Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Katika kuadhimisha Siku ya Usafiri wa Anga Duniani (ICAD) ambayo kilele chake ni Desemba 7, 2024 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Salim Msangi amesema kwa sasa hakuna ndege ambayo inaweza kuingia kwenye anga la Tanzania bila kuonekana.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Desemba 7, 2025 Jijini Dar es Salaam, Msangi amesema kwamba rada nne zimesimikwa mpaka sasa ambazo zinafanya anga lote la Tanzania kuonekana, ambapo amesema kuwa kwa uwezo wa rada zilizopo sasa zina uwezo hadi kuhudumia maeneo mengine ya Nchi jirani.
"Serikali kwa kushirikiana na TCAA kama mnavyofahamu imeweza kununua na kusimika rada nne nchini nzima ambapo sasa hivi tunaweza kuona anga letu lote la Nchi yetu, hakuna ndege yoyote inaweza kuingia nchini bila kuonekana," amesema Mkurugenzi.
Amesema kwamba kabla ya usimikwaji wa rada mpya walikuwa na uwezo wa kuliangalia anga la Tanzania kwa asilimia 25 pekee. Amesema hali ya sasa ya kuliona anga zima inaiweka Tanzania katika hali nzuri kiusalama kupitia Sekta ya Anga.
Aidha, katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo amesema kuwa kupitia mfuko wa 'TCAA Training Fund' ambao ulianzishwa kwa lengo la kufadhili mafunzo ya urubani na uhandisi wa ndege, umewezesha kusomesha marubani wanane ambao wamehitimu pamoja na Mhandisi mmoja ambaye amepata mafunzo katika Chuo cha Ethiopia Academy ambaye tayari naye amehitimu huku pia wengine 10 tayari nao wapo nchini Ethiopia wakiendelea na mafunzo kupitia ufadhili wa mfuko huo.
Amesema kuwa sekta ya anga inaendelea kukua, hivyo inahitajika uwepo wataalamu wa kutosha ikiwemo marubani na wahandisi (fundi ndege) ili kuendana na kasi iliyopo.
Ambapo amesema kwamba mpaka sasa kuna mashirika ya ndege 46 ambayo yamesajiliwa huku mashirika ya nje yakiwa ni 23 na mengine manne yapo katika hatua za mwisho kukamilisha taratibu za kupewa usajili.
Ameongeza kwamba licha ya sekta ya anga kuyumba kipindi cha COVID-19, lakini hali ya ukuaji imeanza kurejea kwa kasi, ambapo amesema kuwa kwa mwaka 2023 abiria milioni 6.8 walihudumiwa na viwanja vya ndege vilivyopo nchini. Matarajio yaliyopo ambayo ameyaeleza ni ongezeko kwa mwaka 2024 hadi kufikia watu milioni 7.8.
Katika kipindi cha Mwaka 2020 amesema kuwa kulikuwepo na anguko lililotokana na COVID-19 ambapo kiwango cha Watu waliotumia usafiri wa ndege ni Milioni 2.8 ikiwa ni anguko la asilimia 50 kutoka katika kiwango cha awali kabla ya janga hilo kuripotiwa.
Hili kuendelea kuiweka katika mazingira endelevu sekta ya anga, amesema kwamba jitihada mbalimbali zinaendelea kuifanya sekta hiyo kuwa bora zaidi kwa kuwahudumia wananchi wengi ikiwemo kuongeza ushindani ambao utapelekea bei za usafiri kushuka.
Hata hivyo imeelezwa mpaka taarifa hiyo inatolewa nchini kuna jumla ya marubani 603 ambao wanatambuliwa na mamlaka hiyo, kati ya hao wazawa ni 344 na wageni 259, ambapo kuna uhitaji wa marubani takribani 160 ili kuendana na ukuaji wa sekta hiyo.
"Serikali kwa kushirikiana na TCAA kama mnavyofahamu imeweza kununua na kusimika rada nne nchini nzima ambapo sasa hivi tunaweza kuona anga letu lote la Nchi yetu, hakuna ndege yoyote inaweza kuingia nchini bila kuonekana," amesema Mkurugenzi.
Aidha, katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo amesema kuwa kupitia mfuko wa 'TCAA Training Fund' ambao ulianzishwa kwa lengo la kufadhili mafunzo ya urubani na uhandisi wa ndege, umewezesha kusomesha marubani wanane ambao wamehitimu pamoja na Mhandisi mmoja ambaye amepata mafunzo katika Chuo cha Ethiopia Academy ambaye tayari naye amehitimu huku pia wengine 10 tayari nao wapo nchini Ethiopia wakiendelea na mafunzo kupitia ufadhili wa mfuko huo.
Amesema kuwa sekta ya anga inaendelea kukua, hivyo inahitajika uwepo wataalamu wa kutosha ikiwemo marubani na wahandisi (fundi ndege) ili kuendana na kasi iliyopo.
Ambapo amesema kwamba mpaka sasa kuna mashirika ya ndege 46 ambayo yamesajiliwa huku mashirika ya nje yakiwa ni 23 na mengine manne yapo katika hatua za mwisho kukamilisha taratibu za kupewa usajili.
Ameongeza kwamba licha ya sekta ya anga kuyumba kipindi cha COVID-19, lakini hali ya ukuaji imeanza kurejea kwa kasi, ambapo amesema kuwa kwa mwaka 2023 abiria milioni 6.8 walihudumiwa na viwanja vya ndege vilivyopo nchini. Matarajio yaliyopo ambayo ameyaeleza ni ongezeko kwa mwaka 2024 hadi kufikia watu milioni 7.8.
Katika kipindi cha Mwaka 2020 amesema kuwa kulikuwepo na anguko lililotokana na COVID-19 ambapo kiwango cha Watu waliotumia usafiri wa ndege ni Milioni 2.8 ikiwa ni anguko la asilimia 50 kutoka katika kiwango cha awali kabla ya janga hilo kuripotiwa.
Hata hivyo imeelezwa mpaka taarifa hiyo inatolewa nchini kuna jumla ya marubani 603 ambao wanatambuliwa na mamlaka hiyo, kati ya hao wazawa ni 344 na wageni 259, ambapo kuna uhitaji wa marubani takribani 160 ili kuendana na ukuaji wa sekta hiyo.