Tatizo Simba sio makocha bali uongozi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Utabadilisha makochaweee kuanzia Julio, Kibaden,......Omog lakini Simba itafungwa tu. Mfano, Tambwe aliachwa Simba akiwa mfungaji bora wa ligi, Niyonzima lazima acheze Simba hata kama ujanja wake umeshakwisha, Mwanjale alikuwa na kasoro gani hadi aachwe? . viongozi Simba wanaiwaza Yanga zaidi kuliko timu zoote za TFF, hii inasababisha Simba ifanye vizuri mashindano ya timu za nje kuliko ya ndani ya nchi. Simba hata ikicheza na Mgambo mawazo na akili yao yote iko Yanga
 
Yanga wanaume.Simba vivulana...Edo Kumwembe wasamehe hawa jamaa zako
 
Kilichosababisha Omog kufukuzwa Simba si sababu ya kufungwa, kwani mara ya kwanza kufungwa tangu ianzishwe?! Fikiri nje ya boksi kabla hujafungua uzi hapa JF
 
Kilichosababisha Omog kufukuzwa Simba si sababu ya kufungwa, kwani mara ya kwanza kufungwa tangu ianzishwe?! Fikiri nje ya boksi kabla hujafungua uzi hapa JF
Unataka kusema Kufungwa Simba na timu ya daraja la pili na kufukuzwa kocha hapohapo ni coincident tu? be serious!! Mbona unatofautiana sana na Hata MO mliki wa Simba aliyekasirikia kufungwa na kumtaka kocha ajiuzulu? Soma ujumbe wa MO kwenye fb alichopost baada ya timu kuvuliwa ubingwa.
 
Mkuu hakuna KIFO kinachokosa sababu OMOG alikua hatakiwi tangu yanga ilipochukua ubingwa,haliyakua iliachwa nyuma kwa point nyingi sana
Hata ujio huu wa huyu MRUNDI sijuwi mnyarwanda kuna watu walisema Omog hana chake
Sema tu ndio hivyo kaingia ktk 18
 
Viongozi wampangie OMOG timu ya kucheza,,, viongozi wanunuwe wachezaji bila kumshirikisha kocha,,, viongozi wao ni makocha,, wachambuzi wa soka,, mwisho wa siku OMOG HAFAI,,, wewe ni kiongozi,, unawezaje kusajili au kushinikiza mchezaji acheze au aachwe? Tatizo ni UONGOZI KUINGILIA MAJUKUMU YA KOCHA., Kwn duniani Simba ndy ya kwnz kufungwa na timu ya daraja LA 2?wachezaji hawachezi kwa moyo,,, pia ni tatizo,,, mchezaji wa kibongo akisha sifiwa anajuwa Mpira basi ANATUNISHA KIBYONGO,, anajiona ndy kila kitu,,,na timu pia haijitumi,,,
 
For sure umetaja maeneo ambayo Simba SC inakosea kwa kiasi kikubwa.
Leo Omog anaondoka,lakini hana nafasi ya kujitetea,kusikilizwa ili washabiki na wanachama waweze kuujua ukweli.Sana sana wote wameaminishwa na viongozi kwamba Omog is wrong na amestahili punishment hii.
Kwangu mimi, Omog is still the best coach ambaye Simba SC imempata ndani ya miaka hii mitatu au minne ya karibuni.With combination na Mayanja, Omog bado angeweza kutuvusha.Nilivyoona Mayanja anaondoka nilijua Omog's days are numbered.
Leo hii tuweke kumbukumbu sawa kwamba:
1.Omog anatuacha nafasi ya kwanza VPL.
2.Omog anatuacha na tiketi ya Confederation Cup ya Afrika.
3.Omog anatuacha na kikombe cha ASFC/F.A.
4.Omog tunamuacha akiwa anahitaji kututumikia.
Kwangu mimi, kukaa mezani na Omog ingependeza zaidi kuliko kuutumia msemo wa "coaches are hired to be fired" pasi na sababu.
Kila la kheri Omog, kila la kheri Simba SC.
 

Attachments

Huna haja ya kusikitika kazi ya ukocha kwasasa ndo kazi nzuri maana km mkataba unaisha unapewa chao unasepa. Lkn pia Omog alikuwa ni mzuri sio kihivyo usemavyo ana safari alikuta simba imeanza kutulia kimapato hs mishahara la asingeweza kufanya hayo aliyofanya. Omog kwasasa ameshindwa kuwatumia wachezaji aliowapata naona upole ulizidi Sana. Pia Omog alishindwa kuwa na timu ya kwanza pia ushindi wa Omog muda wt ulikuwa WA Mashaka Sana kwa simba. Hb fikiria simba iliongoza point nane lkn ikaja kupitwa. WAchezaji viwango vyao vinaporomoka lkn anapangwa tu. Hb mwangalie mzamiru WA mwaka huu hayupo lkn anaacha kumtoa anamtoa nje mwinyi. Yapo makosa mengi ambayo Omog alikuwa dhaifu sna hasa Baada ya kuondoka mayanja Hapo udhaifu WA Omog ulipoonekana dhahiri. Pia wachezaji wetu wana matatizo hasa wazawa hawa nao tuwaseme hawajitambui kbs angalia mzamiru kapotea kbs na wengineo wapo mishahara wanapata kucheza ni tatizo je wakikosa mshahara inakueje Hapo. Naunga mkono uongozi kukuondoa Omog maana timu ilikuwa inazama wakati ina kila kitu kwasasa.. Kuna mwandishi mmoja anasema timu iliandaliwa na kocha msaidizi kusahau kuwa falsafa na kupanga timu Omog alipokuja alizitumia zake Omog...
 
