TBT: Unakumbuka nini kuhusu mabomu ya Mbagala (2009) na Gongo la Mboto (2011)?

TBT: Unakumbuka nini kuhusu mabomu ya Mbagala (2009) na Gongo la Mboto (2011)?

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
673
Reaction score
1,318
Kwa wale ambao wamekuwa wakifuatilia matukio muhimu ya kiusalama nchini, milipuko ya mabomu katika maghala ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huko Mbagala mwaka 2009 na Gongo la Mboto mwaka 2011 ni miongoni mwa matukio yaliyoshtua taifa zima.
IMG_8048.jpeg

Tukio la kwanza la Mbagala lilitokea Aprili 29, 2009, na miaka miwili baadaye, Februari 16, 2011, milipuko mingine ilitikisa Gongo la Mboto, na kusababisha vifo, majeruhi, na uharibifu mkubwa wa mali.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, chanzo cha milipuko yote miwili kilihusisha hali duni ya hifadhi ya mabomu na vifaa vya kijeshi. Ghala zilizohifadhi mabomu hayo zilikuwa na changamoto za miundombinu, ikiwemo uchakavu wa silaha zilizohifadhiwa.
IMG_8051.jpeg

Hii ilisababisha ajali ya kwanza Mbagala, na kisha Gongo la Mboto, ambako hali kama hiyo ilijirudia. Mabomu yalilipuka na kusambaa kwa umbali mkubwa, yakiharibu miundombinu ya kijamii kama nyumba, shule, na hospitali.

Matukio haya yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 50 kwa ujumla, na kujeruhi mamia ya raia. Wengi walipoteza makazi yao huku maelfu ya nyumba zikiharibika. Kwa mfano, baada ya milipuko ya Mbagala, zaidi ya watu 7,000 walihitaji msaada wa haraka wa makazi. Vifo na uharibifu wa mali vilileta huzuni na taharuki, huku jamii ikibaki na maswali mengi kuhusu usalama wa maghala ya silaha yaliyokaribu na makazi ya watu.
IMG_8047.jpeg

Serikali ilichukua hatua za haraka kutoa msaada kwa waathirika, huku Rais wa wakati huo, Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na aliyekua waziri wa Ulinzi wa kipindi hiko Mh. Dr. Hussain Mwinyi, wakitembelea maeneo ya matukio yote mawili.​


Rais Kikwete aliahidi uchunguzi na fidia kwa waathirika. Hata hivyo, mijadala ilizuka kuhusu iwapo hatua zilizochukuliwa na serikali zilikuwa za kutosha au kama matatizo ya msingi ya usalama wa hifadhi ya silaha yalishughulikiwa kikamilifu.
IMG_8053.jpeg

Mbali na vifo na majeruhi, madhara ya kiuchumi yalikuwa makubwa. Serikali ililazimika kutumia rasilimali nyingi kutoa misaada kwa waathirika, wakati raia wengi waliopoteza mali zao walibaki na mzigo wa kurejesha maisha yao. Biashara, makazi, na miundombinu mingine iliyoathiriwa vilihitaji kurekebishwa upya, na baadhi ya maeneo yaliathirika kwa muda mrefu.
IMG_8050.jpeg

Katika tukio la gongo la mboto, aliyekua meya wa Ilala kwa kipindi hicho Mh. Jerry Silla alitoa report iliyoainisha idadi ya majeruhu na vifo, japo report hiyo ilipingwa sana kwa kipindi hiko huku wananchi wakiwa wanahofia kuwa idadi ya watu iliyotajwa ni ndogo kuliko uhalisia


Matukio haya yalifungua mjadala mzito kuhusu usalama wa raia wanaoishi karibu na maghala ya silaha. Wananchi walitilia shaka uwezo wa JWTZ na vyombo vingine vya serikali kudhibiti silaha kwa viwango vinavyohakikisha usalama wa raia. Maswali yalizuka kuhusu kwa nini mabomu haya yaliachwa kuhifadhiwa katika hali duni na ni kwa namna gani serikali inaweza kuhakikisha kwamba milipuko kama hiyo haitatokea tena.

Miaka kadhaa baada ya matukio haya, tunapaswa kujiuliza, je, tumejifunza vya kutosha ili kuzuia ajali kama hizi kutokea tena? Serikali iliahidi kuboresha viwango vya usalama wa maghala ya silaha, lakini bado kuna mijadala kuhusu kama hatua za kutosha zimechukuliwa.

