Tatizo la kutokuona mbali (Myopia)

Tatizo la kutokuona mbali (Myopia)

George Betram

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2015
Posts
4,672
Reaction score
6,272
Habari zenu wanajukwaa nimekua na tatizo la kuona mbali kwa muda mrefu sana,tatizo lililopelekea nitumie miwani ya macho kama kisaidizi cha kuniwezesha kuona vizuri.

Nalichukia hili tatizo maana linanifanya nishindwe kutimiza ndoto zangu nimejitahidi kula karoti na mchicha kama nilivyoelekezwa na baadhi ya watu,lakini sioni mabadiliko hivi ni kweli hili tatizo halina tiba..?
 
Nafikiri halina tiba
Mimi nina miaka kadhaa navaa miwani,na bila miwani siwezi kabisa
Huwa naivua nikilala ama nikienda kuoga tu

Kuna mbaba alinambia tatizo la kutoona mbali linaeza kutibiwa/kupungua kwa kuamka asubuhi na kuangalia majani/maua ya kijani kila siku kwa nusu saa...nilishindwa
 
Umbali gani huo mpaka unashindwa kutimiza ndoto zako???
 
Nafikiri halina tiba
Mimi nina miaka kadhaa navaa miwani,na bila miwani siwezi kabisa
Huwa naivua nikilala ama nikienda kuoga tu

Kuna mbaba alinambia tatizo la kutoona mbali linaeza kutibiwa/kupungua kwa kuamka asubuhi na kuangalia majani/maua ya kijani kila siku kwa nusu saa...nilishindwa
Ngoja na Mimi nijaribu hiyo.
Lakini kwanini ulishindwa..?
 
Nilikua na hilo tatizo nikatafuta dawa weeee nikachoka,nikala karoti kama sungura lakini wapi!
Mwisho wa siku hua natembea na miwani yangu nikitaka kuangalia vitu vilivyo mbali navaa lakini nikiwa natembea kawaida tu sivai ni mpaka nitake kuona mbali ambapo image ya hiyo object inakue bruised
 
Nilikua na hilo tatizo nikatafuta dawa weeee nikachoka,nikala karoti kama sungura lakini wapi!
Mwisho wa siku hua natembea na miwani yangu nikitaka kuangalia vitu vilivyo mbali navaa lakini nikiwa natembea kawaida tu sivai ni mpaka nitake kuona mbali ambapo image ya hiyo object inakue bruised
Ahahaaaaah...
Hatari sana...
Sasa mkuu haupishani na watu unaowafahamu njiani bila kuwasalimia kweli..?
Maana mimi kuna kipindi nilikua nafanya kama wewe,cases za kuwapita watu njiani bila kuwasalimia zikawa nyingi sana,ikanibidi niwe naivaa kila muda(isipokua nikiwa nyumbani tu)..!
Pia nafikiri kushika miwani mkononi au kuiweka mfukoni inaleta usumbufu kidogo..!
 
Pia kuna kipindi miwani yangu ilipasuka...
Nilipokwenda hospital kupima kwaajili ya kutengenezewa miwani mingine nikakuta namba ya lenzi imebadilika(tatizo la kutokuona mbali limeongezeka)...
Daktari akaniuliza kama huwa navaa miwani muda wote au sivai muda wote..!?
Nikamwambia huwa navaa nikiwa darasani na nikiwa naangalia TV tu..!
Daktari wa macho akanambia natakiwa kuvaa miwani muda wote,coz nisipofanya hivyo tatizo litakua linaongezeka kidogo kidogo,hivyo itanilazimu kubadili lenzi mara kwa mara..!
HAKUNAMATATA
 
Nimepata kesi sana za kutosalimia watu kwa sababu mimi nakua nashindwa kuwatambua,imefikia stage wengine wanasema nina dharau,sina heshima,nina maringo etc lakini deep within najua naumwa kwa hiyo hua naomba radhi tu(muda wa kumwambia kila mtu nina tatizo la macho sina)
Ni usumbufu kuibeba kila mahali kwa hiyo muda mwingine naibeba muda mwingine naicha tu makusudi.

Sipendi kuvaa muda wote kwa sababu ukishaanza hivyo ndio inakua kilema cha maisha,yaani hata kama ulikua unaweza kuona mita 100 itashuka uwe unaona mwisho mita 30 ukiwa hujaivaa!!!

Mbona majeshi ya ulaya na america tunaona watu wana miwani jeshini,huku kwetu ukiwa na hili tatizo hawakuchukui kabsa?
Ahahaaaaah...
Hatari sana...
Sasa mkuu haupishani na watu unaowafahamu njiani bila kuwasalimia kweli..?
Maana mimi kuna kipindi nilikua nafanya kama wewe,cases za kuwapita watu njiani bila kuwasalimia zikawa nyingi sana,ikanibidi niwe naivaa kila muda(isipokua nikiwa nyumbani tu)..!
Pia nafikiri kushika miwani mkononi au kuiweka mfukoni inaleta usumbufu kidogo..!
 
Pia kuna kipindi miwani yangu ilipasuka...
Nilipokwenda hospital kupima kwaajili ya kutengenezewa miwani mingine nikakuta namba ya lenzi imebadilika(tatizo la kutokuona mbali limeongezeka)...
Daktari akaniuliza kama huwa navaa miwani muda wote au sivai muda wote..!?
Nikamwambia huwa navaa nikiwa darasani na nikiwa naangalia TV tu..!
Daktari wa macho akanambia natakiwa kuvaa miwani muda wote,coz nisipofanya hivyo tatizo litakua linaongezeka kidogo kidogo,hivyo itanilazimu kubadili lenzi mara kwa mara..!
HAKUNAMATATA
Sasa mbona miwani ukivaa muda wote ndo kama vile inaongeza shida, siku zinavoenda naona hata tv nashindwa kuona vizuri yani inakua haiko clear bila miwani
 
Mimi nilipata shida hiyo nikiwa advance. Niliteseka sana, na kabla ya shida hiyo kunipata nilikuwa kipa wa kutegemewa. Sasa nikawa nawaambia wenzangu kuwa siwezi kusimama golini coz sioni vizuri lakini wakawa wananilazimisha. Mipira ilikuwa inapita kama hakuna MTU golini.

Baadaye nikaja kwenda hospitali nikapimwa miwani, lensi zote zikagoma kusapoti uoni. Nikarudishwa kwa daktari akanipa vidonge vitamin B, lakini wapi? Baada ya dozi ile kuisha nilienda duka la madawa nikihitaji vitamin B lakini wakasema hawana ila wana vitamin B complex, wakanipa hivyo. Baada ya kutumia hali ilibadilika kidogo.
Sisemi moja kwa moja kuwa vilinisaidia, ila hali yangu ya sasa si kama zamani. Nadunda tu bila miwani. Ila kipindi kile, magari yalikuwa yakipita pembeni yangu siwezi soma hata plate number. Mungu ni mwema.
 
Jamani kuna mdogo wangu yani hata kusafisha viatu vya shule hawezi, hawezi kbs bila miwani haoni vzr!! Naumia sana
 
Back
Top Bottom