TAWA: Ongezeko la Tembo ni hatari kwa maisha na mali za watu, Mamlaka iruhusu Uvunaji wa Pembe kwa faida ya Nchi

Alafu baadae watalii si watapungua kuja huku? Au unafikiri wakija kutalii mbugani wanakuja kuangalia nyasi?
Kwa akili zako unadhani kuangalia mnyama kwenze zoo na kufanya utalii wa mbugani kunafanana? Ni sawa na kuogelea kwenye swimingpool halafu useme siendi baharini tena.
 
Ni uzembe tu wa kushindwa kuwadhibiti Wanyama pori ili hali Mwenyezi Mungu amempa Binaadamu mamlaka ya kuwasimamia.

Kuruhusu wavunwe kwa sisi Waafrika tusio na breki itakuwa balaa tupu.

Hiyo misitu yenyewe tunahimizana kila kukicha kuinusuru lakini uvunaji unatishia kuingamiza dunia.
 
Kwa akili zako unadhani kuangalia mnyama kwenze zoo na kufanya utalii wa mbugani kunafanana? Ni sawa na kuogelea kwenye swimingpool halafu useme siendi baharini tena.
Kama hao wanyama huku kwenye mbuga hawapo wamekwisha, watakuja kuangalia nyasi?
 
Kinana amerudi kwenye system, kwa hiyo tutegemee tembo kupungua kama siyo kuisha kabisa
 
Kabisa,huu ni sawa na uhuni tu

Ova
 
Wanataka tu kufanya mambo yao

Ova
 
Official hunting ni utaratibu ambao uko muda mrefu sana.
Yes kuna muda wanyama wanakuwa wengi kupitiliza wanawindwa kwa utaratibu maalum kupitia vibali.

Sent from my SM-A525F using JamiiForums mobile app
Miaka ya nyuma sawa
UN walikuja ifuta kwenye vikao vyao
19 nshasahau ...
Ndiyo ikaingia kwenye magendo

Ova
 
Ni ushauri wa ajabu sana sana

Tusiangalie ongezeko la tembo kwenye mbuga zetu pekee, tuangalie na mbuga za nchi jirani gukaanzeshe zoo za ushirikiano huko.

Huyu jamaa nimemtoa maana kabisa
 
Japokuwa alichokisema ni sahihi kwa namna moja au nyingine, ila nina mashaka kama atadumu kwenye hiyo nafasi kwa kuongea ukweli na kitaalamu. Binafsi huwa naziangalia kwa jicho la kipekee NGOs zinazokuwa zimejipa jina la watetezi wa jambo fulani, wengi wao huwa wapo katika harakati za kisiasa kuimarisha maslahi ya Taifa fulani dhidi ya wapinzani wake.Ninaamini wale wenzangu tuliosoma Cuba watakuwa wamenielewa.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Angetuambia miaka kama 20 hivi iliyopita, walikuwepo tembo wangapi na walikuwa wanatumia eneo kubwa kiasi gani kwa malisho.

Kisha atuambie sasa kuna tembo wangapi huku eneo lao la malisho likiwa limepungua kutoka sq kilometers kadhaa kwenda sq kilometers hizi.

Kinyume na hapo ni porojo tu za kutaka kuhalalisha uwindaji haramu.

Na ningekuwa mimi ni mamlaka yake ya uteuzi ningelia nae.

Tembo kutoka kwenye maeneo yao ya uhifadhi kwani yameaanza leo?

Miaka ya Sabini nikiwa primary, tembo aliingia maeneo ya wananchi huko Rombo akauliwa na wananchi wakachukua kitoweo.

Hakuna aliyekuja na wazo la kutaka kuhalalisha uwindaji wa Tembo maana Mwalimu Nyerere asingemvumilia.

Tuache kutafuta 'simple solutions' bali tumieni Bongo zenu vizuri!
 
Mapori makubwa mengi tu na yenye kuruhusu Ecology ya Tembo

Kwanini tusifanye Translocation...fedha zipo kama njugu kwenye Taasisi za UHIFADHI Kimataifa
 
Mhifadhi upo Mkuu...
 
Yuko sahihi.
Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma tembo wanaharibu mazao ya wananchi na kuua watu mara kwa mara.
Tembo ni wengi mno huko Liwale, Tunduru na sehemu nyingine
 
Tembo anazaa Kila baada ya miaka mitano.

Tumeshuhudia Uuaji wa tembo ukatishia KUTOKOMEA Kwa Hawa viumbe


Yaaan Kisa tembo wetu wachache walobakia, kuingia kwenye mashamba ya watu na kusumbua.

Ndo imegeuka kua ni Wengi 🤣🤣🤣


Huu Ujinga na Maneno kama haya Kwa Hayati JPM yasingekuwepo kabisa
 
Hamna Cha tembo kuzidi, ni uongo na uzushiii.

Tembo wengi wameuliwa kipindi Cha Kikwete.

WAKATI wa JPM ndo hii biashara ikakoma .

Tembo anazaa Kila baada ya miaka mingapi??


Makamo Mwenyekiti wa chama anadhan Tanzania ni ileile ya wajinga.
 
Kaimu ..Kamishina .

Kama sio Tukio linaloongozwa na Makamo Mwenyekiti wa Chama, basi Kaimu Anataka amfurahishe Makamo Mwenyekiti ili asiwe kaimu .


Makamo na genge lake, Wana tabia ya kuchomekea Kitu, ili wasikilizie mwitikio wa watanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…