Kwa kuwa matukio haya yanaacha alama kubwa katika historia ya Tanzania, na ikiwa leo ni alhamisi ya TBT, em tuambie unakumbuka nini kuhusu matukio haya?🤷🏽‍♂️​


View: https://youtu.be/tEmOeOKWcEI?si=B2xOxjCrBjG9HQE2

PIA SOMA:
  1. Thread 'Tukumbushane yaliyojiri mlipuko wa mabomu ya Gongo la Mboto'
  2. Thread 'Milipuko ya mabomu Mbagala ni makosa gani ya na kibinadamu na ya kiufundi yalisababisha kutokea kwa ajali hizi'
  3. Thread 'Bungeni: Milipuko ya mabomu Mbagala yatafuna Tsh. Bilioni 17.4'
 

Attachments

  • IMG_8046.jpeg
    IMG_8046.jpeg
    25 KB · Views: 8
  • IMG_8051.jpeg
    IMG_8051.jpeg
    82.4 KB · Views: 13
Mbagala,
Nakumbuka ilikuwa kama kwenye majira ya mchana saa 6/7 nikiwa maeneo ya Kwa Azizi Ali daladala zilizokuwa zinakwenda Mbagala zilikuwa zinageuza na kurudi maeneo zilikotoka na nyingine zilikuwa zinashusha abiria hapo hapo. Ndipo tulipowauliza madereva/makonda ambao ni marafiki zetu walitujulisha kuwa kuna milipuko imesikika hivyo zimamoto na Kikosi cha Polisi wanaelekea huko. Baada ya muda ndio watu wengi walionekana wakitokea huko kwa kukimbia, na baada ya muda kuna kipande kimoja cha bomu kikaangukia maeneo ya Uhasibu.

Gongolamboto
Ilikuwa ni majira ya saa 1/2 Usiku nikiwa maeneo ya Buza, kuna manzi nilikwenda kuicheki, hii ndio milipuko ilisikika kabisa...pamoja na kuonekana mwanga angani. Nikaagana na yule manzi na kusepa.
 
Ninachokumbuka tu ni dada mmoja akiwa na underwear pekee alikutwa msimbazi center anashindwa hata kueleza amefikaje hapo katika hali hiyo.

Basi baada ya kutulia na wasamaria kumsitiri ndio akaanza kutiririka anasema ilikuwa majira ya saa tatu kasoro usiku alikuwa ametoka bafuni kuoga akiwa na amejifunga kanga na kuingia ndani ile amevaa underwear akasikia mlipuko, ikabidi atoke na kanga yake ila hakukumbuka kurudi tena ndani kwa yaliyotokea,
 
Mbagala,
Nakumbuka ilikuwa kama kwenye majira ya mchana saa 6/7 nikiwa maeneo ya Kwa Azizi Ali daladala zilizokuwa zinakwenda Mbagala zilikuwa zinageuza na kurudi maeneo zilikotoka na nyingine zilikuwa zinashusha abiria hapo hapo. Ndipo tulipowauliza madereva/makonda ambao ni marafiki zetu walitujulisha kuwa kuna milipuko imesikika hivyo zimamoto na Kikosi cha Polisi wanaelekea huko. Baada ya muda ndio watu wengi walionekana wakitokea huko kwa kukimbia, na baada yamuda kuna kipande kimoja cha bomu kikaangukia maeneo ya Uhasibu.

Gongolamboto
Ilikuwa ni majira ya saa 1/2 Usiku nikiwa maeneo ya Buza, kuna manzi nilikwenda kuicheki, hii ndio milipuko ilisikika kabisa...pamoja na kuonekana mwanga angani. Nikaagana na yule manzi na kusepa.
katika hizi case zote mbili hukuwawahi kuhusi kama ni vita au ulikuwa unafikiria nini hasahasa hii ya pili iliyotokea usiku?
 
katika hizi case zote mbili hukuwawahi kuhusi kama ni vita au ulikuwa unafikiria nini hasahasa hii ya pili iliyotokea usiku?
Watanzania hatuko makini na hivyo vyote ulivyotaja, binafsi sikuwahi hata kuwazia vita, ile ya Mbagala yenyewe mpaka nilipoona magari ya Polisi yanaelekea huko. Hii ya Gongolamboto wengi tulikuwa tunadhani ni Diwali ile ya Wahindi, lakini nilijiuliza sana lakini mbona Diwali fataki huwa maeneo ya Posta Posta!!
 
Back
Top Bottom