futurestar hebu kuja hapa eleza vizuri gonjwa yako pia jinsia yako.
Je wewe ni Mke au Mme?
Hao fangus ni wa nje?
Au ikiwa wewe Mke, Je, hao fangus ni wa ndani au nje?
Unataka kusaidiwa basi jitahidi kujieleza watu wakuelewe vyema vinginevyo utaishia kupata majibu ya juu juu tu na hautafanikiwa kuitibu.
USHAURI.
Ikiwa fangus wanaosumbua ni wa nje bila kujali wewe ni Mke au Mme, fanya yafuatayo
1. Hakikisha haufugi nywele sehemu za siri kwani zinatunza uchafu na majimaji
2. Hakikisha sehemu za siri ni safi muda wote.
3. Hakikisha sehemu za siri ni kavu muda wote.
4. Hakikisha unaoga asubuhi na jioni na kisha kausha na paka dawa sehemu hizo za siri. Nashauri utumie FUNGIFENG
5. Kama wewe ni Mme acha tabia ya kuparamia wanawake ovyo leo huyu kesho yule unaokoteza fangus
6. Kama wewe ni Mke acha tabia ya kuparamia wanaume ovyo kwani unaokoteza fangus
7. Hakikisha chupi unazovyaa ni kavu na safi muda wote, ikiwa wewe ni Mke unaweza badilisha mara 2 kwa siku
8. Usiku unaweza usivae chupi ukavaa bukta au nguo za kulalia pekee, hii utaruhusu maeneo nyeti kupata hewa
9. Chup ikivaliwa mara moja ifuliwe, usirudie. haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke.
Kwa uchache ni hayo tu.
Kama ni fangus za ndani, mimi sina majibu.