Tatizo la umeme: Awamu ya tano haiwezi kukwepa lawama labda tu kama madai hayana ukweli

Swali langu linaenda TANESCO kila siku wanatuambia kwamba TZ kwa sasa wanazalisha takribani umeme wa 1600MW na matumizi ya nchi nzima kwasasa ni 1200MW ,jana wametangaza wana upungufu wa 358MW inakuwaje wanataka kufanya mgao wakati bado tuna ziada ya 42MW ambao ni umeme mwingi sana Kigoma tu yote matumizi yao ni 7MW.
 
sina hakika lakini hili suala la mgao wa umeme, soon tu utasikia kuwa flani na flani wanapewa mkataba wa kuzalisha umeme ili kuliuzia shirika, kutokana na mgao uliopo

hapo ndipo nitakapoamini kuwa upigwaji umerejea, maana awamu iliyopita kuvunja mikataba ya unyonyaji kwa shirika kuuziwa umeme iligusa maslahi ya wengi, usidhani wapo tayari kutelekeza mitambo waliyoinunua kwa hela nyingi na hawana pa kuipeleka
 
Hahahahah justification ya hilo ndio inatafutwa sasa hivi
 
Nyerere alisema kiongoz mpya anayeingia ikulu ana takiwa kuendeleza mazur ya mtanguliz wake na kuachana na Mambo baya , sasa chakushangaza Samia yeye ana chukua mabaya mazur ana ya acha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yataka watu wenye akili na weledi kukubali, wengi wetu tuna mtazamo hasi kwa kila jambo

Sent from my MRD-LX1F using JamiiForums mobile app
 
Nyerere alisema kiongoz mpya anayeingia ikulu ana takiwa kuendeleza mazur ya mtanguliz wake na kuachana na Mambo baya , sasa chakushangaza Samia yeye ana chukua mabaya mazur ana ya acha

Sent using Jamii Forums mobile app
JPM aliendeleza ya Kikwete? Acha unafiki!! What about mradi wa mwendokasi phase 2 and 3? Kuunganisha wilaya zote kwa lami? Mradi wa gas Mtwara ambao tayari serikali ilikuwa imeshainvest hela nyingi kule? Katiba mpya pale ilipoishia iliendelezwa? Bandari ya Bagamoyo ambayo mazungumzo yalishaanza? Maboresho ya shule za kata kwa kuongeza/kuajiri walimu wapya, kujenga maabara za kisasa, kuongeza madarasa? ACHENI UNAFIKI NYIE WATU, HILI SUALA LA UMEME LITAPITA KAMA YALIVYOPITA MENGINE, SOON MTATUPIWA JAMBO LINGINE LA KULALAMIKA, Mpo kama mafisi kudandia hili kabla halijaisha mnatupiwa fupa lingine mnaanza kuhangaika nalo
 
Ukitangaza tu unauawa siku hiyohiyo. Aise lile dubwana lilikuwa katili balaa hata mungu huko aliko atakuwa analishangaa. Si unaona hata mke wake ameanza kupendeza
Maovu mengi sana yalifanyika kipindi chake, watu wengi waliumizwa, watu walifungwa midomo, amekomba hela zote mifuko ya jamii kwenda kufanya miradi yake isiyo na planning, kaiumiza sana hiyo TANESCO kwa kuifanyisha mambo kinyume na maelekezo ya wataalamu kisa apate sifa utawala wake eti umeme haukatiki!!!! ILA NDIYO HIVYO, MAREHEMU APUMZIKE KWA AMANI!! UZURI NI KWAMBA HATORUDI TENA.......
 
Kwa
Kwa hiyo leo unayo lipoti kuwa hayo maji yamepungua kiasi gani na haya mabwawa kwa saa yanatoa mgwt ngapi kwa ujumla kama tatizo ni maji?
Je hili la kuafanya ukarabati nibla uongo?

Kumbuka wakati makamba akiwa wazili wa mazingila ndiye aliyepinga kujengwa kwa hilo bwawa na mpaka sasa kunatafutwa sababu ya kulionyesha hilo .bwawa halifai ili lisijengwe na inaonekana yeye hana mpango nalo sema tu kwa kuwa limefikia hatua kubwa
Kama tatizo ni ukame kwa nini wasipande miti kila sehem na kutunza vyanzo vya maji?
Badala yake wanaenda kujifunza misri ambako wana jangwa eti misri ya kijani.

Yaani sisis tukajifunze misri wakati tuna nchi yenye hali nzuri ya mzingila?

Hapa ni kutafuta sababubya kusitisha ujenzi wa mwalim nyerere hydropower.
Wanatuandaa kisaikolojia.
 
Wakatai wanasubili swala la umeme lipite lije lingine hizo hasara wanazopata nani atawafidia
Kwa hiyo hii nchi ni ya kusubili majanga yapite kila mda huku watu wakikosa kusonga mbale na umli unaisha ili wabaki masikini miaka yote bali watawala wao wanatajilika na kodi za hao wanaosubili yapite?

Msicheze na maisha ya watu kwa visingizio visivyokua na maana.
Kama wameshindwa basi warudishe wakoloni watawale kwa muda ilia hizo shida ziondoke.
 
