Uchaguzi 2020 Tatizo la sera za Rais Magufuli ni kutogusia maendeleo ya watu kwenye kampeni zake

Uchaguzi 2020 Tatizo la sera za Rais Magufuli ni kutogusia maendeleo ya watu kwenye kampeni zake

Sasa umefika muda wa kampeni wananchi wamejitokeza wengi walikuwa wanategemea kusikia maendeleo yanayowagusa watu
Ni kweli miundombinu ni muhimu lakini maendeleo ya watu ni muhimu pia kwa hili Mheshimiwa kuna kila dalili watu itabidi waendelee kukaza mikanda kwa kipindi kingine cha miaka mitano ili miradi ikamilike
Maendeleo ya vitu bila ya maendeleo ya watu hayo sio maendeleo ya kweli. Nilijiandaa sana kusikia sera za maendeleo ya watu mfano namna ya kuwapa bima wananchi zaidi ya milioni 50, issue za food security na kadhalika. Ila ninachokisikia ni midege na ma-SGR tu. Ndiyo maana kampeni za sasa hazina mvuto
 
Kwa miaka mitano tangia uingie madarakani wapo wananchi wengi waliokuunga mkono wakakubali kufunga mikanda wakasahau yale yote uliyowaahidi ili mambo ya msingi yafanyike wakitegemea mambo yatakuwa mazuri mbeleni

Ni kweli umefanya mengi Mheshimiwa kama watangulizi wako ambayo walishayafanya anajenga reli ya kisasa,unajenga bwawa,umeboresha miundombinu mingine kama flyover na barabara

Sasa umefika muda wa kampeni wananchi wamejitokeza wengi walikuwa wanategemea kusikia maendeleo yanayowagusa watu
Ni kweli miundombinu ni muhimu lakini maendeleo ya watu ni muhimu pia kwa hili Mheshimiwa kuna kila dalili watu itabidi waendelee kukaza mikanda kwa kipindi kingine cha miaka mitano ili miradi ikamilike
Maendeleo ya watu yanakuwaje? Fafanua kwa undani
 
Hivi mtu anashindwa kupata hata chai ya asubuhi, anadandia malori kwenda kijijini kwake eti aje kupanda flyover sijui ndege. Labda zile ndege za sabasaba.
 
Unazungumziaje maendeleo ya watu wakati hujaweka viwezeshi vya hao watu kupata maendeleo? Huwezi kuwa na viwanda vikubwa vinavyoajiri watu wengi bila kuwekeza kwenye umeme wa uhakika. Huwezi kuwaambia wananchi walime mazao ya biashara wakati hujawekeza katika miundombinu ya kuwafikia wananchi. Huwezi kutaka wananchi wafanye kazi wakati hujawekeza kwenye huduma ya afya. Huwezi kuhubiri afya njema wakati hujawekeza kwenye maji safi. Usitegemee maendeleo ya watu katika sehemu ambayo mtu akitaka kwenda eneo jingine lenye umbali wa kilomita 300 anatumia siku mbili hadi tatu. Usitegemee maaendeleo ya watu katika eneo ambalo watu wanalima nyanya lakini zinatumia siku tano hadi kufika sokoni. Huwezi kutegemea maendeleo ya watu katika eneo ambalo mtoto anatembea umbali wa kilomita 30 kuikuta shule. Huwezi kutegemea maendeleo ya watu katika serikali ambayo zaidi ya asilimia 20 ya wafanyakazi wanatumia vyeti vya kufoji.
 
Huo umati wa watu hapo uwanjani Shinyanga, aah, aah aah acha kabisa. Utanzania siafu katika kichuguu chao wakiwa wamevamiwa na neema ya kumbikumbi.

Mabeberu na kibaraka wao mkuu Lissu sura zimewashuka kwa aibu na sijui wataenda kuzificha wapi nyuso zao oktoba baada ya uchaguzi. NTv ya Kenya mko wapi? Mkuje huku muabike.
Uwanjani tulienda kuangalia tamasha la mziki wala hatujaenda kumsikiliza yeye!!
 
Kwa miaka mitano tangia uingie madarakani wapo wananchi wengi waliokuunga mkono wakakubali kufunga mikanda wakasahau yale yote uliyowaahidi ili mambo ya msingi yafanyike wakitegemea mambo yatakuwa mazuri mbeleni

Ni kweli umefanya mengi Mheshimiwa kama watangulizi wako ambayo walishayafanya anajenga reli ya kisasa,unajenga bwawa,umeboresha miundombinu mingine kama flyover na barabara

Sasa umefika muda wa kampeni wananchi wamejitokeza wengi walikuwa wanategemea kusikia maendeleo yanayowagusa watu
Ni kweli miundombinu ni muhimu lakini maendeleo ya watu ni muhimu pia kwa hili Mheshimiwa kuna kila dalili watu itabidi waendelee kukaza mikanda kwa kipindi kingine cha miaka mitano ili miradi ikamilike

sio tatizo la magufuli ni tatizo la wajinga ambao hawajui uwekezaji huanza kwanza! haiwezekani ufanye kazi sehem ambapo hapafanyiwa uwekezaji kuanzia kujenga ofisi
 
Kuzidi ya lisu?
Watu wa chadema kila kukicha mnateseka na mwazo hata mkiwa kwenye majukwaa mnatoa povu la moshi wa kumi mpaka mapafu yenu yatajaa ukungu.

Mpaka uchaguzi uishe mtakuwa wateja wa mahospitali yaliyo jengwa na jembe.
Umeandika nn sio lazima ujibu kila kitu unapoteza haina yako humu au ndio mnafundishwa huko ccm maana nasikia hata baba yenu anasema anataka kazi ya kufagia kwa vyumba vya malaika. Jifunzeni kutoa hoja za kufikirika
 
Umeandika nn sio lazima ujibu kila kitu unapoteza haina yako humu au ndio mnafundishwa huko ccm maana nasikia hata baba yenu anasema anataka kazi ya kufagia kwa vyumba vya malaika. Jifunzeni kutoa hoja za kufikirika
Punguzeni hasira kwenye mikutano hao ni watu sio ng'ombe.
 
Back
Top Bottom