Tatizo la maji limetatuliwa, la umeme litakwisha karibuni na miradi mingine yote inakamilishwa. Watanzania tuunge mkono juhudi za serikali yetu

Tatizo la maji limetatuliwa, la umeme litakwisha karibuni na miradi mingine yote inakamilishwa. Watanzania tuunge mkono juhudi za serikali yetu

Ni kweli ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kuleta mvua, lakini Serikali ilianza kuchukua hatua za makusudi katika kutatua tatizo la maji, ndio maana ilipeleka fedha nyingi kukamilisha visima kule kigamboni.
Tatizo la umeme sio la jana, Serikali hii haiwezi kutatua kwa siku moja, kutatua changamoto ya umeme inahitaji uwekezaji ikiwa ni pamoja kufanya mataengenezo ya mitambo yetu na kuleta vyanzo vipya vya umeme, ndio maana Serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi ili kukamilisha mradi wa JNHPP, pia miradi mingine inakuja itakyokuwa mbdala wa vyanzo vilivyopo sasa, tumuamini Waziri wa Nishati Mh. Makamba, lakini pia tuiamni na kuipa muda Serikali ya awamu ya sita kutatua kero ya umeme na kubaki historia

Ni rahisi kuamini ngamia kuingia kwenye tundu la Sindano kuliko kumuamini marope...
 
@Pancras Suday hukuona visima vilivyozinduliwa kigamboni? Ni kweli kunyesha kwa mvua kumepunguza tatizo, lakini Serikali pia umechukua jitihada za makusudi kutatua upungufu wa maji
Hivyo visima vilipozinduliwa kwani vilimaliza mgao wa maji!? Si vilipunguza tu, na kwa nini miaka 60 ya uhuru tuwe tunaimba matatizo yale yale !?
 
Mkuu umesahau mwishoni kuweka namba yako ya simu ,kuna viti viwili bungeni vya rais vimebakia.
 
Ni kweli ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kuleta mvua, lakini Serikali ilianza kuchukua hatua za makusudi katika kutatua tatizo la maji, ndio maana ilipeleka fedha nyingi kukamilisha visima kule kigamboni.
Tatizo la umeme sio la jana, Serikali hii haiwezi kutatua kwa siku moja, kutatua changamoto ya umeme inahitaji uwekezaji ikiwa ni pamoja kufanya mataengenezo ya mitambo yetu na kuleta vyanzo vipya vya umeme, ndio maana Serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi ili kukamilisha mradi wa JNHPP, pia miradi mingine inakuja itakyokuwa mbdala wa vyanzo vilivyopo sasa, tumuamini Waziri wa Nishati Mh. Makamba, lakini pia tuiamni na kuipa muda Serikali ya awamu ya sita kutatua kero ya umeme na kubaki historia

sasa huoni kama tuko reactive baada ya proactive dalili ya kwanza mtu kushindwa kuwa kiongozi hiyo.

Umeme ni suala basic sana, miaka yote ilipaswa tuwe na enough capacity + reserve + standby power vz ongezeko la watu na shughuli za uzarishaji...
Kushindwa nayo kusolve basics na kufanya proper calculation watu wasiingie kwenye shida za mara kwa mara ni another failure ya uongozi.
 
Serikali ya awamu ya sita haijawahi kupumzika katika kutatua kero za Watanzania, tatizo la maji lililokuwa limetokea hivi karibuni hasa kwa Wakazi wa Dar Es Salaamu limetatuliwa kwa asilimia 100, tatizo la mgao wa umeme liko mwishoni kuwa historia, kila kitu kinahitaji muda na fedha.

Watanzania tuendelee kuunga mkono Serikali ya awamu ya Sita, miradi yote ya maendeleo iiliyopangwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imeanza kutekelezwa, fedha zimeshapelekwa, miradi iliyokuwa imeanza kutekelezwa miaka ya nyuma hakuna mradi hata mmoja uliosimama.

Ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara za mwendo kasi, madaraja, vivuko, SGR, JNHPP, Ujenzi wa madarasa, ujenzi wa mabweni, ujenzi wa nyumba za Watumishi, Ujenzi wa majengo ya kiutawala, miradi ya kilimo etc.

Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, iko kwa ajili ya Watanzania na ni ukweli usio pingika awamu hii hali ya Demokrasia ni ya juu kabisa, ndio maana kila mtu yuko huru kutoa maoni na akasikilizwa. Tatizo la vijana wengi wanaamini kutukana na kukosoa tu ndio kutoa maoni.

