Tatizo la maji limetatuliwa, la umeme litakwisha karibuni na miradi mingine yote inakamilishwa. Watanzania tuunge mkono juhudi za serikali yetu

Kutwa kushinda kulalama kwenye mitandao huu mda na nguvu ungeitumia kuchimba hata kisima
 
Mkuu Glenn kwani huoni juhudi za Serikali? Issue ya maji ilikuwa kwa sababu ya ukame, Serikali imetatua kwa kuongeza visima ili kutatua shida ya maji
 
Tatizo la maji limetatuliwa au ni kwa sababu mvua zimeanza kunyesha, umeme nao tunatarajia hali kuwa shwari kwa sababu mabwawa mda si mrefu yatatengamaa kwa sababu za mvua basi, hakuna kitu serikali ya ccm inaweza kukifanya kwa 100%
@Pancras Suday hukuona visima vilivyozinduliwa kigamboni? Ni kweli kunyesha kwa mvua kumepunguza tatizo, lakini Serikali pia umechukua jitihada za makusudi kutatua upungufu wa maji
 
Hongereni serekali kwa kutatua tatizo la maji dar, maana wake zetu wametombwa sana wiki mbili hizi kwa kisingizio cha kwenda kutafuta maji
Hakuna uhusiano katika hili, mtu kama ni tabia yake itabaki kuwa hivyo Mnyenz
 
2025 Kuna watu watakosa ajenda, halafu na katiba tunaichomekea kidoogo uchaguzi ukikaribia, lengo kufuta kabisa hija zao
Kwa namna Serikali ya awamu ya sita inavyosimamia utekelezaji wa miradi ya Maendeleo hakuna ubishi katika hilo chiembe
 
Tatizo la maji limeamuliwa na Allah baada ya kusikia kilio cha walio wengi wakati chawa wako bize kulamba asali bila ya kuwa na time na kero za wananchi.
 
Ngoja watu waone utekelezaji Kwa vitendo (uhalisia) na sio matamko tu.

Isijekuwa zilongwa mbali zitendwa mbali.
 
Ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara za mwendo kasi, madaraja, vivuko, SGR, JNHPP, Ujenzi wa madarasa, ujenzi wa mabweni, ujenzi wa nyumba za Watumishi, Ujenzi wa majengo ya kiutawala, miradi ya kilimo etc.
Tunaomba majibu ya hii scandal hapa👇

 
Mvua zimeanza kunyesha usitake kuwaona Watanzania mabwege kama nyie chawa wa ccm
 
Ni kweli ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kuleta mvua, lakini Serikali ilianza kuchukua hatua za makusudi katika kutatua tatizo la maji, ndio maana ilipeleka fedha nyingi kukamilisha visima kule kigamboni.
Tatizo la umeme sio la jana, Serikali hii haiwezi kutatua kwa siku moja, kutatua changamoto ya umeme inahitaji uwekezaji ikiwa ni pamoja kufanya mataengenezo ya mitambo yetu na kuleta vyanzo vipya vya umeme, ndio maana Serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi ili kukamilisha mradi wa JNHPP, pia miradi mingine inakuja itakyokuwa mbdala wa vyanzo vilivyopo sasa, tumuamini Waziri wa Nishati Mh. Makamba, lakini pia tuiamni na kuipa muda Serikali ya awamu ya sita kutatua kero ya umeme na kubaki historia
 
Niliona Siasa tupu zinaendekezwa Mkuu wangu.

Ila huyo mnayemsifia sifia hamna lolote la maana amelifanyia Taifa mpaka sasa mkuu.
Mkuu TANMO hivi ni kweli huoni miradi yote inayotekelezwa? Hakuna hata mradi mmoja uliosimama na miradi mipya inaendelea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…