Same here...hamu sina...mabomu ya gongo la mboto 😀 😀 😀 sitasahau
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Same here...hamu sina...mabomu ya gongo la mboto 😀 😀 😀 sitasahau
Tupe story kidogo aisee😁Same here...hamu sina...
nakuja unihadithie pm nisome ulivyokikimbiza kinaniliu...🤣nyokooo unipigie nikuadithie
Mpaka leo najiuliza wanaokimbia marathon mapafu yao yakoje? Niliongozana na baba aliyekuwa na kichanga cha approx chini ya miezi 3, hakijafunikwa chochote. Ikabidi nimpatie kanga niliyokuwa nayo amfunike. Namuuliza mamake yuko wapi, kosa, ndio kaanza kilio mke wangu..mke wangu...Ama, nikajiongezea mbio kunusuru ya kwangu...Tupe story kidogo aisee😁
poleni sana!Mpaka leo najiuliza wanaokimbia marathon mapafu yao yakoje? Niliongozana na baba aliyekuwa na kichanga cha approx chini ya miezi 3, hakijafunikwa chochote. Ikabidi nimpatie kanga niliyokuwa nayo amfunike. Namuuliza mamake yuko wapi, kosa, ndio kaanza kilio mke wangu..mke wangu...Ama, nikajiongezea mbio kunusuru ya kwangu...
Ukahisi Diwali gani ipo Gongolamboto, hukujiuliza Wahindi gani waishi uko.Watanzania hatuko makini na hivyo vyote ulivyotaja, binafsi sikuwahi hata kuwazia vita, ile ya Mbagala yenyewe mpaka nilipoona magari ya Polisi yanaelekea huko. Hii ya Gongolamboto wengi tulikuwa tunadhani ni Diwali ile ya Wahindi, lakini nilijiuliza sana lakini mbona Diwali fataki huwa maeneo ya Posta Posta!!
Jeshi lolote lile duniani mlipuko kwenye ghala la silaha unaweza tokea.Hii ilionesha ni namna Gani hili jeshi la wavunja matofali lilivyo na uwezo mdogo kijeshi.Yaani silaha tu kuzihifadhi vizuri limeshindwa Hadi imepelekea milipuko kutokana na uchakavu na mazingira mabovu?.Kama kutunza tu limeshindwa je wanauwezo kweli wa kuenda na wakati kama majeshi mengine kama jeshi la Rwanda.
Kwa wale ambao wamekuwa wakifuatilia matukio muhimu ya kiusalama nchini, milipuko ya mabomu katika maghala ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huko Mbagala mwaka 2009 na Gongo la Mboto mwaka 2011 ni miongoni mwa matukio yaliyoshtua taifa zima.
Tukio la kwanza la Mbagala lilitokea Aprili 29, 2009, na miaka miwili baadaye, Februari 16, 2011, milipuko mingine ilitikisa Gongo la Mboto, na kusababisha vifo, majeruhi, na uharibifu mkubwa wa mali.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, chanzo cha milipuko yote miwili kilihusisha hali duni ya hifadhi ya mabomu na vifaa vya kijeshi. Ghala zilizohifadhi mabomu hayo zilikuwa na changamoto za miundombinu, ikiwemo uchakavu wa silaha zilizohifadhiwa.
Hii ilisababisha ajali ya kwanza Mbagala, na kisha Gongo la Mboto, ambako hali kama hiyo ilijirudia. Mabomu yalilipuka na kusambaa kwa umbali mkubwa, yakiharibu miundombinu ya kijamii kama nyumba, shule, na hospitali.
Matukio haya yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 50 kwa ujumla, na kujeruhi mamia ya raia. Wengi walipoteza makazi yao huku maelfu ya nyumba zikiharibika. Kwa mfano, baada ya milipuko ya Mbagala, zaidi ya watu 7,000 walihitaji msaada wa haraka wa makazi. Vifo na uharibifu wa mali vilileta huzuni na taharuki, huku jamii ikibaki na maswali mengi kuhusu usalama wa maghala ya silaha yaliyokaribu na makazi ya watu.