Tuipende Tanzania yetu, tuunge mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Ikiwa kiongozi mkuu wa Dar alisema isilaumiwe Dawasco kwa mgao ilaumiwe mvua imechelewa. Na umeme pia ni upungufu wa maji. Sasa mvua iliyolaumiwa imenyesha kwanini tusiishukuru pia mvua iliyolaumiwa. Imenyesha maji yamejaa shida imeisha
 
Hahah tatizo limetatuliwa na "waziri wa mvua"
 
sasa huoni kama tuko reactive baada ya proactive dalili ya kwanza mtu kushindwa kuwa kiongozi hiyo.

Umeme ni suala basic sana, miaka yote ilipaswa tuwe na enough capacity + reserve + standby power vz ongezeko la watu na shughuli za uzarishaji...
Kushindwa nayo kusolve basics na kufanya proper calculation watu wasiingie kwenye shida za mara kwa mara ni another failure ya uongozi.
Mkuu Nangu Nyau unachosema ndio Serikali ya awamu ya sita sasa inachokifanya ili hapo baadaye kusiwe na shida kama hizi, Serikali imeendelea kuwekeza mabilion ya fedha ili kutafuta chanzo mbadala na tofauti tofauti cha umeme, ndio maana unaona JNHPP inaendelea, kuna miradi ya gesi, jua , upepo inakuja, kikubwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali, uwekezaji mkubwa kama huo ni ngumu kukamilisha kwa miaka miwili ambapo Serikali ya awamu hii imekuwa madarakani
 
Ikiwa kiongozi mkuu wa Dar alisema isilaumiwe Dawasco kwa mgao ilaumiwe mvua imechelewa. Na umeme pia ni upungufu wa maji. Sasa mvua iliyolaumiwa imenyesha kwanini tusiishukuru pia mvua iliyolaumiwa. Imenyesha maji yamejaa shida imeisha
Ila tukumbuke maji yalipokuwa ya mgao tulilaumu serikali huku tukijua tatizo ni ukame hata mgao ulivoisha acha tuipongeze serikali hata kama tunajua ni mvua imenyesha huu. Ndo ungwana
 
Serikali ya awamu ya sita haijawahi kupumzika katika kutatua kero za Watanzania, tatizo la maji lililokuwa limetokea hivi karibuni hasa kwa Wakazi wa Dar Es Salaamu limetatuliwa kwa asilimia 100, tatizo la mgao wa umeme liko mwishoni kuwa historia, kila kitu kinahitaji muda na fedha.

Watanzania tuendelee kuunga mkono Serikali ya awamu ya Sita, miradi yote ya maendeleo iiliyopangwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imeanza kutekelezwa, fedha zimeshapelekwa, miradi iliyokuwa imeanza kutekelezwa miaka ya nyuma hakuna mradi hata mmoja uliosimama.

Ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara za mwendo kasi, madaraja, vivuko, SGR, JNHPP, Ujenzi wa madarasa, ujenzi wa mabweni, ujenzi wa nyumba za Watumishi, Ujenzi wa majengo ya kiutawala, miradi ya kilimo etc.

Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, iko kwa ajili ya Watanzania na ni ukweli usio pingika awamu hii hali ya Demokrasia ni ya juu kabisa, ndio maana kila mtu yuko huru kutoa maoni na akasikilizwa. Tatizo la vijana wengi wanaamini kutukana na kukosoa tu ndio kutoa maoni.

Tuipende Tanzania yetu, tuunge mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Mtasifia ujinga sana lakini hamteuliwi ng'o !!! CCM ina wenyewe na nyie siyo sehemu ya hao wenyewe, nyie vibaka tu
 
Mkuu Watu8 vile visima kigamboni hukuviona pia? Mvua imeleta neema na Serikali imefanya kwa uwezo wake

Visima vilizinduliwa na maji kwa kiasi kikubwa yaliendelea kuwa ya mgao, hayakuwa toshelevu kwa maeneo yote...

Kwa kifupi tuishukuru mvua iliyoanza kunyesha mikoani wiki kadhaa nyuma...
 
Mkuu miaka miwili tu hapo Nyuma haya matatizo ya Maji na Umeme hayakuwa makubwa kama ilivyo sasa.

Siyo chuki Mkuu wangu..
Wewe nae uwe unatumia akili,hiyo Miaka 2 ilikuwambwa na ukame? Hiyo Miaka 2 vyombo vya habari vilikuwa huru kuripoti?

Awamu ya 6 ndio imefanya kazi kubwa Sana kwenye sekta ya Maji,bajeti tuu Ni Mara 2 ya awali.
 
Back
Top Bottom