Tatizo sio ada bali ubovu wa mitaala ya elimu yetu

Baada ya kuandika hivyo,ilibidi utoe ushauri wa namna huo mtaala mpya unavyotakiwa uwe,jinsi unavyofanyakazi na output yake inakuaje, otherwise utakua umeongea kitu ambacho na wewe huna idea nacho
 
Kila kitu ni hatua, hakika ni mwanzo mzuri pia, hata hiko kidog kinachopatikana kwenye mitaala iliyopo basi tukipate wote.

Kwahiyo hii hatua nayo sio kazi bure itanufaisha kwa namna yake.
 
Kibaka ni tabia tu sio kwasababu amekosa elimu mzuri shuleni,

We huoni huko kuna watu wamesomeshwa kwenye shule na vyuo bora duniani lakini wapo wanatuibia kodi zetu huko wanaingiza mfukoni mwao,

Usifanye mchezo na tabia ww hata umpe elimu ya namna gani atadokoa tu.
 
Ada siyo tatizo kama ulivyosema,tatizo kubwa na utitiri wa vifaa na fedha za michango.michango pekee yake kwa mwanafunzi wa kidato cha tano ni zaidi ya milioni moja wakati ada ni 75,000 tu kwa mwaka.kuna vitu ambavyo vinamwumiza mzazi lkn serikali havioni,km vitabu,karatasi,godoro,pesa ya umeme,walinzi,mitihani,stationery,vifaa vya chakula,malazi,matibabu,gharama za safari na posho za mjiani nk ndo vinavyoumwumiza.mzazi ada ni danganya toto tu.leo hii mtoto anatoka bukoba na amepangiwa songea hebu fikiri mzazi atatumia kiasi gani?
 
Ni kweli kabisa.
Hakuna mjadala wowote Wa kitaifa uliofanyika Ili kufuta ada za Sh. 40000 Kwa shule za sekondari halafu Mtoto huyo huyo Wa maskini akifika Chuo anakosa mkopo na akipata anapewa 40% ,Kisha Mzazi anaenda kuuza nyumba mtoto asome Chuo Ili apate ujuzi. Akimaliza Chuo hakuna ajira , mtoto anaajiriwa kuendesha bodaboda Kwani Mzazi Hana uwezo Wa kumnunulia ya kwake binafsi.
Ni aibu Kwa Taifa Kuwa na wasomi wanaowaza kupata kura na vyeo Ili wakasomeshe watoto Wao Shule za gharama kuanzia nursery mpaka form six.

Kwa Nini sekondari wasiendelee kulipa Ada japo kidogo Ili serikali iwekeze kwenye Elimu ya Juu na Elimu za ufundi.

Hii nchi Ina fedha nyingi tatizo ni matumizi mabaya ya akili na matumizi yake.
JKT mafunzo yanatolewa Bure.
Darasa la kwanza mpaka kidato cha Sita Bure.
Magereza Bure.
Wabunge posho kubwa
Mawaziri matumizi makubwa.
Ndege zisizo na faida.
Sekondari kila Kata bila Miundo mbinu mizuri na Walimu.

Mwenge unatumia pesa nyingi kuliko miradi inayozinduliwa.
Misafara mikubwa ya viongozi.

Kiinua mgongo Kwa Mbunge na diwaniambao hawajastaafu.

Mikopo inatolewa kisiasa kila Halmashauri matokeo yake hakuna Marejesho. Pesa zinapotea na uchaguzi unaofuata MTU anapata kura Ili alee familia yake huku akiacha Taifa likijiendesha kwa mikopo.

Yote hayo ni matumizi mabaya ya Kodi kwenye nchi maskini.
 
Naunga mkono hoja, mfumo mzima wa Utoaji wa ELIMU ktk Ngazi zetu iangaliwe upya. KATIBA mpya iliangalie Hilo.

1. Mitaala iendane na mahitaji ya Karne ya 21. ELIMU ilenge kumsaidia anaehitimu kutumia mazingira yaliyopo kujiajiri.

2. ELIMU ya msingi itolewe Kwa miaka 4 pekee.
Hivi sasa mtoto wa kike anabalehe akiwa na miaka 8, pia life span imepungua, ni vzr muda wa Utoaji ELIMU iendane na mazingira sasa.

3. Chakula mashuleni kitolewe Bure kuanzia upili, msingi na kuendelea. Serikali ishirikiane na MZAZI kufanikisha Hilo, Tulifanikiwa miaka 50 iliyo pita, tunaweza Leo na zaidi.

4. Mwalimu anafundisha ELIMU ya msingi awe na ELIMU ya Juu kuanzia Degree kwenda juu, Hawa form 4 hawafai.

5.Uzalendo ufundishwe mashuleni na ELIMU ya kujitegemea ifundishwe kuanzia level za chini.

6. Mtoto aangaliwe KIPAWA alichozaliwa nacho kiendelezwe, mf mwenye kipaji Cha mpira wa miguu, apelekwe shule màalum tangu awali.

Mengine mtaongezea wadau. Amen
 
Tuna WATU Wa ajabu sana kwenye nchi za Kiafrika.

Yani MTU Msomi kabisa anafuta ada ya sh.70,000/ Kwa mwaka halafu anamtoza mtoto huyo huyo ada ya mil.2 anapoingia Elimu ya Chuo kupata ujuzi.
MTU aliyeshindwa kulipa Ada ya sh. 70,000/- atawezaje kulipa mil.2 kusoma Diploma. ??

