Hongera sana Joyce Kiria,hope ni Mrs Kilewo.MUNGU ni mwema sana,hatazami mambo kama sisi binadamu tunavyoyatazama...yeye si mwingi wa hasira bali mwingi wa rehema,husamehe bila kuhoji na hana kisasi,uhukumu kwa haki bila upendeleo na hutoa bila kuombwa.
Makosa yameumbwa kwa ajili ya mwanadamu,ubinadamu hutimia kwa kukiri madhaifu yetu na kuanza upya,kwani wewe ni nani hata usimkosee Mungu wako?kwani wewe ni nani hata Mungu asikusamehe na kuanza upya?
Nabii Daudi ambayo kwayo ukoo wa Yesu umetokea alimkasirisha Mungu,akiwa amejazwa na tamaa za mwili,alimpenda mke wa Huria,Daudi akiwa juu ya paa akizungukazunguka alimuona mke wa Huria ktk utupu wake,akaingia tamaa na kumtamani,ili kutimiza adhma yake akamuweka Huria mstari wa mbele ktk jeshi vitani,ili afe naye azini na mke wa Huria.
Alitimiza,lkn Mungu alimsamehe na kumuweka kama mfalme wa Mataifa,na ktk yeye ukoo wa Yesu ukazaliwa,kwani wewe ni nani usiye hata ktk ukoo wa Yesu na usitende dhambi?Mungu husamehe,tena katufunza tusamehe 7x70,Mwanamke Malaya aliyekimbia mikononi mwa Yesu ili asipigwe mawe alipona,si kwa sbb ya ubaunsa wa Yesu bali sbb ya hekima ya Yesu,aliyewataka makusanyo wasio na dhambi wawe wa kwanza kumtupia,wote walitawanyika abb hakukuwa na asiye na shambi.
Mungu hatazami kama mwanadamu anavyotazama,yupo tayari kuwaacha kondoo kenda walio zizini ili kumfuata mmoja aliyepotea,alimpa mamlaka Sauli aliyewatesa na kuwaua wafuasi wake,akampa upofu na Anania akamrudisha ktk nuru ili kumpa ushuhuda,hatimaye Sauli akabatizwa na kuitwa Paulo,akizunguka Samalia na Yudea kuutangaza habari njema.
Nayasema haya sbb kuna watu wameanza kuhukumu,wasijue lililo ndani yako na lililo ktk kusudi la Mungu,na wengine si kwa lolote,bali kwa chuki za kisiasa kwa mmoja wa waliofunga ndoa.
Tusihukumu ili tusije tukahukumiwa,kipimo kile tuwajaziacho wenzetu kwa kuwahukumu,ndio tutakachojaziwa na sisi.