TAWA: Ongezeko la Tembo ni hatari kwa maisha na mali za watu, Mamlaka iruhusu Uvunaji wa Pembe kwa faida ya Nchi

TAWA: Ongezeko la Tembo ni hatari kwa maisha na mali za watu, Mamlaka iruhusu Uvunaji wa Pembe kwa faida ya Nchi

Alafu baadae watalii si watapungua kuja huku? Au unafikiri wakija kutalii mbugani wanakuja kuangalia nyasi?
Kwa akili zako unadhani kuangalia mnyama kwenze zoo na kufanya utalii wa mbugani kunafanana? Ni sawa na kuogelea kwenye swimingpool halafu useme siendi baharini tena.
 
Ni uzembe tu wa kushindwa kuwadhibiti Wanyama pori ili hali Mwenyezi Mungu amempa Binaadamu mamlaka ya kuwasimamia.

Kuruhusu wavunwe kwa sisi Waafrika tusio na breki itakuwa balaa tupu.

Hiyo misitu yenyewe tunahimizana kila kukicha kuinusuru lakini uvunaji unatishia kuingamiza dunia.
 
Kwa akili zako unadhani kuangalia mnyama kwenze zoo na kufanya utalii wa mbugani kunafanana? Ni sawa na kuogelea kwenye swimingpool halafu useme siendi baharini tena.
Kama hao wanyama huku kwenye mbuga hawapo wamekwisha, watakuja kuangalia nyasi?
 
Kinana amerudi kwenye system, kwa hiyo tutegemee tembo kupungua kama siyo kuisha kabisa
 
Huyu aache uhuni hakuna tembo walioongezeka. Tembo walipungua sana zikaundwa kila kampeni kuwalinda, wakatumika kila aina ya wasanii na watu maarufu kupiga vita mauaji ya tembo. Aache ujinga huyu ana beep hapo.

Ila mama amezidi kuwa mpole, mtu Kama huyu anayezungumza hivi ilipaswa amuweke pembeni faster tu
Kabisa,huu ni sawa na uhuni tu

Ova
 
Kumbuka meli ya makamu mwenyekiti ilikutwa na pembe za ndovu akadai alikuwa hajui ni mzigo gani umepakiwa.... lakini Mzee wa Kino tukumbuke mzigo hadi uingizwe melini kuna ukaguzi ambapo mwenye meli hutoa bill of lading kuthibitisha kapokea mzigo husika na idadi yake. Mimi naona kama makamu anarudi kwenye biashara yake kinamna.
Wanataka tu kufanya mambo yao

Ova
 
Official hunting ni utaratibu ambao uko muda mrefu sana.
Yes kuna muda wanyama wanakuwa wengi kupitiliza wanawindwa kwa utaratibu maalum kupitia vibali.

Sent from my SM-A525F using JamiiForums mobile app
Miaka ya nyuma sawa
UN walikuja ifuta kwenye vikao vyao
19 nshasahau ...
Ndiyo ikaingia kwenye magendo

Ova
 
Imeelezwa kuwa ongezeko la Wanyamapori Nchini limekuwa chachu ya kuwa na ongezeko la ushawishi wa ujangiri, uvamizi wa maeneo ya Wananchi ambapo humesababisha uhasama kati ya mamlaka za Serikali na Wananchi.

View attachment 2354405

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wananyamapori Tanzania (TAWA), Mabula Misungwi Nyanda ameyasema hayo Mkoani Dar Es Salaam 10 Septemba 2022 alipokuwa aliongea na Wanahabari kwenye hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve)

Amesema ongezeko hilo la Wanyama hasa Tembo limekuwa na madhara na inapotokea kunatakiwa kufanyika uwindaji kumekuwa na vikwazo kutoka kwa watetezi wa Haki za Wanyama ambao hawataki Tembo Wavunwe kwa Manufaa ya Nchi.

Kamishna Nyanda anasema: “Idadi ya Wanyama inaongezeka lakini ardhi haiongezeki, Tanzania tunatakiwa kuonesha tunapata faida kutokana na Wanyama tulionao.

“Hata kisayansi inaeleza kuwa kuna hatua inafika inabidi Wanyama wapunguzwe, wasipopunguzwa matokeo yake ndio kama hivyo tunasikia wanavamia makazi ya watu na kufanya uharibifu na wakati mwingine kuua watu.

“Ndio maana tuna kanuni kuwa lazima ifike hatua Wanyama lazima wawindwe na wauliwe kwa faida ya Nchi.

“Mfano Tembo kwa sasa wamekuwa wakihusika katika matukio mengi ya mauaji na uharibifu wa mali, kama hakutakuwa na kitu cha ziada kuokoa hali hii hali inaweza kuzidi kuwa mbaya.

“Tunashauri Serikali iruhusu uwindaji halali wa Tembo kwa maelekezo maalum, ambayo ni kuwinda Tembo wazee na madume hadi itakapobaki idadi fulani ambayo inakuwa haina madhara kwa kiasi kikubwa.