Ajabu sana mkuu, , timu yetu hii,, yaani ufukuze kocha timu ingali inaingoza ligi,,,
 
Club ya Simba pamoja na washabiki wake wooote hawana akili timamu, kila mara nimekuwa nikisema hili.

Thinking tank ya simba ni wale wazee wa msimbazi waliokuwa sababu ya kuondoka makocha waliopita kabla ya Omog na hawana jipya lolote.

Oooh Manji...oooh...!

Kuwa shabiki wa Yanga kuna raha yake wallah.
 
Jiangalie ndugu...kuwa na kauli nzuri....kwahiyo na nyie shabik wa yanga wote matahiraaaaa
 
Mkataa pazuri pabaya panamngoja! Sasa sijui Simba wanataka nini?
Basi wamrudishe Patrick Phiri
 
Still lawama zangu nitazielekeza kwa wachezaji na viongozi.
1.wachezaji(baadhi yao) wamekosa spirit ya kupambana.Kocha anatimiza majukumu yake ambapo wachezaji anawaassign cha kufanya.Sometime game plan inabadilika lakini huoni wachezaji wakijituma,wakijitutumua kuitetea Brand ya Simba SC.Hili ni tatizo.
2.viongozi wamejitwisha majukumu yaso yao.Hiki kitu ni cha kawaida sana kwa Simba na Yanga.Mipango ya usajili wanaifanya wao.Kila kiongozi ana wachezaji wake na at the same time,wanamshinikiza kocha nani aanze na nani asianze.Kwa mfano Niyonzima alikuwa wa nini Simba? Tulimuhitaji wakati ule anatoka Kigali kabla hajatua Kuala Lumpur (Yanga) ambako ameitumikia kwa muda mrefu na kwa mafanikio makubwa lakini ndo huyo tunae.
Aaah, kila la kheri Omog kila la kheri Simba SC.
 
Tukumbushane Hans van Pluim alifukuzwa Yanga ikiwa nafasi ya ngapi?
 
Nyi mnaoshabikia hii mitimu ya simba n.a. yanga mnajitia presha bure ,,,,, Me binafsi nilishaachaga ushabiki wa hii mitimu kitambo,, SIMBA na yanga ilikuwa zamani,
 
Mkataa pazuri pabaya panamngoja! Sasa sijui Simba wanataka nini?
Basi wamrudishe Patrick Phiri
Si ajabu! Ukiangalia utabaini kwamba ili adumu na timu, kocha wa Simba lazima awe ‘Hewalla bwana’ kwa Uongozi.Aridhie kutafutiwa wachezaji. Aridhie kupangiwa timu. Aridhie kuingizwa maneno ya viongozi mdomoni mwake kwa yeye kubaki kimya (kama alivyosemekana Phiri kutomtaka Amisi Tambwe kwenye kikosi), aridhie wachezaji kuamriwa kucheza chini ya kiwango na baadhi ya viongozi, aridhie lawama za timu kushindwa licha ya kasoro zote hizo. Na hatimaye aridhie ‘kusitishwa mkataba wake kwa maslahi ya pande zote mbili’. Phiri, Omog, Mrhm Sianga (ingawa yeye alidumu muda mrefu kutokana na wachezaji walioletwa enzi zake kuwa wazuri na kwa hivyo wakambeba) ndio makocha sahihi wa Simba kwa mintarafu hiyo. Logarusic, Kyerr, Kopunovic, Kibadeni/Julio Na kama hao hawawezi kubaki salama ndani ya Simba kwa sababu hawawezi kukubali mambo hayo.
 
Yanga walishastuka mapema kuhusu tatizo la kusajili na kumpangia Kikosi kocha. Wachezaji anaowakuta kocha sio issue. Lakini kumsajilia Karne hii eti kwa kuwa Makofia kuona mzuri ni uzwazwa mkubwa sana.
Hivi kwa nini mtu kama Hans Pope asiwe kocha kabisa? Kaburu vile vile.
Hata suala la kocha msaidizi. Kocha yafaa atafute mwenyewe mtu wa kumsaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…