Tatizo la ufaulu duni wa masomo ya Mathematics na Physics bado halijaeleweka!

Tatizo la ufaulu duni wa masomo ya Mathematics na Physics bado halijaeleweka!

Sababu zinazochangia ufaulu duni ni pamoja na,

1. IQ ndogo za wanafunzi

2. Wanafunzi kutumia muda wao mwingi kwenye mambo ya ngono, bangi, vigodoro, tamthilia, muziki na mpira

3. Usimamizi mbovu wa wazazi/walezi kwa watoto wao.

4. Jamii kuyachukulia masomo hayo kama masomo ya "Wateule" kitu kinachoathiri kisaikolojia mitazamo ya wanafunzi.

5. Mazingira duni ya kujifunzia.

6. Upungufu wa walimu wa masomo hayo, mfano utakuta shule ina wanafunzi 800 ila ina mwalimu mmoja au wawili wa hisabati, kwa mazingira hayo hakuna muujiza wa walimu kumudu kufundisha vema idadi hiyo.

7. Ualimu imebaki ni kazi kama kazi zingine na sio wito tena, hivyo walimu wako busy na maisha kuliko kazi.

8. Siasa.

.Acha niishie hapo kwa sasa.
 
Hali ni mbaya sana, kuna uwezekano hata walimu wa masomo hayo kwa sasa ni weupe balaa.....si unajua mitaala ilishachakachuliwa ndo mavuno yake tunayoshuhudia sasa.

Na vijana siku hizi wamekuwa bize na mambo kibao mara TV, bongo fleva, tamthilia, amapiano, miso misondo na matakataka kibao yaliyoletwa na utandawazi ukilinganisha na enzi zetu ambapo mambo ya TV na simu za mkononi hayakuwepo.​
 
Ukijumlisha na hii kauli ya "Mwalimu hapa ni wapi?" Watastandardize sana matokeo.
 
Sababu zinazochangia ufaulu duni ni pamoja na,

1. IQ ndogo za wanafunzi

2. Wanafunzi kutumia muda wao mwingi kwenye mambo ya ngono, bangi, vigodoro, tamthilia, muziki na mpira

3. Usimamizi mbovu wa wazazi/walezi kwa watoto wao.

4. Jamii kuyachukulia masomo hayo kama masomo ya "Wateule" kitu kinachoathiri kisaikolojia mitazamo ya wanafunzi.

5. Mazingira duni ya kujifunzia.

6. Upungufu wa walimu wa masomo hayo, mfano utakuta shule ina wanafunzi 800 ila ina mwalimu mmoja au wawili wa hisabati, kwa mazingira hayo hakuna muujiza wa walimu kumudu kufundisha vema idadi hiyo.

7. Ualimu imebaki ni kazi kama kazi zingine na sio wito tena, hivyo walimu wako busy na maisha kuliko kazi.

8. Siasa.

.Acha niishie hapo kwa sasa.
Mkuu umemaliza kila kitu. umepita mule mule. Hata hivyo, niliwahi kuandika kwa urefu kuhusu suala la ufaulu duni wa wanafunzi wa kizazi hiki kwenye uzi huu hapa chini.

Moderator tafadhali unganisha huu uzi na uzi uliotangulia ili tuwe na maoni ya pamoja kwa mustakabali chanya wa elimu ya watoto wetu.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Haya masomo sio magumu kama inavyosemekana ila tatizo ni walimu wa haya masomo, hapa nadhani muundo wa maslahi ya mwalimu wa masomo ya sayansi uwe tofauti na mwalimu wa sanaa mfano stashahada ya daktari na mwalimu wa fizikia au hesabu iwe sawa.
 
Hili tatizo ndilo linaweza kukuonesha uwezo wa akili za watu wetu na namna wanavyoweza kutatua changamoto mbalimbali katika jamii yetu.

Hisabati, fizikia, kemia na baiolojia ni maisha, kwani hayo masomo yanahitaji akili nzuri ambazo ndo zinahitajika katika kuinua uchumi, kuongeza ubunifu, kutatua changamoto za magonjwa, kukuza teknolojia.

Taifa lipo hapa lilipo kwa sababu akili za watu wengi hazipo kwenye ubora unaotakiwa kwa mstakabali wa maendeleo ya watu wenyewe na nchi kwa ujumla.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom