TBT: Unakumbuka nini kuhusu mabomu ya Mbagala (2009) na Gongo la Mboto (2011)?

TBT: Unakumbuka nini kuhusu mabomu ya Mbagala (2009) na Gongo la Mboto (2011)?

Hii ilionesha ni namna Gani hili jeshi la wavunja matofali lilivyo na uwezo mdogo kijeshi.Yaani silaha tu kuzihifadhi vizuri limeshindwa Hadi imepelekea milipuko kutokana na uchakavu na mazingira mabovu?.Kama kutunza tu limeshindwa je wanauwezo kweli wa kuenda na wakati kama majeshi mengine kama jeshi la Rwanda?.
 
Hii ilionesha ni namna Gani hili jeshi la wavunja matofali lilivyo na uwezo mdogo kijeshi.Yaani silaha tu kuzihifadhi vizuri limeshindwa Hadi imepelekea milipuko kutokana na uchakavu na mazingira mabovu?.Kama kutunza tu limeshindwa je wanauwezo kweli wa kuenda na wakati kama majeshi mengine kama jeshi la Rwanda.
Unaongea kama vile wanahifadhi embe kwenye friji au kama vile mabomu yanaongea!!
 
Waziri wa Ulinzi hakuhojiwa na Polisi.
Nakumbuka pia Rais Ali Hassan Mwinyi alikuwa anasema," Nchi yetu safi kabisa. Siyo kama jirani zetu. Hapa hatuzalishi wakimbizi. Hapa tunapokea wakimbizi."
Kesho yake yale mabomu yakalipuka na wakimbizi wengi walikwenda Stadium.
Halafu nasikia watoto wengi walipotea.
Af,nakumbuka nilikuwa nimefunga kula chakula for two weeks non-stop .
Niko Mikocheni naisikiliza Ile milipuko inadunda kwenye moyo wangu.
Nikashukuru siko karibu kule.
Halafu ilikuwepo tafrifa kwenye garden ya Ikulu
Nilikuwa na - chat na yule Kamanda wa Jeshi anaitwa Mbowe, alikuwa Jeshini amekamatwa finances za Jeshi.
Nikamuuliza unamfahamu Freeman.
Akasema ni,sijui alisemaje,yule Freeman ni mdogo wangu au kama mtoto wangu.
Basi kesho yake asubuhi,for some reason, Kikwete akamchagua yule kuiongoza tume ya kupelekeza lile tukio.
 
Mabomu ya Gongolamboto.

Nipo nyumbani natazama tv, sasa majira kama ya saa moja nikaanza kusikia miungurumo kama, basi kwakuwa tikuwa sana na shida ya maji haya kutoka zaidi ya siku 4.

Nilitoka nje nikiwa na mabeseni kwa ajiri ya kukinga maji, hivyo nikayayegesha kama kawaida, ila kilichonishangaza kila nikipiga jicho angani sioni dalili za mvua ingawaje miungurumo imepamba moto.

Ndipo nilipo rudi ndani kukutana na maandishi chini ya tv, yakielezea milipuko inayo endelea kulindima huko Gongolamboto.

babu wa maraha.
 
Waziri wa Ulinzi hakuhojiwa na Polisi.
Nakumbuka pia Rais Ali Hassan Mwinyi alikuwa anasema," Nchi yetu safi kabisa. Siyo kama jirani zetu. Hapa hatuzalishi wakimbizi. Hapa tunapokea wakimbizi."
Kesho yake yale mabomu yakalipuka na wakimbizi wengi walikwenda Stadium.
Halafu nasikia watoto wengi walipotea.
Nchi yetu ni kweli kabisa hatuzalishi wakimbizi. Kuna tofauti kubwa kati ya wakimbizi na watu walioondoka kwenye makazi yao au kuelekea kuishi sehemu nyingine. Mtu ambaye hajavuka mpaka wa Kimataifa sio mkimbizi. Sasa hawa wa Mbagala na Gongolamboto walivuka mpaka gani wa Kimataifa??1
 
Nilijua Kagame ndio katuvamia Sasa Mkwere na Makamanda wake wanauona Moto kumbe.

Nilikuwa shule Asee niliwasomba watu kwa stori za Nini kinaendelea kuja kugeuka Hilo mobb lilivyonizunguka kuskiza Counter Intel wa Domitory namba 3 nikimwaga fiction.
Hakika watanikumbuka Zaid ya hayo mabomu yenyewe.
#CHAI.
 
Kwa wale ambao wamekuwa wakifuatilia matukio muhimu ya kiusalama nchini, milipuko ya mabomu katika maghala ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huko Mbagala mwaka 2009 na Gongo la Mboto mwaka 2011 ni miongoni mwa matukio yaliyoshtua taifa zima.

Tukio la kwanza la Mbagala lilitokea Aprili 29, 2009, na miaka miwili baadaye, Februari 16, 2011, milipuko mingine ilitikisa Gongo la Mboto, na kusababisha vifo, majeruhi, na uharibifu mkubwa wa mali.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, chanzo cha milipuko yote miwili kilihusisha hali duni ya hifadhi ya mabomu na vifaa vya kijeshi. Ghala zilizohifadhi mabomu hayo zilikuwa na changamoto za miundombinu, ikiwemo uchakavu wa silaha zilizohifadhiwa.

Hii ilisababisha ajali ya kwanza Mbagala, na kisha Gongo la Mboto, ambako hali kama hiyo ilijirudia. Mabomu yalilipuka na kusambaa kwa umbali mkubwa, yakiharibu miundombinu ya kijamii kama nyumba, shule, na hospitali.

Matukio haya yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 50 kwa ujumla, na kujeruhi mamia ya raia. Wengi walipoteza makazi yao huku maelfu ya nyumba zikiharibika. Kwa mfano, baada ya milipuko ya Mbagala, zaidi ya watu 7,000 walihitaji msaada wa haraka wa makazi. Vifo na uharibifu wa mali vilileta huzuni na taharuki, huku jamii ikibaki na maswali mengi kuhusu usalama wa maghala ya silaha yaliyokaribu na makazi ya watu.

Serikali ilichukua hatua za haraka kutoa msaada kwa waathirika, huku Rais wa wakati huo, Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na aliyekua waziri wa Ulinzi wa kipindi hiko Mh. Dr. Hussain Mwinyi, wakitembelea maeneo ya matukio yote mawili.​


Rais Kikwete aliahidi uchunguzi na fidia kwa waathirika. Hata hivyo, mijadala ilizuka kuhusu iwapo hatua zilizochukuliwa na serikali zilikuwa za kutosha au kama matatizo ya msingi ya usalama wa hifadhi ya silaha yalishughulikiwa kikamilifu.

Mbali na vifo na majeruhi, madhara ya kiuchumi yalikuwa makubwa. Serikali ililazimika kutumia rasilimali nyingi kutoa misaada kwa waathirika, wakati raia wengi waliopoteza mali zao walibaki na mzigo wa kurejesha maisha yao. Biashara, makazi, na miundombinu mingine iliyoathiriwa vilihitaji kurekebishwa upya, na baadhi ya maeneo yaliathirika kwa muda mrefu.

Katika tukio la gongo la mboto, aliyekua meya wa Ilala kwa kipindi hicho Mh. Jerry Silla alitoa report iliyoainisha idadi ya majeruhu na vifo, japo report hiyo ilipingwa sana kwa kipindi hiko huku wananchi wakiwa wanahofia kuwa idadi ya watu iliyotajwa ni ndogo kuliko uhalisia


Matukio haya yalifungua mjadala mzito kuhusu usalama wa raia wanaoishi karibu na maghala ya silaha. Wananchi walitilia shaka uwezo wa JWTZ na vyombo vingine vya serikali kudhibiti silaha kwa viwango vinavyohakikisha usalama wa raia. Maswali yalizuka kuhusu kwa nini mabomu haya yaliachwa kuhifadhiwa katika hali duni na ni kwa namna gani serikali inaweza kuhakikisha kwamba milipuko kama hiyo haitatokea tena.

Miaka kadhaa baada ya matukio haya, tunapaswa kujiuliza, je, tumejifunza vya kutosha ili kuzuia ajali kama hizi kutokea tena? Serikali iliahidi kuboresha viwango vya usalama wa maghala ya silaha, lakini bado kuna mijadala kuhusu kama hatua za kutosha zimechukuliwa.

Kwa kuwa matukio haya yanaacha alama kubwa katika historia ya Tanzania, na ikiwa leo ni alhamisi ya TBT, em tuambie unakumbuka nini kuhusu matukio haya?🤷🏽‍♂️​


View: https://youtu.be/tEmOeOKWcEI?si=B2xOxjCrBjG9HQE2

PIA SOMA:
  1. Thread 'Tukumbushane yaliyojiri mlipuko wa mabomu ya Gongo la Mboto'
  2. Thread 'Milipuko ya mabomu Mbagala ni makosa gani ya na kibinadamu na ya kiufundi yalisababisha kutokea kwa ajali hizi'
  3. Thread 'Bungeni: Milipuko ya mabomu Mbagala yatafuna Tsh. Bilioni 17.4'

Mlipo wa mwanzo ulikuwa mwaka 2003 au 2004 kama sikosei hapo Gongo la Mboto…Inaonekana tukio hili wengi hawalikumbuki sana.
 
Mbagala,
Nakumbuka ilikuwa kama kwenye majira ya mchana saa 6/7 nikiwa maeneo ya Kwa Azizi Ali daladala zilizokuwa zinakwenda Mbagala zilikuwa zinageuza na kurudi maeneo zilikotoka na nyingine zilikuwa zinashusha abiria hapo hapo. Ndipo tulipowauliza madereva/makonda ambao ni marafiki zetu walitujulisha kuwa kuna milipuko imesikika hivyo zimamoto na Kikosi cha Polisi wanaelekea huko. Baada ya muda ndio watu wengi walionekana wakitokea huko kwa kukimbia, na baada yamuda kuna kipande kimoja cha bomu kikaangukia maeneo ya Uhasibu.

Gongolamboto
Ilikuwa ni majira ya saa 1/2 Usiku nikiwa maeneo ya Buza, kuna manzi nilikwenda kuicheki, hii ndio milipuko ilisikika kabisa...pamoja na kuonekana mwanga angani. Nikaagana na yule manzi na kusepa.
😂😂 yani ww matukio yote mawili ulikuwemo, unatakiwa kuwa steringi wa hii movie aisee😂😂​
 
Back
Top Bottom