Tatizo la Mabaka, Mba na Fungus (Fangasi) sugu na kuwashwa sehemu za siri kwa wanaume na wanawake- Fahamu chanzo, Dalili na Matibabu yake

Vinci wakati mwingine wengine huwa wanaogopa hata vivuli vyao.
Mamndenyi unampa pole kwani ni yeye, amesema ni rafiki yake na sio yeye...alaaa.:suspicious: mwambie mfikishie pole rafiki yako.
 
Last edited by a moderator:
LEO tuangalie fangasi wanaoshambulia sehemu za siri, yaani Tinea cruris. Aina hii ya fangasi ndiyo inayofahamika na Watanzania wengi zaidi ya aina nyinginezo na waathirika huwashwa sana sehemu za siri.

​






Dalili zake

Kuna dalili nyingi sana za ugonjwa huu lakini kubwa kuliko zote ni kuwa fangasi hawa huambatana na muwasho mkali wa eneo lenye maambukizi hasa sehemu za siri, rangi ya ngozi ya eneo lenye maambukizi hubadilika na kuwa na muundo wa duara, mfano wa sarafu.
Dalili nyingine ni ngozi kukauka kisha kubanduka, na kama mgonjwa asipopata tiba mapema basi atatokwa na majimaji kwenye eneo la ngozi lililoathirika pamoja na kutoka kwa harufu mbaya kwenye eneo hilo.

UNAVYOAMBUKIZWA

Kuna njia nyingi zinazoweza kusababisha uambukizi wa maradhi haya, lakini ili uambukizaji huu uwezekane lazima kuwe na mazingira rafiki ya kuwezesha fangasi kuishi na kuhama kwa urahisi.

Mazingira haya rafiki kwa kuruhusu fangasi hawa kuweza kutoka kwa mtu mmoja au sehemu moja ya mwili kwenda kwa mwingine huhitaji uwepo wa hali ya joto pamoja na majimaji sehemu iliyoathirika na

maambukizi hutokea kwa kugusana na mtu aliye na maambukizi tayari.

Mtu anaweza kupata maambukizi ya fangasi hawa kwa kushirikiana kimapenzi na mwenzake aliye na

ugonjwa au kwa kushirikiana mavazi na mtu aliyekwisha pata maambukizi au kushirikiana taulo au hata

sabuni na vifaa vya usafi wa mwili kwa mtu zaidi ya mmoja.

Watu ambao huweza kupata maambukizi ya fangasi wa sehemu za siri ni wale wanaofanya kazi

zinazohusisha ukaaji kwenye maji yaliyotuama kwa muda mrefu, wanaoshiriki mapenzi na wenza wenye

maambukizi ya fangasi hao na wote ambao wana fangasi za kwenye vidole kwani fangasi wale wanaweza

kuhamishwa kupitia kwenye kucha na kuhamia kwenye eneo hilo la siri;

-Wengine wanaoweza kupata maradhi haya ni wale wanaofanya usafi wa mwili kwa kutumia maji yaliyobeba

vimelea vya fangasi hao, wasiojikausha vizuri maungo ya sehemu za siri, watu wenye maradhi

yanayosababisha kushuka kwa kinga, hususan kisukari, wanaovaa nguo zaidi ya moja hali inayosababisha

mwili kushindwa kupunguza joto lake hivyo kutoa jasho, wanaovaa nguo za kubana sana hasa zile

zinazobana sana kwenye maeneo ya maungo ya siri na wenye unene wa kupindukia;

Lakini watu wanaokunywa dawa za kuua vimelea (antibiotics) kwa muda mrefu au wenye ujauzito ambao

huchangia kushuka kwa kinga ya mwili nao wanaweza kupata ugonjwa huu
.



 
Asante sana kwa somo nzuri, fangasi ni ugonjwa unaowasumbua wengi. Naomba kufahamu tiba ya ugonjwa huu.
 

