TCRA, acheni kujitetea kuhusu mikopo ya mtandaoni; je, hamna uwezo wa kuagiza makampuni ya simu kutosajili lipa namba wanazotumia kupokea marejesho?

TCRA, acheni kujitetea kuhusu mikopo ya mtandaoni; je, hamna uwezo wa kuagiza makampuni ya simu kutosajili lipa namba wanazotumia kupokea marejesho?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Watanzania, tufike mahali tujiulize swali hli dogo tu:

Mikopo ya mitandaoni hutolewa kwa wateja kutumiwa hela kwenye simu zao na zaidi marejesho hutumwa kwa haya makampuni kwa kutumia lipa namba za mitandao ya simu. Sasa kama mpaka wanakuwa wamesajili lipa namba kwenye menu ya mitandao ya simu, TCRA wanashindwa nini kuagiza makampuni ya simu kusitisha maramoja usajili wa lipa namba za haya makampuni kama kweli wana dhamira ya dhati ya kudhibiti hii biashara inayofanywa kihuni na baadhi ya makampuni?

Mpaka kusajili namba ya kufanyia malipo maarufu kama "namba ya kampuni" , ni lazima utatakiwa kuwa na viambatanisho maalumu, na kama sikosei, utatakiwa kuwa na leseni ya biashara, leseni ya BOT, cheti kutoka BRELA, n.k pamoja na kutoa taarifa zingine kama anuani ya makazi, n.k.

Kwa mtazamo wangu, TCRA, kama regulator, kwa kushirikiana na BOT na makampuni ya simu, wangeweza kabisa kudhibiti wanaofanya hii biashara ya kukopesha mitandaoni bila kufuata taratibu, ila nachokiona hiyo dhamira haipo na ndio maana hii biashara haramu inazidi tu kushamiri humu nchini.

Je, tukisema kwasababu serikali inapata kodi na makampuni ya simu nayo yanapata faida kwa kila transaction inayofanyika na ndio maana hatua hazichukuliwa, tutakuwa tunakosea?

Nato wito kwa waandishi wa habari na hata wabunge wahoji maswali specific kama haya kwa TRCA, BOT na makampuni ya simu kwasababu haiwezekani watu wafanye biashara haramu kwa kutumia mitandao ya simu inayosimamiwa na kudhibitiwa na serikali halafu serikali ikashindwa kuwabaini hawa watu. Haingii akilini hata kidogo.

TCRA, kama sheria na kanuni zinawabana katika kudhibiti haya makampuni, kwanini hamchukui hatua za kubadili sheria na kanuzi au kuomba kutungwa kwa sheria/kanuni mpya zitazowawezesha kukabiliana na haya mapungufu kama wanavyofanya BOT kwa kutoa miongozi mipya kila wakati?

Tuache kudanganyana kabisa kuhusu haya mambo.

 
Mkuu TCRA wanatoa leseni kwa kuangalia vigezo na masharti ,kuwa na kampuni ya kukopesha bidhaa siyo kosa kisheria,kuna kampuni zinatoa mikopo ya pikipiki,bajaji,simu etc ukitaka kurejesha unarejesha kwa namba yao ya kampuni.....Kabla ya kukopa kuna masharti ya mkopo kama unakubaliana unakopa kama haukbaliani unaacha maana hawalazimishi.

Ni hivyo hivyo kwa Microfiance kuna zile hazipo online(Finca etc) na kuna zingine zipo online(TALA etc) ,zote zinafanya biashara....Na huko kote hawalazimishi kukopa....TCRA/BOT wataingia endapo tu wakopeshaji wamekiuka makubaliano ya makato....Kama awali haujakopa walikwambia wataka interest 20% halafu baadae wakakata 80% TCRA/BOT wana haki ya kuingilia na kabla haujakopa wanakupa mkeka kuanzia mwanzo wa makato hadi mwisho na unasaini na wanakwambia kila mwezi au wiki utarudisha amount hii kwa namba yao...

Kosa la hao jamaa naloliona ni kuchukua taarifa za watu wa phonebook na kuanzaia kuwapigia simu na kutangaza wanakudai hapo ndiyo shida na kabla ya kuinstall app yao wanakwambia kabisa kwamba wanachukua number kwenye simu yako na kama hautaki wachukue namba basi usi-install app yao.
 
Mkuu TCRA wanatoa leseni kwa kuangalia vigezo na masharti ,kuwa na kampuni ya kukopesha bidhaa siyo kosa kisheria,kuna kampuni zinatoa mikopo ya pikipiki,bajaji,simu etc ukitaka kurejesha unarejesha kwa namba yao ya kampuni.....Kabla ya kukopa kuna masharti ya mkopo kama unakubaliana unakopa kama haukbaliani unaacha maana hawalazimishi.

Ni hivyo hivyo kwa Microfiance kuna zile hazipo online(Finca etc) na kuna zingine zipo online(TALA etc) ,zote zinafanya biashara....Na huko kote hawalazimishi kukopa....TCRA wataingia endapo tu wakopeshaji wamekiuka makubaliano ya makato....Kama awali haujakopa walikwambia wataka interest 20% halafu baadae wakakata 80% TCRA wana haki ya kuingilia na kabla haujakopa wanakuoa mkeka kuanzia mwanzo wa makato hadi mwisho na unasaini na wanakwambia kila mwezi au wiki utarudisha amount hii kwa namba yao...

Kosa la hao jamaa naloliona ni kuchukua taarifa za watu wa phonebook na kuanzaia kuwapigia simu na kutangaza wanakudai hapo ndiyo shida na kabla ya kuinstall app yao wanakwambia kabisa kwamba wanachukua number kwenye simu yako na kama hautaki wachukue namba basi usi-install app yao.
Kama vigezo na mashariti haviangalii uhalali wa kisheria wa biashara inayofanywa na makampuni ya simu, basi hili ni tatizo lingine na ni wakati sasa wa kutazama upya hizi sheria na kanuni.
 
Kama vigezo na mashariti haviangalii uhalali wa kisheria wa biashara inayofanywa na makampuni ya simu, basi hili ni tatizo lingine na ni wakati sasa wa kutazama upya hizi sheria na kanuni.

Kampuni ya simu kabla hayajasajili Namba ya kampuni wanawaomba waprovide KYC ambazo documents hizo zote hutolewa na mamlaka husika wanakuwa nayo....Ukiona kampuni imepewa namba ya malipo means wamefuata taratibu na docs zote including leseni ya biashara,usajili etc
 
Kampuni ya simu kabla hayajasajili Namba ya kampuni wanawaomba waprovide KYC ambazo documents hizo zote hutolewa na mamlaka husika wanakuwa nayo....Ukiona kampuni imepewa namba ya malipo means wamefuata taratibu na docs zote including leseni ya biashara,usajili etc
Sasa inakuwaje wanashindwa kuwakamata kwa makosa ya kusambaza picha na taarifa za wateja wao mitandaoni walioshindwa kulipa madeni yao?
BOT wanadai mengi ya haya makampuni hayana leseni ya BOT. Sasa inakuwaje wanasajili lipa namba?
 
Watanzania, tufike mahali tujiulize swali hli dogo tu:

Mikopo ya mitandaoni hutolewa kwa wateja kutumiwa hela kwenye simu zao na zaidi marejesho hutumwa kwa haya makampuni kwa kutumia lipa namba za mitandao ya simu. Sasa kama mpaka wanakuwa wamesajili lipa namba kwenye menu ya mitandao ya simu, TCRA wanashindwa nini kuagiza makampuni ya simu kusitisha maramoja usajili wa lipa namba za haya makampuni kama kweli wana dhamira ya dhati ya kudhibiti hii biashara inayofanywa kihuni na baadhi ya makampuni?

Mpaka kusajili namba ya kufanyia malipo maarufu kama "namba ya kampuni" , ni lazima utatakiwa kuwa na viambatanisho maalumu, na kama sikosei, utatakiwa kuwa na leseni ya biashara, leseni ya BOT, cheti kutoka BRELA, n.k pamoja na kutoa taarifa zingine kama anuani ya makazi, n.k.

Kwa mtazamo wangu, TCRA, kama regulator, kwa kushirikiana na BOT na makampuni ya simu, wangeweza kabisa kudhibiti wanaofanya hii biashara ya kukopesha mitandaoni bila kufuata taratibu, ila nachokiona hiyo dhamira haipo na ndio maana hii biashara haramu inazidi tu kushamiri humu nchini.

Je, tukisema kwasababu serikali inapata kodi na makampuni ya simu nayo yanapata faida kwa kila transaction inayofanyika na ndio maana hatua hazichukuliwa, tutakuwa tunakosea?

Nato wito kwa waandishi wa habari na hata wabunge wahoji maswali specific kama haya kwa TRCA na makampuni ya simu kwasababu haiwezekani watu wafanye biashara haramu kwa kutumia mitandao ya simu inayosimamiwa na kudhibitiwa na serikali halafu serikali ikashindwa kuwabaini hawa watu. Haingii akilini hata kidogo.

Tuache kudanganyana kabisa kuhusu haya mambo.

TCRA kwa kukataa kuwajibika , huo ni udhaifu mkubwa.
Hivi katika kusimamia huu uchumi mchanga wa watanzania TCRA tupo pamoja lakini?
Wakiona hujuma inatookea wao watakunja mikono kifuani na kuondoka zao?
TCRA wakajipange.
 
Sasa inakuwaje wanashindwa kuwakamata kwa makosa ya kusambaza picha na taarifa za wateja wao mitandaoni walioshindwa kulipa madeni yao?
BOT wanadai mengi ya haya makampuni hayana leseni ya BOT. Sasa inakuwaje wanasajili lipa namba?

-Hapo kuna Uzembe umefanyika ,kusambaza picha na taarifa za mteja ni kosa kisheria kwanza la Cyber na pili la privacy act...wateja inabidi wa-initiate case kisa mamlaka husika zichukue hatua icluding polisi enforce law.
 
-Hapo kuna Uzembe umefanyika ,kusambaza picha na taarifa za mteja ni kosa kisheria kwanza la Cyber na pili la privacy act...wateja inabidi wa-initiate case kisa mamlaka husika zichukue hatua icluding polisi enforce law.
Kama sikosei, sheria inawruhusu kuingilia kati na kuchukua hatua bila kusubiri kupokea malalamiko rasimi kutoka kwa waathirka.

Hata Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binfsi(PDPC), nao wanaweza kuchukua hatua ila na wao wapo wapo tu.
 
Kama sikosei, sheria inawruhusu kuingilia kati na kuchukua hatua bila kusubiri kupokea malalamiko rasimi kutoka kwa waathirka.

Sure incase kama wakikutana nazo na mara nyingi huwa wakiulizwa wanasema hawajaziona ,hata speaker aliulizwa kuhusu utekaji akasema hajawahi kuona ,polisi kipindi cha lissu anasema anafatiliwa na gari wakasema hawafanyii kazi za mitandaoni ,so kuavoid hizo discrepancy nawashauri wateja wafungue case wenyewe.
 
Mkuu TCRA wanatoa leseni kwa kuangalia vigezo na masharti ,kuwa na kampuni ya kukopesha bidhaa siyo kosa kisheria,kuna kampuni zinatoa mikopo ya pikipiki,bajaji,simu etc ukitaka kurejesha unarejesha kwa namba yao ya kampuni.....Kabla ya kukopa kuna masharti ya mkopo kama unakubaliana unakopa kama haukbaliani unaacha maana hawalazimishi.

Ni hivyo hivyo kwa Microfiance kuna zile hazipo online(Finca etc) na kuna zingine zipo online(TALA etc) ,zote zinafanya biashara....Na huko kote hawalazimishi kukopa....TCRA/BOT wataingia endapo tu wakopeshaji wamekiuka makubaliano ya makato....Kama awali haujakopa walikwambia wataka interest 20% halafu baadae wakakata 80% TCRA/BOT wana haki ya kuingilia na kabla haujakopa wanakupa mkeka kuanzia mwanzo wa makato hadi mwisho na unasaini na wanakwambia kila mwezi au wiki utarudisha amount hii kwa namba yao...