Hoja yangu kwa yule bwana ni ile ile---
Kwanini hakuwa na succession plan? Ilikuwaje akahodhi kila kitu hadi mipango mizuri aliyokuwa nayo iliyowezesha kupata umeme muda wote!?
Kwanini hakuamua kuwekeza kujenga mifumo thabiti kwa manufaa ya taifa?--
Succession plan umeiosoma wapi mangi
Kiongozi gani ameshaakuwa a Succession plan hadi uje uikaumu awamu ya 5
 
Sisi tunazungumzia mgao wa umeme ndugu yeye samia Atawale atakavyo kwa kuifungua nchi au vyovyote atakavyoona inafaa , lakin sio kuweka mgao wa umeme
 
Bandari ya bagamoyo ni kuuza nchi miaka 99 tokea tupate Uhuru hatuja fika, Kampuni za gas alifukuza wote mikataba yote kikwete alichukua 10% magufur aka watimua akasema makubaliano Yao na serikal iliyopita haitambui, kuhusu umeme matakataka na mautumbo yote ya serikali zilipita, mfano Symbion, Agreco, iptl, wote aka watimua hakuangalia ma generator yaliletwa na Obama wa bush

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefika huku Tunduma tangu mwaka 2016 nimekuta ni mgao wa umeme kwa kwenda mbele wanakata kila jumanne, alhamis na Jumamosi. Hata alivyokuja JPM huku wananchi walilalamika sana kuhusu kukatika ovyo kwa umeme lakini akawapa jibu moja la ovyo sana "NENDA KASHIKE WAYA ULE KAMA HAKUNA UMEME". Kwahiyo mpk last week hakukuwa na tofauti yoyote chini ya JPM na SSH. Shida kubwa imeanza kuanzia J3 mpk leo kila siku wanakata umeme asbh mpk jioni.
Acheni upumbavu jamani!

Jk alikuwa na mgao wa umeme wa kufa mtu!

Magufuli hakuwa na mgao kabisa wa umeme...!

Samia kaingia tu tayari mgao, hebu twambieni huyu mnaemlaumu yeye alikuwa anatumia mitambo ipi?
 
Hakuna jamii isiyo na Changamoto, hata huko Uswisi kwenye kila kitu bado changamoto zipo!! Ni wakati sasa wa hii Serikali ya akina Samia kupambana kutatua hizo changamoto!! Hili tatizo la umeme na maji lipo muda mrefu sana, na kila serikali inayoingia madarakani haioneshi nia ya dhati kulitatua hilo zaidi ya matamko na politics za majukwaani na kutafuta sifa za kijinga!! Swali ni kuwa je hii serikali ya sasa itaweza kutatua hili tatizo na tulisahau kabisa TZ? Tusubiri tuone, muda siku zote huwa unajibu!! Ila sishauri watumie zile njia za dharula za kutatua tatizo hili zilizotumika awamu ya 3 na 4 ambazo baadaye ziliingiza nchi kwenye mikataba ya hovyo kabisa.
 
Unaweza kuleta ushahidi hapa kuhusu miaka 99 ya bandari ya Bagamoyo? Na Kikwete kuchukua 10% ya mkataba wa gas?
 
Sisi tunazungumzia mgao wa umeme ndugu yeye samia Atawale atakavyo kwa kuifungua nchi au vyovyote atakavyoona inafaa , lakin sio kuweka mgao wa umeme
Ikibidi mgao utakuwepo (Kutokana na chanzo cha umeme tunachotumia), muhimu wapambane watatue hilo tatizo kwa muda mrefu ujao, bila blah blah za kisiasa na kuiingiza nchi kwenye majanga mengine ya kimikataba
 
Unaweza kuleta ushahidi hapa kuhusu miaka 99 ya bandari ya Bagamoyo? Na Kikwete kuchukua 10% ya mkataba wa gas?
Bora mara Mia tunge ingia makubaliano ya ujenz wa bandari na mabeberu kuliko wa China Una wajua wachina wewe watatujengea libandari lao watalitumia miaka 99 wakija kutuachia halifai tena kwa matumizi itabid serikal iingie galama za ujenz upya, alafu Wachina Wana njaa na wadokozi wa vitu vidogo vidogo tofauti na wazungu, Mim nimefanya kazi na Wachina nawajua vizur sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafikiri hukumwelewa Zitto vizuri. Issue iliyopo ni kwamba ktk miaka 5 hii hatukuongeza hata 1MW, je ni uongo? Na kama taifa lilishaingia gharama za kuanzisha miradi ambayo ingepunguza changamoto ya upungufu wa umeme, je ilikuwa ni sahihi kuzififisha jitihada hizo au zingeendelezwa na kuboreshwa pale palupokuwa na mapungufu! Kama mradi mkubwa unaojengwa utachukua takribani miaka 7 kukamilika je wimbo wa Tanzania ya viwanda ungeendelea kusubiri hadi mradi huo utakapo kamilika! Je unadhani kwa kusitisha jitihada za makusudi zilizokuwa na lengo la kupunguza chanagamoto ya upungufu wa umeme ilikuwa ni busara na njia sahihi ya uongozi au ni kuaminisha watu kuwa aliyepita hakufanya chochote cha maana ila mm ndiye ninayejua na kuweza kila kitu!
 
hahahah mkuu mbona mwendokasi inaendelea na sasa imefika asilimia 40? hebu punguzeni uongo bhana.....au wewe unaishi wapi ? umepita mawasiliano au umepita kariakoo na mbagala? au sio mradi wa mwendokasi ule? hahahaha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…