Serikali ilichukua hatua za haraka kutoa msaada kwa waathirika, huku Rais wa wakati huo, Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na aliyekua waziri wa Ulinzi wa kipindi hiko Mh. Dr. Hussain Mwinyi, wakitembelea maeneo ya matukio yote mawili.
Rais Kikwete aliahidi uchunguzi na fidia kwa waathirika. Hata hivyo, mijadala ilizuka kuhusu iwapo hatua zilizochukuliwa na serikali zilikuwa za kutosha au kama matatizo ya msingi ya usalama wa hifadhi ya silaha yalishughulikiwa kikamilifu.
Mbali na vifo na majeruhi, madhara ya kiuchumi yalikuwa makubwa. Serikali ililazimika kutumia rasilimali nyingi kutoa misaada kwa waathirika, wakati raia wengi waliopoteza mali zao walibaki na mzigo wa kurejesha maisha yao. Biashara, makazi, na miundombinu mingine iliyoathiriwa vilihitaji kurekebishwa upya, na baadhi ya maeneo yaliathirika kwa muda mrefu.
Katika tukio la gongo la mboto, aliyekua meya wa Ilala kwa kipindi hicho Mh. Jerry Silla alitoa report iliyoainisha idadi ya majeruhu na vifo, japo report hiyo ilipingwa sana kwa kipindi hiko huku wananchi wakiwa wanahofia kuwa idadi ya watu iliyotajwa ni ndogo kuliko uhalisia
Matukio haya yalifungua mjadala mzito kuhusu usalama wa raia wanaoishi karibu na maghala ya silaha. Wananchi walitilia shaka uwezo wa JWTZ na vyombo vingine vya serikali kudhibiti silaha kwa viwango vinavyohakikisha usalama wa raia. Maswali yalizuka kuhusu kwa nini mabomu haya yaliachwa kuhifadhiwa katika hali duni na ni kwa namna gani serikali inaweza kuhakikisha kwamba milipuko kama hiyo haitatokea tena.
Miaka kadhaa baada ya matukio haya, tunapaswa kujiuliza, je, tumejifunza vya kutosha ili kuzuia ajali kama hizi kutokea tena? Serikali iliahidi kuboresha viwango vya usalama wa maghala ya silaha, lakini bado kuna mijadala kuhusu kama hatua za kutosha zimechukuliwa.
Kwa kuwa matukio haya yanaacha alama kubwa katika historia ya Tanzania, na ikiwa leo ni alhamisi ya TBT, em tuambie unakumbuka nini kuhusu matukio haya?🤷🏽♂️
View: https://youtu.be/tEmOeOKWcEI?si=B2xOxjCrBjG9HQE2
PIA SOMA:
Tupe maelezo huu ulikuwaje mkuuMlipo wa mwanzo ulikuwa mwaka 2003 au 2004 kama sikosei hapo Gongo la Mboto…Inaonekana tukio hili wengi hawalikumbuki sana.
True..hii kitu vita kilinifikirisha sana kipindi kile, sisi yalikuwa ya bahati mbaya. Imagine nchi ambazo hiyo milio ni 24/7!..Itoshe kusema uliyasikia kwa mbali hali ilikuwa hivyo, je watumiaji wakiwa field inakuwaje!! Vita mbaya sana tuendelee kudumisha amani yetu!!
Ilikuwa mida ya saa saba kwenda Saa nane mchana nakumbuka tulikuwa darasani kipindi cha Physics mwalimu akiwa mzee mmoja anaitwa Nzohi.Tupe maelezo huu ulikuwaje mkuu
Sasa mkuu si ungeyarudisha kambi iNilidaka kwa mikono yangu mabomu zaidi ya 12
Kumuita afande AFWANDE ni matusi hayo...... si raia wala afwande, wote tulitoka nduki!
😅
... usini'misquote' ndugu!, ... juzijuzi tu nilikuwa Kawe!Kumuita afande AFWANDE ni matusi hayo...
😂😂😂😂😂