Tatizo la vipele vinavyotokana na kunyoa nywele kichwani chini ya kisogo (Acne Keloidalis Nuchae)

Tatizo la vipele vinavyotokana na kunyoa nywele kichwani chini ya kisogo (Acne Keloidalis Nuchae)

Huu ugonjwa unatokana na fungus ambao wanakuwa super imposed by bacterial infection hivyo mgonjwa hatakiwi kukwangua nywele zote saluni kwani machine za kunyolea hupelekea maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine pia kunyoa nywele za kisogoni kuelekekea shingoni ni jambo linalochangia sana maambukizi ya ugonjwa huu...madereva wa magari na watu wanaofanya sana kazi za jasho hupata zaidi ugonjwa huu kwa kuwa jasho la kichwani likikutoka na likakaukia hupelekea maambukizi ya ugonjwa huu
Mkuu mimi nina tatizo la ndevu kuotea ndani (ingrown hair) naomba msaada.
 
mkuu hii dawa sina hakika kama inapatikana tz ,lakini naweza kukusaidia ikakufika kama upo dar weka detail zako ama ni pm niangalie naweza vipi kukusaidia . karibu sana.
Kwa mby naipataje na inauzwaje
 
Wakuu nimekutana na wanaume wengi wenye hili TATIZO, baadhi nimefanyanao mahojiano lkn wengi wanasema hawajui chanzo wameshituka tu wapo hivyo shieeda Ni nini Kwa anayejua jamani mawazo, maoni au ushauri!
Vinyozi, vinyozi ni shiida. Mi nakumbuka 2006 ilikuwa moro baada ya kunyoa saloon moja hivi tatizo la vipele kichwani likaibuka. Nilitumia dawa kibao hola zaidi ya kupungua. Nimeacha red meat zote,soda soda wapi
 
Aliniandikia dawa ya kupaka inaitwa candiderm cream na vidonge vya anti allergy kwa jina sivikumbuki nilikuwa nameza vinne kwa siku kwa muda siku 28. Pole Sana.
Angalau naanza kupata mwelekeo,hapo regency huyo Dr. bingwa anaitwa nani
 
Kaka naomba namba yako
Kaka polesana.hivo vipele kwanza kabla hujaanza kupaka dawa yeyote lazima uvibinye.vinakuwa na tundu ambapo ndiko unywele unachomokea. Ukibinya kinatoa uchafu mweupe kama chunusi.ikibidi ukitoboe na pini.hapo lazima uwe na MTU wa kukubinya.alafu upake Dawa inaitwa Fucide.ukimaliza kupaka utasikia pana washa maana kwamba dawa imeingia.inauZwa sh/6500.utanipa majibu.
 
Habari wakuu..
Kuna tatizo la kutoka na vijiuvimbe vidogo vidogo kama vipele sehemu ya nyuma ya kichwa karibu na shingo. Kuna yeyote anayejua chanzo chake na dawa ya tatizo hilo? Naomba msaada wenu..
 
Acha kuchonga nywele eneo lililo athirika baada ya kunyoa,kisha tumia mafuta ya kulainisha ngozi ulalapo hadi patakapo lainika. Mafuta hayo ni kama yale ya mgando ambayo mfano wake ni Vestiline petrolium jerry n.k
 
Wakuu na mimi hili tatizo limenipata. Nimekunywa vidonge mpaka basi. Msaada jamani.
 
Nasumbuliwa sana na vipele kichwani kwa muda mrefu,vinawasha na kutoa majimaji.Nimetumia dawa za kupaka na kunywa lakini bado tatizo haliishi.Mara nyingi nikitumia dawa vinaisha lakini baada ya muda vinarudi tena.Nimepima afya kuhusu hili gonjwa letu nipo salama.Hivyo basi naombeni ushauri nitumie dawa gani ili niweze kupona.
pole mkuu waone wataalamu wa ngozi kuna jamaa yangu nae aliupata ugonjwa kama huo yeye alienda hospitali akaandikiwa sindano kwa muda kama wa miezi mitatu alichoma mara tatu kama sijakosea now zimekauka na kashapona mara nyingi unasababishwa na bacteria huko masaluni tunapoenda kunyoa nywele hawazingatii usafi wa mashine zao zile hivyo tuwe waangalifu na hizi saluni zetu ikiwezekana kuwa na mashine yako ukienda kunyoa unaenda nayo unampa kinyozi anakunyoa na mashine yako..
 
Wataalamu njooni huku mtupe tiba,mi natamani nikawaone watu wa tiba asili.
 
Nasumbuliwa sana na vipele kichwani kwa muda mrefu,vinawasha na kutoa majimaji.Nimetumia dawa za kupaka na kunywa lakini bado tatizo haliishi.Mara nyingi nikitumia dawa vinaisha lakini baada ya muda vinarudi tena.Nimepima afya kuhusu hili gonjwa letu nipo salama.Hivyo basi naombeni ushauri nitumie dawa gani ili niweze kupona.
Vipi mkuu ulifanikiwa kupata dawa/
 
Back
Top Bottom