Shule za Boarding zitakua na changamoto nyingi sana mana Kuna masuala ya maji,umeme, matengenezo, madawati yanavunjika, umeme unapata shot, taa zinaungua, mabomba yanavuja n.k. Stationary n k. Chakula n.k. Huduma hizo Mzazi Kuzichangia Hata kidogo ni haki na wajibu. Haiwezekani kukopa Ulaya mamilioni Kisha tunadanganya Kuwa tunauwezo Wa kusoma Bure.
Tangu WAKATI Wa Mwalimu ada ndogo zilikuwepo Ila watoto Wa maskini sana na yatima walipewa barua maalumu Toka Serikali za mitaa na ada Zao zilikua zinalipwa na Halmashauri anakotoka.
 
Hebu Tanguliza shukrani kwanza kwa kufutiwa hiyo Ada ndio uanze kukosoa .
Alietakiwa apate maoni ya wadau kabla ya kufuta hiyo 70,000/- njaa Kwa watoto ni tatz kubwa.

Kama wamelala njaa usiku familia, hata akienda shule asubuhi haezi elewa.

Viongozi Hawa ,hawakutokana na ridhaa ya wananchi.

Lazima wakosee Kila wanachofanya.

Pia hatuhitaji kuwapongeza wanapotimiza wajibu wao, VICHWA vitajaa maji.😠😠😠😠
 
Kwani hujui kwamba Serikali ya SSH inapitia mitaala yote na kuanzia mwaka 2023 watoto wataanza kwa kudoma mtaala mpya?

Samia sio mjinga kama wewe na yule aliyetaka wawe wanamuabudu na kujiweka kwenye vitabu vya Historia.
Serikali inatumwa na wananchi, HAIJIPANGII, bila kushirikisha wananchi ni kujisumbua tu.

Ya nini kujivisha USTARLING bandia? Mtu akikalia kiti anajiona ana akili kuliko BOSS alomweka pale ambaye ni MWANANCHI.

Uliza watu upate vitu, KATIBA mpya itatusaidia kutuondolea ujinga huu, yaan viongozi wanadhani Wana akiliii, kumbe wap.
 
Aliyekwambia Hawashirikishwi nani? Kutunga mfumo wa Elimu ni sawa na Katiba? Ndio maana kuna jopo likeundwa na linashirikisha makundi maslahi Ili kupata mitaala Bora..
 
Aliyekwambia Hawashirikishwi nani? Kutunga mfumo wa Elimu ni sawa na Katiba? Ndio maana kuna jopo likeundwa na linashirikisha makundi maslahi Ili kupata mitaala Bora..
KATIBA ni Sheria mama, marekebisho mengi kwenye mfumo wa ELIMU yanagusa Katiba hii tunavyolalamikia.

Hujiulizi inakuwaje kila Rais aliingia anakuja na yake?

Mfumo IMARA unatakiwa uwe na Dira ya miaka 100 au zaidi, huwezi kutumia akili ya waziri aliepo, na akiondoka anakuja mwingine na yake.
 
Unamdanganya nani? Sheria za Elimu na mambo ya katiba wapi na wapi? Kama hujui na huwezi fikia jopo Holo ujue huna maana yeyeto wala mchango wowote..

Badala ya kulaumu ungekuja na mapendekezo,jukwaa hili linasomwa na watu wa serikali Kwa hiyo weka mchango wako watachukua,kwani hujasikia Max akipongezwa Bungeni?
 
Ndugu unabishana Hadi ktk hili? Kwa uelewa wako suala la ELIMU halina mahusiano na KATIBA kimfumo?

Walokuajiri walitumia vigezo Gani kukupa KAZI?

Kuna msanii mmoja Jina anaitwa NYANDU: aliimba pale KIJANI L.Mumba ni NYUMBA ya matapeli hakukosea.
 
Ndugu unabishana Hadi ktk hili? Kwa uelewa wako suala la ELIMU halina mahusiano na KATIBA kimfumo?

Walokuajiri walitumia vigezo Gani kukupa KAZI?

Kuna msanii mmoja Jina anaitwa NYANDU: aliimba pale KIJANI L.Mumba ni NYUMBA ya matapeli hakukosea.
Jibu swali na onyesha ambapo mitaala inahusiana na Katiba..

Narudia Mitaala haihitaji makongamano ya Katiba.
 
Jibu swali na onyesha ambapo mitaala inahusiana na Katiba..

Narudia Mitaala haihitaji makongamano ya Katiba.
Kwako ni sawa, akitumbuliwa huyu waziri aliepo naye aje na mawazo yake?

ELIMU ni suala muhimu halihitaji siasa na utashi binafsi.

ELIMU ni suala la KIKATIBA pia nasisitiza, Mtu anapoongelea KATIBA usifikiri ni suala la UCHAGUZI pekee.

Katiba inagusa mifumo yote ya ELIMU, MAZINGIRA, UCHUMI, KILIMO, UFUGAJI,UTALII,. MUUNGANO, SIASA nk. Amen
 
Hili ni suala la serikali baada ya wadau kusema elimu haitoshi sio swala la Waziri.
 
Hawa ndio watanzania niwajuao mimi sasa HAWANA JEMA.
 
Haiwezekani, Haiwezekani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…