“Inapotokea uwindaji wa aina hiyo kisha pembe za ndovu zikauzwa, Nchi inapata faida, hiyo ni nzuri badala ya kusikiliza NGO ambazo nyingine kwao hazina hata mbuga lakini zinakuwa Hodari katika kusimamia Wanyama kutopunguzwa wakati madhara tunapata sisi. Kama nchi tunao uwezo wa kuangalia Sheria na kanuni zetu, hizi pembe za ndovu zikiuzwa zinaweza nufaisha nchi kwani ni Maliasili yetu.

“Hata kama mamlaka haitatoa ruhusa hiyo, kumbuka kuwa kadiri Tembo wanavyosababisha madhara kwa wananchi ndivyo ambavyo nao (Tembo) wanakuwa hatarini kuuawa kinyume cha sheria na haohao Wananchi.” Pia inaongeza uhasama kati ya Serikali na Wananchi wake.

=====

MY TAKE
Six African Nations Agreed to Push for Restarting Ivory Trade
31 May 2022

With the elephant population growing out of control in parts of southern Africa, several countries in the region agreed at a conference to support Zimbabwe’s push for the legalization of the international ivory trade.

Last week’s conference, organized by Zimparks, Zimbabwe’s wildlife management authority, was attended by representatives of Botswana, Namibia, South Africa, Tanzania and Zambia.

Ni ushauri wa ajabu sana sana

Tusiangalie ongezeko la tembo kwenye mbuga zetu pekee, tuangalie na mbuga za nchi jirani gukaanzeshe zoo za ushirikiano huko.

Huyu jamaa nimemtoa maana kabisa
 
Imeelezwa kuwa ongezeko la Wanyamapori Nchini limekuwa chachu ya kuwa na ongezeko la ushawishi wa ujangiri, uvamizi wa maeneo ya Wananchi ambapo humesababisha uhasama kati ya mamlaka za Serikali na Wananchi.

View attachment 2354405

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wananyamapori Tanzania (TAWA), Mabula Misungwi Nyanda ameyasema hayo Mkoani Dar Es Salaam 10 Septemba 2022 alipokuwa aliongea na Wanahabari kwenye hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve)

Amesema ongezeko hilo la Wanyama hasa Tembo limekuwa na madhara na inapotokea kunatakiwa kufanyika uwindaji kumekuwa na vikwazo kutoka kwa watetezi wa Haki za Wanyama ambao hawataki Tembo Wavunwe kwa Manufaa ya Nchi.

Kamishna Nyanda anasema: “Idadi ya Wanyama inaongezeka lakini ardhi haiongezeki, Tanzania tunatakiwa kuonesha tunapata faida kutokana na Wanyama tulionao.

“Hata kisayansi inaeleza kuwa kuna hatua inafika inabidi Wanyama wapunguzwe, wasipopunguzwa matokeo yake ndio kama hivyo tunasikia wanavamia makazi ya watu na kufanya uharibifu na wakati mwingine kuua watu.

“Ndio maana tuna kanuni kuwa lazima ifike hatua Wanyama lazima wawindwe na wauliwe kwa faida ya Nchi.

“Mfano Tembo kwa sasa wamekuwa wakihusika katika matukio mengi ya mauaji na uharibifu wa mali, kama hakutakuwa na kitu cha ziada kuokoa hali hii hali inaweza kuzidi kuwa mbaya.

“Tunashauri Serikali iruhusu uwindaji halali wa Tembo kwa maelekezo maalum, ambayo ni kuwinda Tembo wazee na madume hadi itakapobaki idadi fulani ambayo inakuwa haina madhara kwa kiasi kikubwa.

“Inapotokea uwindaji wa aina hiyo kisha pembe za ndovu zikauzwa, Nchi inapata faida, hiyo ni nzuri badala ya kusikiliza NGO ambazo nyingine kwao hazina hata mbuga lakini zinakuwa Hodari katika kusimamia Wanyama kutopunguzwa wakati madhara tunapata sisi. Kama nchi tunao uwezo wa kuangalia Sheria na kanuni zetu, hizi pembe za ndovu zikiuzwa zinaweza nufaisha nchi kwani ni Maliasili yetu.

“Hata kama mamlaka haitatoa ruhusa hiyo, kumbuka kuwa kadiri Tembo wanavyosababisha madhara kwa wananchi ndivyo ambavyo nao (Tembo) wanakuwa hatarini kuuawa kinyume cha sheria na haohao Wananchi.” Pia inaongeza uhasama kati ya Serikali na Wananchi wake.

=====

MY TAKE
Six African Nations Agreed to Push for Restarting Ivory Trade
31 May 2022

With the elephant population growing out of control in parts of southern Africa, several countries in the region agreed at a conference to support Zimbabwe’s push for the legalization of the international ivory trade.

