TBC wanaandika Jenerali Musuguri alizaliwa 1920, Mkuu wa Majeshi ameandika katika taarifa rasmi, kwamba Musuguri alizaliwa 1925. TBC mjirekebishe

Ukiona hivyo ujue kuwa hiyo 1920 ndo sahihi zaidi kuliko 1925.
Miaka ya nyuma umri wa kuzaliwa ulikuwa una chakachuliwa kirahisi kwa sababu mbalimbali!
 
Viwango vimeshuka, kila sehemu. Sijui tutafikia kilele cha kushuka lini, ili tuanze kujenga upya. Tusipo bahatika, tutabaki huko huko chini, mithili ya Haiti!
Hatari sana.
 


Mkuu wa Majeshi Mstaafu ni Generali mwandamizi kuliko wote aliyekuwa hai ; INASIKITISHA SANA AMIRI JESHI MKUU ambaye ameondoka kwenda marekani analeta dharau kwa kumtuma Naibu Waziri Mkuu ( cheo Bandia) kumuwakilisha kwenye tukio zito kama hilo ….. angalau kama kashindwa angemtuma MAKAMU WA RAIS

HII inaonyesha ni Aidha Rais mwenyewe hajui uzito wa Generali Musuguri au tu wasaidizi wake wameamua kufharau au hawajaiva kimfumo

Mara zote misiba ya afisa na kamanda mpiganaji wa level ya CDF kama Rais yupo nchini wanatakiwa kufika yeye mwenyewe au msaidizi wake mkuuu.

Hizi ni dharau !!!!
 
Atkuwepo kwenye mazishi
 
Ukiona hivyo ujue kuwa hiyo 1920 ndo sahihi zaidi kuliko 1925.
Miaka ya nyuma umri wa kuzaliwa ulikuwa una chakachuliwa kirahisi kwa sababu mbalimbali!
Jeshi ndio lina jalada lake akiwa katika ajira, ye ye binafsi ndiye ali-disclose umri wake kwa jeshi
 
Atkuwepo kwenye mazishi
Tusubiri Ila Angeshangaza sana kama hivo Sawa ; ila kwa hadhi hiyo ingefaaa Makamu wa Rais amuwakilishe kwa Dar es Salaaam … kuliko kutuma mtu junior haileti heshima au imeshindikana Rais Mstaafu Atoshe kwa Dar ….
 
Mwl Jk Nyerere kazaliwa 1922 na ukiwaangalia kwenye picha yeye na nyerere wakiwa pamojo mwl anaonekana mkubwa
 
Tanzania a failed state
 
Mbona rahisi tu Mkuu, ukiingia Google ukaandika Musuguri atimiza miaka 100 utayapata Mahojiano haya aliyofanya na Azam TV miaka minne nyuma, kaeleza kila kitu. Alishiriki Misa na kufanya Tafrija fupi pia. Tuliheshimu Jeshi letu na vile linajitoa kwa moyo wa dhati pasi na kujibakiza kwa Usalama wa Tanzania na kesho yetu bora. Changamoto za kiuandishi zinarekebishika haipaswi kuwa sintofahamu kama ulivyowasilisha.
 

Attachments

  • Screenshot_20241030_063832.jpg
    267.6 KB · Views: 6
Kwa hili nawatetea TBC mkuu wa majeshi ndio kakosea,Musuguli alisherehekea kutimiza miaka 100,nakumbuka ni miaka michache imepita.
Sema wazee wa zamani walifoji sana umri
 
Nakumbuka miaka ya nyuma alitimiza miaka 100 ,sasa kama alizaliwa 1925 inakuwaje alitimiza miaka 100 siku hizo za nyuma?
 
Ule utaratibu wa kushika sikio ndio uanze shule miaka yao ndio uliasisiwa nini mana wazee wa zamani kweli wengi miaka wamepunguza. Wa 1958 unakuta kwny faili kaweka 1965 au 1961
 
Rekodi nyingi za awali zinasema Musuguri alizaliwa 1920.
 
Wahariri wa TBC siwaelewi, wana access ya Mkuu wa Majeshi, Msemaji wa Jeshi, lakini bado wanakosea. Hata katika taarifa ya habari ya saa moja usiku wa leo, habari inahusu Mkoa wa Mwanza, caption imeandikwa Kigoma.
Nikiulizwa nimwamini nani kati ya TBC na TPDF, bila kusita nitawaamini TBC kwa sababu TPDF wanatumia rekodi za kazi ambazo kwa miaka ya zamani watu wengi taarifa za umri wao hazikuwa sahihi!! Na ukiangalia rekodi nyingi online zinaonesha alizaliwa 1920; kwahiyo inawezekana yeye mwenyewe aliwahi kufanya mahojiano hapo zamani, hususani baada ya kustaafu na alipoulizwa alizaliwa mwaka gani, akataja hiyo 1920 na ikawa ndo public knowledge huku JWTZ wakibaki na official work records. Na kwa upande mwingine, sitashangaa nikisikia miaka yote hiyo ni ya kubahatisha tu!
 
Unaona bora uamini mambo ya kufikirika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…