TB Joshua kuzikwa Julai 11

TB Joshua kuzikwa Julai 11

Okay,
Wapopo wana mila mila sana, ni kama sherehe za harusi wanaweza fanya hata tatu na mbwembwe kibao za kuenzi tamaduni za makabila yao
Yes kule hata harusi huwa ni tatu na kubwa na hata msibani hawaliagi hovyo ka huku kwetu, kule huvaa Hadi sare kujipodoa hucheza ka harusini kumbe ni msibani
 
Kifo ni kuzaliwa katika Ulimwengu Mwingine ambao unaitwa Ulimwengu wa Roho.Kama ilivyo kuishi katika tumbo la Mama tukiwa watoto wachanga kisha tukazaliwa katika Ulimwengu wa Dunia ndivyo siri tuliyoumbiwa ya kuishi katika nafsi tofauti na ulimwengu tofauti.

Mtoto akiwa katika Tumbo la Mama yake,kama angepewa nguvu za mwili tunazozitumia Duniani yani Kutembea kutoka eneo moja kwenda jingine,na kufanya yale tunayofanya n.k.basi tumbo la mama linakuwa Dunia kwa mtoto ambae ameumbiwa kipindi cha miezi 9 kuishi katika ulimwengu wa tumbo.Na Kama kungekuwa na familia katika Ulimwengu wa Tumbo la Mama,mtoto akizaliwa ulimwengu wa dunia,ile familia wangechukulia amekufa na kuweka msiba ila hawajui duniani alikoelekea kukoje na tofauti ya kifo ni kwamba huko kinakuwa kifo cha kuondoka na Mwili wakati huku duniani kifo tunaacha Mwili Roho inaondoka nakuingia ulimwengu mwingine. Kwa hiyo katika Ulimwengu Mpya wanaompokea mgeni wanasema amezaliwa, ila alikotoka wale katika ulimwengu huo wanasema amekufa. Hivyo basi Njia ya Kuingia kwa Mwanadamu katika ulimwengu wa Dunia ni kwa kuzaliwa Kupitia Mwili wa Mwanamke,vivyohivyo njia ya kuingia Katika ulimwengu wa Roho ni kwa kuzaliwa kupitia Mwili wake Mwenyewe au Kufa.

Siri nyingine ni kwamba mtoto akiwa tumboni anategemea nguvu na msaada kutoka katika ulimwengu wa Dunia ambao Mama anamlisha,Pia Mtoto awezi kuuona ulimwengu wa dunia hata kama atapewa uwezo wa macho kuona zaidi ataona anga la majimaji lililomzunguka kama nasi tuonavyo mbingu na anga ila nje ya ulimwengu wa Dunia atuwezi kuona kwa Macho wala kuingia kwa Mwili.Hata Mwanadamu apate uwezo kiasi gani wa kitekinologia hawezi kuingia ulimwengu wa Roho bila kupitia katika Mwili wake Mwenyewe au Kufa.Kwenda anga za mbali na sayari zingine ni sawa na mtoto kuzunguka ndani ya tumbo la Mama yake ila akitaka kutoka nje ya tumbo mlango ni mmoja.

Kumbuka pia tunaweza kumuona mtoto na kufuatilia mwenendo wake wa ukuaji sisi tulio duniani lakini mtoto awezi kutufuatilia.Vivyo hivyo walio katika ulimwengu wa Roho wana uwezo wa kutufuatilia na kututawala kwa uzuri au kwa ubaya na hapo panatokea Mtawala Mkuu ambae ni Mwenyezi Mungu na Mshindani wake tunaemwita Shetani.

Katika kuzaliwa katika ulimwengu wa dunia tumenyimwa uwezo wa kuchagua tuzaliwe wapi,hivyo unajikuta umezaliwa Somalia,Tanzania au Ulaya na wengine wetu wamezaliwa kwenye familia zenye matatizo na wengine zenye raha na utajiri.Lakini katika kuzaliwa katika ulimwengu wa Roho tumepewa uwezo kuchagua ,tuzaliwa kwenye ufalme upi wa Nuru(Amani na Furaha) au giza(Matatizo).Nguvu ya Chaguo la wapi utaelekea inajengwa tukiwa hapa Duniani kutokana na Imani na matendo uliyoshikilia hivi sasa.
 
Wenzetu Magharibi wanaamini mtu akifa sio mwisho wake, kuna maisha mengine baada ya kufa. Na mazishi yao huwa ni more of a celebration, kufurahia maisha ya mpendwa wao hapa duniani na kumtakia kheri kwenye maisha yake mapya. So anapokufa wanamfanyia the so called befitting burial. Kwa hiyo lazima wachukue muda kujipanga kumfanyia hiyo sherehe, na ndiyo hapo inategema kati ya mtu na mtu (titles). Nakumbuka first time nasikia hili, kuna Nigerian Actor alikuwa anaitwa Justus Esiri alikuwa amefariki; imepita miezi miwili ndiyo nakuja kusoma eti anazikwa. Baba yake Yemi Alade na yeye alifariki January akaja kuzikwa May n.k

Hiyo befitting burial ndiyo unakuta jeneza la gharama, Aso ebi (sare, kama mnavyojua mishono ya kinigeria) + grand party. Na naonaga wanakuwa wanaimba na kucheza haswa (nawazia kilio cha wanyaki). So kwa wenzetu wakifiwa ni stress mara mbili; kwanza mmempoteza ndugu yenu, na pili ni gharama za mazishi; inakuwa kama mashindano sasa nani alizikika kifahari zaidi. Lakini kwa Northeners ambao wengi ni Muslims, mazishi yao ni chapchap kama kawaida.

IMG_9901.JPG
 
Ujinga na umaskini ni vitu vitakavyoendelea kuwatafuna waafrika milele. Muda wote huo, wanasubiri nini kuzika?
Mtu akifa inapaswa azikwe mara moja na mambo mengine ya kimaisha yaendelee.
We umeiga waarabu kuzika haraka
 
Mambo yenu tu hayo wakristo.
Sisi waislam haturembi, ukifa saa 2 ya hasbuh saa 7 mchana tunakufukia hiyo ni Dunia nzima.
 
Back
Top Bottom