Last week’s conference, organized by Zimparks, Zimbabwe’s wildlife management authority, was attended by representatives of Botswana, Namibia, South Africa, Tanzania and Zambia.

Japokuwa alichokisema ni sahihi kwa namna moja au nyingine, ila nina mashaka kama atadumu kwenye hiyo nafasi kwa kuongea ukweli na kitaalamu. Binafsi huwa naziangalia kwa jicho la kipekee NGOs zinazokuwa zimejipa jina la watetezi wa jambo fulani, wengi wao huwa wapo katika harakati za kisiasa kuimarisha maslahi ya Taifa fulani dhidi ya wapinzani wake.Ninaamini wale wenzangu tuliosoma Cuba watakuwa wamenielewa.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Angetuambia miaka kama 20 hivi iliyopita, walikuwepo tembo wangapi na walikuwa wanatumia eneo kubwa kiasi gani kwa malisho.

Kisha atuambie sasa kuna tembo wangapi huku eneo lao la malisho likiwa limepungua kutoka sq kilometers kadhaa kwenda sq kilometers hizi.

Kinyume na hapo ni porojo tu za kutaka kuhalalisha uwindaji haramu.

Na ningekuwa mimi ni mamlaka yake ya uteuzi ningelia nae.

Tembo kutoka kwenye maeneo yao ya uhifadhi kwani yameaanza leo?

Miaka ya Sabini nikiwa primary, tembo aliingia maeneo ya wananchi huko Rombo akauliwa na wananchi wakachukua kitoweo.

Hakuna aliyekuja na wazo la kutaka kuhalalisha uwindaji wa Tembo maana Mwalimu Nyerere asingemvumilia.

Tuache kutafuta 'simple solutions' bali tumieni Bongo zenu vizuri!
 
Mapori makubwa mengi tu na yenye kuruhusu Ecology ya Tembo

Kwanini tusifanye Translocation...fedha zipo kama njugu kwenye Taasisi za UHIFADHI Kimataifa
 
Angetuambia miaka kama 20 hivi iliyopita, walikuwepo tembo wangapi na walikuwa wanatumia eneo kubwa kiasi gani kwa malisho.

Kisha atuambie sasa kuna tembo wangapi huku eneo lao la malisho likiwa limepungua kutoka sq kilometers kadhaa kwenda sq kilometers hizi.

Kinyume na hapo ni porojo tu za kutaka kuhalalisha uwindaji haramu.

Na ningekuwa mimi ni mamlaka yake ya uteuzi ningelia nae.

Tembo kutoka kwenye maeneo yao ya uhifadhi kwani yameaanza leo?

Miaka ya Sabini nikiwa primary, tembo aliingia maeneo ya wananchi huko Rombo akauliwa na wananchi wakachukua kitoweo.

Hakuna aliyekuja na wazo la kutaka kuhalalisha uwindaji wa Tembo maana Mwalimu Nyerere asingemvumilia.

Tuache kutafuta 'simple solutions' bali tumieni Bongo zenu vizuri!
Mhifadhi upo Mkuu...
 
Yuko sahihi.
Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma tembo wanaharibu mazao ya wananchi na kuua watu mara kwa mara.
Tembo ni wengi mno huko Liwale, Tunduru na sehemu nyingine
 
Tembo anazaa Kila baada ya miaka mitano.

Tumeshuhudia Uuaji wa tembo ukatishia KUTOKOMEA Kwa Hawa viumbe


Yaaan Kisa tembo wetu wachache walobakia, kuingia kwenye mashamba ya watu na kusumbua.

Ndo imegeuka kua ni Wengi 🤣🤣🤣


Huu Ujinga na Maneno kama haya Kwa Hayati JPM yasingekuwepo kabisa
 
Ona mwanadam alivyokuwa mbinafsi
Anajiona kama yeye ndiyo Ana hakimiliki ya kuishi duniani
Mnaposema tembo wamezidi ina maana mnataka muwapunguze kwa kuwaua!
Kwanini msiwahamishe wapelekwe
Kwenye mbuga zingine
Hii ni roho na tamaa mbaya ya mwanadam

Ova
Hamna Cha tembo kuzidi, ni uongo na uzushiii.

Tembo wengi wameuliwa kipindi Cha Kikwete.

WAKATI wa JPM ndo hii biashara ikakoma .

Tembo anazaa Kila baada ya miaka mingapi??


Makamo Mwenyekiti wa chama anadhan Tanzania ni ileile ya wajinga.
 
Kaimu ..Kamishina .

Kama sio Tukio linaloongozwa na Makamo Mwenyekiti wa Chama, basi Kaimu Anataka amfurahishe Makamo Mwenyekiti ili asiwe kaimu .


Makamo na genge lake, Wana tabia ya kuchomekea Kitu, ili wasikilizie mwitikio wa watanzania
 
Back
Top Bottom