Na Dk Isaack Maro ; Isaac.I.Maro@gmail.com

KWA UFUPI

  • Kwa kawaida, maradhi haya hushambulia zaidi vijana walio katika umri wa balehe na watoto.

Katika mwendelezo wa makala yetu ya maradhi ya ngozi tunaendelea kuangalia maradhi ya ngozi yatokanayo na fangasi, leo tukiangalia hamira (yeast) yanavyoshambulia sehemu mbalimbali za mwili. Maradhi haya kitaalamu huitwa tinea versicolor.

Utango tango (mba)




Mba ni maradhi maarufu zaidi kati ya magonjwa mengi yanayosambazwa na fangasi wanaoitwaMalassezia furfur ambao kwa kawaida huishi kwenye ngozi ya watu wazima bila kusababisha matatizo yoyote ya kiafya.

Vimelea hivi husababisha ngozi kwenye sehemu ndogo ya mwili kubadilika rangi ukilinganisha na rangi ya ngozi ya sehemu ya mwili iliyoizunguka.

Mba hushambulia nani?

Kwa kawaida, maradhi haya hushambulia zaidi vijana walio katika umri wa balehe na watoto.

Mwonekano wake

Maradhi haya hutambulika kwa namna mbalimbali, lakini ya muhimu zaidi ni mwonekano wake. Hutambulika kitaalamu kama ‘versicolor., neno la Kigiriki linalomaanisha kubadilika kwa rangi ya ngozi na hii humaanisha kuwa sehemu ya ngozi inayopata maambukizi ya maradhi haya hubadilika rangi yake kutoka ile ya asili.

Mfano rahisi ni mabadiliko ya rangi ya ngozi kutoka maji ya kunde na kuwa nyeusi zaidi au nyeupe zaidi ukilinganisha na sehemu za ngozi zilizozunguka eneo lenye maambukizi ya fangasi hao.

Ni sehemu gani hushambuliwa?

Maeneo ya ngozi yanayoathiriwa zaidi katika mwili ni mabega, shingo, mgongo na kifua.

Mara nyingine maradhi haya hushambulia maeneo ngozi inapojikunja kama vile maungo ya mikono, ngozi ya chini ya matiti, maeneo ya siri hasa pale miguu inapoanzia. Uso mara nyingi hauathiriki, ingawa kwa watoto wanaweza kupata maambukizi ya kwenye kidevu, pua, mashavu na hata paji la uso.
Mara nyingi, fangasi hawa wanaposhambulia uso hushambulia kwa wingi kiasi kwamba ukimtazama mgonjwa kwa haraka haraka unaweza kudhani kuwa hiyo ndiyo rangi yake halisi ya ngozi na kuwa maeneo ambayo hayajaathirika ndiyo yaliyoathirika.

Sababu za kutokea kwake

Sababu za maradhi haya bado zinafanyiwa uchunguzi, lakini kama nilivyosema kwenye makala za nyuma kuhusu namna fangasi wanavyosambaa, na kwamba, sababu hizi pia ni muhimu, nazo ni;

-Hali ya majimaji kwenye ngozi (inaweza kuwa hata jasho)

-Hali ya hewa ya joto (fangasi wanakua vizuri kwenye hali ya joto)

-Kinga ya mwili ikiwa chini

-Mabadiliko ya homoni

Inawezekana pia maradhi haya kupata watu ambao wamekosa sababu zilizotajwa hapo juu.

Usambaaji wake

Kwa vile vimelea vya fangasi vinavyosambaza maradhi haya kwa hali ya kawaida huishi kwenye ngozi si lazima mtu aambukizwe, bali kwa kawaida maradhi haya hutokea tu.

Itaendelea Chanzo. AFYA YA NGOZI : Hamira; jamii ya fangasi wenye madhara mwilini - mwanzo - mwananchi.co.tz





 
CLOTRIMAZOL,apply the cream in a thin layer(1/2 cm stripe) 2-3 times per day for 1-2 weeks until no further symptoms .
 
