Tatizo la Ucheleweshwaji wa Mikopo Benki ya CRDB

Tatizo la Ucheleweshwaji wa Mikopo Benki ya CRDB

Akili 09 Nguvu 01

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2015
Posts
695
Reaction score
1,377
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Nimekua nikisikia kutoka kwa baadhi ya watu(wateja wa benki ya CRDB) kuwa wameomba Mikopo kutoka katika benki hiyo lakini kwa muda mrefu hawajapatiwa fedha/mkopo huo lakini wameshaanza kukatwa fedha kwa ajili ya mkopo huo

Hivi karibuni nimekua mhanga wa jambo hilo(mkopo wa CRDB). Mimi ni mteja wa benki hiyo niliomba mkopo kutoka katika benki tangu tarehe 10 ya mwezi Machi hadi leo tarehe 30 Aprili sijapatiwa fedha?mkopo huo na wameshaanza kunikata,

Kila nikienda kwa Afsa mikopo wa branch hii ananiambia kua yeye ameshamaliza kila kitu shida ipo Makao makuu, yaani kwa sasa ukiomba mkopo benki ya CRDB mahali popote pale Tanzania hii basi Makao makuu ya CRDB ndo watalazimika kupitia Maombi yako na wao ndo wataamua kukupa au kutokupa. Baada ya kumsumbua sana Afsa mikopo akalazimika kunionesha list ya wateja walioomba mkopo tangu mwezi Machi lakini bado hawajapata

Nina rafiki yangu yupo mikoa ya Kaskazini nae aliomba mkopo CRDB tangu mwezi Machi naye hadi leo hajapata(tunawasiliana kila siku ili kujua maendeleo)

Benki ya CRDB kama hamna fedha za kutoa mikopo basi sitisheni tu kuliko kusumbuana na kutiana hasara namna hii(ninapoomba mkopo nakua na shida na fedha kwa wakati huo kwahiyo toeni mikopo kwa wakati,

Huu utaratibu wa mikopo yote Tanzania hii kuwekwa kutoka Makao makuu umeanza lini, mbona kipindi cha Mkurugenzi yule kulikua hakuna mambo haya? mjitafakari kama hamna fedha semeni

Kama una mpango wa kuombs Mkopo CRDB utachelewa sana, ikiwa aliyeomba mwezi machi hadi leo hajapata, je wewe ukiomba Mwezi huu utapata lini?' TAFAKARI, CHUKUA HATUA'
Nina hasira sana
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Nimekua nikisikia kutoka kwa baadhi ya watu(wateja wa benki ya CRDB) kuwa wameomba Mikopo kutoka katika benki hiyo lakini kwa muda mrefu hawajapatiwa fedha/mkopo huo lakini wameshaanza kukatwa fedha kwa ajili ya mkopo huo

Hivi karibuni nimekua mhanga wa jambo hilo(mkopo wa CRDB). Mimi ni mteja wa benki hiyo niliomba mkopo kutoka katika benki tangu tarehe 10 ya mwezi Machi hadi leo tarehe 30 Aprili sijapatiwa fedha?mkopo huo na wameshaanza kunikata,
CRDB haiwezi kustawi tena, nsekela hawezi kuimudu, vita alopigwa kimei hii ndo KARMA
 
Sio chai hii? Yaan uanzwe kukatwa makato ya mkopo kabla hujapewa mkopo?
 
Aisee mbona kuna jamaa yangu aliomba mkopo crdb na akapata ndani ya siku 7 tuu, na walimwambia within a week mambo yatakua poa na kweli siku 7 wakampigia simu kua mambo yameiva.
 
Hii inatokea CRDB nawajua watu watatu waliomba mikopo hadi wakaamua kuahirisha, wakajazishwa fomu za kucancell
 
Sio chai hii??? Yaan uanzwe kukatwa makato ya mkopo kabla hujapewa mkopo???
Mkuu mtu unaanzaje kuleta chai katika ishu kama hii? huu ni Ukweli kabisa kua CRDB wamachelewa kuweka fedha za mkopo, yaani unaweza kuwa washaanza kukukata kabla ya wewe kupata fedha yako
 
Nendeni Nmb
Yaah mtu unaeza enda NMB kuomba mkopo na ukapata within a reasonable time. Tatizo ni kua ulishaenda CRDB na washaanza kukukata salary slip ishaathirika, unaendaje NMB? Otherwise ue mteja mpya na ushajua Ucheleweshwaji huu wa CRDB ndo waeza enda NMB
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
CRDB IMEFIRISIKA THIS IS SERIOUS HAWANA FEDHA ZA KUKOPESHA WATUMISHI ZAIDI YA UJANJA KAMA HUU. MAELEZO MENGI UTEKELEZAJI 0!! HOVYO KABISA. MKIWA NA SHIDA YA KUKOPA NENDENI NMB UHAKIKA KWA 100% NDANI YA SIKU 7 TU!!
 
Ni shida zamani 24hrs baada ya jiwe ni one month.Baada ya mwendazake kuifilisi crdb akamuhonga ubunge Kimei kwa ahadi ya kuwa waziri wa pesa
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Nimekua nikisikia kutoka kwa baadhi ya watu(wateja wa benki ya CRDB) kuwa wameomba Mikopo kutoka katika benki hiyo lakini kwa muda mrefu hawajapatiwa fedha/mkopo huo lakini wameshaanza kukatwa fedha kwa ajili ya mkopo huo
Vp mkuu wamekuwekea mkopo wako au bado?
 
Vp mkuu wamekuwekea mkopo wako au bado?
Walishaniwekea mkuu, siku nimejiandaa kwenda kuabort mkopo kwakweli nilijiandaa kishari kabisaa lakini yule dada wa mikopo anakanambia kua tayari wameshaniwekea masaa machache waliyopita na akanionesha pale kweli nikaona mzigo upo
Basi nikaondoka pale kwa furaha zotr na kwenda bar nikupongeza kidogo
 
Walishaniwekea mkuu, siku nimejiandaa kwenda kuabort mkopo kwakweli nilijiandaa kishari kabisaa lakini yule dada wa mikopo anakanambia kua tayari wameshaniwekea masaa machache waliyopita na akanionesha pale kweli nikaona mzigo upo
Basi nikaondoka pale kwa furaha zotr na kwenda bar nikupongeza kidogo

Ukaenda bar na hela ya mkopo [emoji3] kukopa harusi kulipa matanga.
 
Walishaniwekea mkuu, siku nimejiandaa kwenda kuabort mkopo kwakweli nilijiandaa kishari kabisaa lakini yule dada wa mikopo anakanambia kua tayari wameshaniwekea masaa machache waliyopita na akanionesha pale kweli nikaona mzigo upo
Basi nikaondoka pale kwa furaha zotr na kwenda bar nikupongeza kidogo

Nilikua nasubiri hii sentensi ya mwisho… hongera mkuu hivi riba Yao ni % ngapi?
 
Back
Top Bottom