hospital

Sent using Jamii Forums mobile app
Dokta akiviona ndio atasema kama vinatibika au havitibiki. Hapa watakupa majibu batili na ya kukutisha au kukukejeli na matusi sababu hata doktari waliopo humu jukwaani hawajaona hivyo vinyama hawawezi kupiga ramli.
 

Hizo mkuu zinaweza kua hali ya kawaida kama hakuna maumivu wala harufu inayosikika inasababishwa na mimba kupelekea mishipa ya damu kuvimba
Ni hali ya kawaida kama hakuna harufu maumivu yeyote
Ila zaidi ya hapo ni vema kumuona daktari
 
Kama umeshindwa kuweka picha tuone vikoje basi uende hospital kwanza. Au unataka tuanze kupiga ramli? Hivi Wa Tanzania tukoje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kungekuwa hata na kapicha kabisa nadhani sisi madoctor tungejua tuanzie wapi
 
Kuna vitu ni ngumu sana kutoa ushauri hasa kuhusu afya ya mwili. Maana utaombwa picha uone ni dharau lakini hata ukifika kwa dokta naye anataka kuona. Heri uende hospital tu .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ivi ni utahira wa aina gani una tatizo la afya sehemu za siri badala uende hospitali unaleta umbea uku , sasa mfano mtu akataja dawa flan upake , unajuaje aliyekupa huo ushaur ni daktar na iyo dawa haina madhara?

Tuache kutokua serious kwa vitu vya msingi kama afya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ni mpuuzi sana hii ni medical case na uache kumdhalilisha ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa sasa wewe unaingiaje hapo sirini ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mficha maradhi mautu humuumbua, wewe mwone mjinga lakini mwisho wa siku kuna watakaochukulia mzaha na kujibu kwa kejeli, kuna mwingine atajifanya anafuata ethics kama wewe na mgojwa hajapata jibu lakini kuna wengine ni wataalamu ama wamewahi kukumbwa na tatizo kama hilo, ama ni madaktrari bingwa wa hospitali ama ni madaktari bingwa wa kienyeji wakamwonyesha njia ambayo atapitia kiulaini akaliondoa tatizo la ndugu yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…