Pia jaribu kumeza vidonge vya Clamovid, hii ni dawa yenye Amoxicillin plus Clavunic acid ina uwezo mkubwa kumaliza kabisa hata gonoria sugu.
 
dawa ya fungus kwenye uume nini?

CLOTRIMAZOL,apply the cream in a thin layer(1/2 cm stripe) 2-3 times per day for 1-2 weeks until no further symptoms .

Mkuu.@mtoto wa maskin Tumia Dawa aliyokwambia Mkuu.@mimi49 itakusaidia lakini usikose kwenda kumuona Daktari akupige pia sindano ili uweze kupona haraka pole sana.

kwa kuongezea na maelekezo ya wakuu waliotangulia, pia unatakiwa ubadilishe chupi kila siku na kujikausha vizuri kwa "paper towel" au taulo maalum kila baada ya kujisafisha kwa maji!
 
Jamani ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje mana kila nikikaribia kuingia ktk cku zangu za kike ninapata fangas, ni mejarbu kila dawa ila cjui ata nini, zaid ya yote wkt mwngine vpele hutokea juu ya sehem i ya cr, nimeenda kwa madaktar wengi na kila mtu ansasema yake, kuna moja aliniambia ni kaswende nikameza dawa na cndano nikamalza lkn ugonjwa ukawepo 2, mwngne akaniambia ni dall zangu za izo cku km wengne anavyotokwa na chunusi, wa mwisho akaniambia ilo ni tatzo la kawaida kwa jinsia ya ke,

Naombeni ushauri, ni fanyeje mana nimechoka na ili tatzo.
 
Naombeni msaada wenu, jamani fangasi inanisumbua sana mana kila nikkarbia kuingia ktk zle cku za kke nawashwa sana na majimaji fulani yanatoka zaid ya yote vpele km vjpu vyenye usaha hutokea juu ya ile sehem ya cr, nimeenda kwa maktari wengi sana, baadhi wameniambia kuwa ni kaswende nikameza dawa na kuchomwa cndano lkn ugonjwa ukabak palepale, huyu akaniambia ni dalili za cku za kike km wengine wanavyotokwa na chunuc, mwingine akasema nijambo la kawaida kwa jnsia ya kike ila 2 nizdshe usaf lakini bado hali yangu co nzuri.

Jamani ndugu zangu, naombeni ushauri wenu nifanyaje mana nimechoka sana na i hali.
 
Pole sana mkuu. Hebu jaribu kufikiria katika wapenzi wako ulowahi kuwa nao kama ulishasikia wakikwambia umewaambukiza fangas. Hapo ndipo unaweza kujua kama hizo fungus zinatokana na wewe kuwa kwenye cku zako ama la. Mara nyingi fungus zinazotokana na mwanamke kuwa kwenye siku zake huwa ni mara chache sana kumwambukiza mwenzi wa kiume. Na huwa zinafikia mahali zinaisha zenyewe bila hata wewe kujua. Nimeprove kutoka kwa mpenzi wangu.
 
Umesema unapokaribia siku zako!? Wakati mwingine kunakuwa shwari? Hayo majimaji yanatoa harufu?
 
nawashwa sana na majimaji fulani yanatoka zaid ya yote vpele km vjpu vyenye usaha hutokea juu ya ile sehem ya cr, baadhi wameniambia kuwa ni kaswende nikameza dawa na kuchomwa cndano lkn ugonjwa ukabak palepale.

Kaswende ni ugonjwa hatari sana!

Ni PM uniambie historia yako ya sex patners ndipo nitoe ushauri!Ikiwezekana hata niuone uchi unao sumbuliwa na ugonjwa usio julikana kupitia skype ili nijue nn hasa tatizo!

Pole sana in advance
 
Dah kijana wewe noma unataka kuona private yake kwanza,Umehua band lol
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…