Kosa la hao jamaa naloliona ni kuchukua taarifa za watu wa phonebook na kuanzaia kuwapigia simu na kutangaza wanakudai hapo ndiyo shida na kabla ya kuinstall app yao wanakwambia kabisa kwamba wanachukua number kwenye simu yako na kama hautaki wachukue namba basi usi-install app yao.
TCRA wamejiexpose kuwa ni vilaza.
Sasa Cyber Crimes wanawaachia polisi ambao si wajuzi sana kwenye shughuli za kimtandao?
Kutowajibika kwa TCRA kwenye hili ni kosa kubwa sana, maana wanao uwezo wa kutrack communications za aina zote nchini.
 
Mkuu TCRA wanatoa leseni kwa kuangalia vigezo na masharti ,kuwa na kampuni ya kukopesha bidhaa siyo kosa kisheria,kuna kampuni zinatoa mikopo ya pikipiki,bajaji,simu etc ukitaka kurejesha unarejesha kwa namba yao ya kampuni.....Kabla ya kukopa kuna masharti ya mkopo kama unakubaliana unakopa kama haukbaliani unaacha maana hawalazimishi.

Ni hivyo hivyo kwa Microfiance kuna zile hazipo online(Finca etc) na kuna zingine zipo online(TALA etc) ,zote zinafanya biashara....Na huko kote hawalazimishi kukopa....TCRA/BOT wataingia endapo tu wakopeshaji wamekiuka makubaliano ya makato....Kama awali haujakopa walikwambia wataka interest 20% halafu baadae wakakata 80% TCRA/BOT wana haki ya kuingilia na kabla haujakopa wanakupa mkeka kuanzia mwanzo wa makato hadi mwisho na unasaini na wanakwambia kila mwezi au wiki utarudisha amount hii kwa namba yao...

Kosa la hao jamaa naloliona ni kuchukua taarifa za watu wa phonebook na kuanzaia kuwapigia simu na kutangaza wanakudai hapo ndiyo shida na kabla ya kuinstall app yao wanakwambia kabisa kwamba wanachukua number kwenye simu yako na kama hautaki wachukue namba basi usi-install app yao.
Ni watanzania wachache wenye akili timami wataelewa hilo nchi imejaa wajinga watu wasioelewa mifumo na vitu wanavoongea sasa mtu anahisi serikali haitambui 😂 inatambua vizuri sana ila kuna kitu kinaitwa vigezo na masharti kuzingatiwa unasema ndio,, si kwamba unakopewa au unashikiwa mtutu,, ni sawa na dem kwenda geto kwa muhuni na kuuliza kwanini umenifanya hivi 😂 ndo hizi akili matapeli na wadaiwa sugu ndo wanalalamikia swala hilo wakitaka mserereko 😂
 
Sijawahi ona kama kuna jambo lolote ambalo limewahi kufanywa na mamlaka za serikali kwa ajili ya kuwalinda raia wake. Watu wapo kwa ajili ya kujinufaisha binafsi na si vinginevyo.
Shida hapo nni nn 😂 unataka wakupe bire au?
 
Sasa inakuwaje wanashindwa kuwakamata kwa makosa ya kusambaza picha na taarifa za wateja wao mitandaoni walioshindwa kulipa madeni yao?
BOT wanadai mengi ya haya makampuni hayana leseni ya BOT. Sasa inakuwaje wanasajili lipa namba?
Unahakika hawana leseni za BOT 😂 umefatilia list ya hayo makampuni yalio na leseni na yasiyo na leseni? Kwanini ukope kwa wasio na leseni na ulalamike, kwanini ukope na usirejeshe deni, kwenye biashara the more the risk the higher return wanarisk kutoa mikopo yao kwa watu wezi kama nyie kuliko mikopo ya kibank ambayo hata usipolipa wanabeba dhamana zako 😂 umeingia kule hujasoma vigezo na masharti umekubali haya yote yanaandikwa kule sasa umewatapeli kwanini wasikutafute picha zako unazani walichukua kwenda bandika ukutani kama mama? Watanzania akili zetu bado ndogo sana tunapenda mitelezo tutalainishwa 😂
 
Back
Top Bottom