Tazama harusi ya kigogo wa CHADEMA, Henry Kilewo alivyofunga ndoa na Joyce Kiria

kama ndoa ya kwanza ilikugharimu ni sawa kwa hii ukasahihisha makosa maana ni ndoa ya pili. inakuwa vigumu wa wale wanaofanya ndoa ya kwanza maana si rahisi kuwa na ya pili. sikumbuki kuona watu wanaachana na kuwa na ndoa nyingine kubwa maana ungelazimika kuchangisha watu wale wale walioshiriki ile ya awali. Je wangechanga?
 
Kwa wakirsto mnaruhusiwa kufunga ndoa mara mbili kanisani, huyu mwanamke ameishawahi kufunga ndoa kanisani na DJ wa Clouds FM Nelly, au sheria zimefanyiwa marekebisho.
 
uzinzi umebalikiwa..hamna ndoa hapo ,kwanza huyo mwanamke mtalaka! Kanisa gani hilo !?
 
Kwa wakirsto mnaruhusiwa kufunga ndoa mara mbili kanisani, huyu mwanamke ameishawahi kufunga ndoa kanisani na DJ wa Clouds FM Nelly, au sheria zimefanyiwa marekebisho.

Mbona mnajaa povu hivo na kanisa wakati kasema ndoa ya pili ni ya Bomani/serikali?
 

Kweli una wivu wa kike kama alivyosema mtu mmoja humu... Nani kakwambia Kilewo ni mchaga? Acha kukurupuka man. Fwata yako ya wanaume yatakushinda.
 
nadhani haikua harusi ila wamefunga ndoa
 
Katiba na sheria ya kanisa zimebadilishwa ..... Ndo mana joyce kaolewa mara mbili kanisani .....
Dini nyingine ni za kibiashara zaidi
 
Wachawi utawajua tu
 

Ndugu huwezi kuongea chochote bila kutaja hawa wa2!
 

Mathayo 5:31-32
Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
 

Kuna baadhi ya sababu zinalazimisha kanisa kutoa go ahead ya kuenda mahakamani kwa ajili ya talaka. Uzinzi uliokithiri, unyanyasaji kwa maana ya abuse na ugomvi usioisha. Sharti ni lazima kupitia baraza la wazee wa kanisa kabla ya kwenda mahakamani.
 
Mathayo 5:31-32
Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

Hebu tuwe serious. Kwa mfano binti kama huyo, mumewe alikuwa labda mzinzi ama anampiga, na wakaachana. Hivi kiimani tunategemea hatokaa aolewe tena ama hata kupata watoto kwa sababu ya dhambi ya mumewe? Tunaokolewa kwa neema, kwa njia ya imani. Ndo maana nampenda Mungu wa rehema na neema
 
Kuna baadhi ya sababu zinalazimisha kanisa kutoa go ahead ya kuenda mahakamani kwa ajili ya talaka. Uzinzi uliokithiri, unyanyasaji kwa maana ya abuse na ugomvi usioisha. Sharti ni lazima kupitia baraza la wazee wa kanisa kabla ya kwenda mahakamani.

Hakuna hata sababu moja ya msingi katika hizo ulizoandika inayopelekea ndoa kuvunjwa! Sababu pekee ni 1. Kama mume ni towashi kabla ya kufunga ndoa (siyo aupate akiwa kwenye ndoa). Pia kama mke au mume ana tatizo lolote litakalopelekea wasifaidi tendo la ndoa. 2. Undeclared children. Kwamba mmefunga ndoa halafu miezi michache baadaye linaletwa kundi la watoto wa mmojawapo wa wanandoa ambao hawakutajwa uwepo wao. Ama ikigundulika mmojawapo wa wanandoa alikuwa katika ndoa.


Biblia inaruhusu kutengana kwa muda kwa lengo la kurejeleana hapo baadaye, vinginevyo unless death do us apart. Ukimpenda Mungu utazishika amri zake, nothing less nothing more. Ndoa ni takatifu, ni lazima iheshimiwe na watu wote.
 

Kuna watu wana uelewa finyu kuhusu Biblia, ukiisoma vizuri utagundua kuwa inaruhusu Talaka ila kwa mashariti magumu. Maana maandiko yanasema; Mtu asimuache Mkewe/Mmewe isipokuwa kwa Uzinzi, kwa kosa la uzinzi mwanandoa aweza kumuacha mwenza wake, lakini mchakato huu utafanya na kanisa pamoja na wanandoa wenyewe kuanzia ngazi ya chini mpaka ngazi ya juu. Katika Ukristo ndoa ni kitu kinacho heshimika sana tofati na dini nyingine ambazo unaoa leo baada ya mwezi 1 ukijisikia kutoa talaka unatoa.
 

Kutengana kwa lengo la kulejeana ina maana gani?
 

Mkuu pamoja na uelewa wangu finyu, hakuna andiko linaloruhusu talaka katika biblia takatifu. Onesha hicho kifungu ili nami nipanue uelewa wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…