KERO TCRA, hawa matapeli wa “TUMA KWA NAMBA HII” tutaishi nao milele?

KERO TCRA, hawa matapeli wa “TUMA KWA NAMBA HII” tutaishi nao milele?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kuna shida, piah Kwa baadhi ya wasajili lain Wana Tabia ya kujifanya mtandao unasumbus mara baada ya mteja kuweka fingerprint, na kumtaka mteja arudie Tena kuweka kidole, na hapo kusajili lain nyingne pasipo mteja kufaham kma namba yake ya NIDA imesajili zaidi ya namba Moja, piah linapaswa lidhibitiwe hili
 
Juzikati hapa nilienda kwa wakala wa airtel money kuweka kiasi fulani cha pesa katika simu yangu, baada ya kutoka tu kwa wakala sikukaa hata lisaa nikaanza kupigiwa simu na watu wanaodai ni wahudumu wa wateja Airtel, mbaya zaidi wakawa wananipigia kwa kutumia laini za mitandao mingine tofauti 😅. Hapa nachelea kusema kabisa kuna namna hawa watu wanashirikiana kujua nani ana pesa na nani hana, pia mara nyingi kwann laini za TTCL ndio zinatumika zaidi kutuma hizo sms? 🤔
 
Screenshot_2022-05-29-09-23-51-767_com.google.android.apps.messaging.jpg
Screenshot_2022-05-29-09-24-43-830_com.google.android.apps.messaging.jpg
Screenshot_2022-05-29-09-25-29-522_com.google.android.apps.messaging.jpg
Screenshot_2022-05-29-09-25-38-060_com.google.android.apps.messaging.jpg
Screenshot_2022-05-29-09-25-52-828_com.google.android.apps.messaging.jpg
Screenshot_2022-05-29-09-26-02-635_com.google.android.apps.messaging.jpg
 
Hii ni changamoto inayotusumbuwa kwa kiwango kikubwa sana, ukiwa una fanya miamala miamala ya simu mara kwa mara , au ukiwa unatunza pesa zako kwenye simu kwa hizi pesa pesa.

Ukiachana na hizi messages wanazotutumia kuna mda wanafanya hadi direct transfers kutoka line yako kwenda kwenye Bank Account fulani.

Ukianza kufuatilia tu unakuta hata polisi wenyewe wana anza kuku katisha tamaa au utafute mtu wa nje kwa gharama zako binafsi akufuatilie kumtafuta muhisika wa apo na bado uta ambiwa akuna assurance ya kupata ulichopteza kwa 100% zaidi utaongeza gharama za ufuatiliaji.

Huu ni mtando sio mdogo na wanahusika na huu wizi wengi.

Kikubwa cha kushauriana tu ni kwamba tuwe tunatumia sana Bank kufanya miamala yetu ya kifedha na kutoweka kiasi kikubwa cha fedha kwenye hizi simu pesa pesa kwenye laini.

Mabenki mengi yapo serious na Brand zao.

Tuweni makini sana maaana hawa watu wanarudisha sana watu nyuma
 
Nchi yetu na nyingi za ulimwengu wa tatu zina tatizo kubwa la kuruhusu jambo lililo kinyume na sheria ama uhuni tu kuendelea kwa muda huku taasisi zenye kazi ya kuzuia uhuni huo kukaa kimya.

Unaweza kusema huwezi kutapeliwa, lakini hiyo haina maana kuwa kinachoendelea kiendelee tu.

Nakumbuka tarehe 9 Mei 2022 majira ya saa 2.50 usiku nilipopokea ilikuwa simu ya ndugu yangu lakini alitumia namba ya mtu mwingine akiomba kiasi fulani cha pesa ili afanyiwe kipimo siku ya pili asubuhi (huyu alikuwa mgonjwa amelazwa katika hospitali fulani), katika mazungumzo nilimuuliza hiyo pesa nitume kwenye namba hii? akasema ndio.

Uzuri nilikuwa na hicho kiasi hivyo skupoteza muda, nikafanya muamala. Nikapiga kumueleza kuwa nimeshafanya muamala, naye akathibitisha kupokea.

Dakika chache baadaye ikaingia meseji kutoka namba 0733 584 129 iliyosomeka ''Nitumie tu kwenye namba hii 0716 135 528 Jina ni PAULO MAEMBE''

Hapa nikatafakari sana, kutapeliwa ni rahisi sana kwa sababu ya ''coincidence'', yaani kama ningekuwa sijatuma ile hela kwa ndugu yangu kulikuwa na nafasi kubwa sana kwa mimi kutuma ile hela kwa sababu ya mfuatano wa matukio na uharaka wa pesa husika.

Kwa kuwa nilikuwa na muda na kwa kuwa ni jambo rahisi kufanya uchunguzi mdogo, nikaamua kuanza kumtafuta huyu mtu anayeitwa Paulo Maembe.

Katika ulimwengu wa kidijitali, kupata taarifa ni jambo rahisi sana. Na wengi wetu tunaacha ''digital prints'' kwenye mitandao ya kijamii.

Kupitia ''search engine'' jina la Paulo Maembe likatokea mara kadhaa, nikaanza kumtafuta kwenye mitandao, baada ya siku chache nikapata mpaka namba halisi ya simu na mahali anapoishi.

Baada ya mazungumzo nikagundua kuwa namba yake imesajiliwa mara kadhaa na yeye mwenyewe hajui. Kwa wepesi tuliweza kuthibitisha mpaka kijana aliyemsajilia line ya simu ambaye kwa makusudi alisajili namba za ziada kwa sababu hizi za utapeli.

Zoezi la yeye kuthibitiisha namba zake likafanyika na hatimaye ile namba ya utapeli ikawa ipo ''deactivated''.

Mambo machache niliyogundua kuhusiana na huu utapeli wa ''tuma kwenye namba hii''

1. Vijana wengi wanaosajili namba nje ya ofisi husika za mitandao ya simu, huwa wanasajili namba nyingi unapoenda kusajili.

Wakati wanakwambia network inasumbua huku ukiwa umeshaweka finger print jua amesajili namba ya kwanza, anapokwambia embu turudie jua hapo inasajiliwa namba ya pili. Baada ya hapo anakupa namba moja huku ukiwa umebakisha namba nyingine mezani kwake ambayo yeye ataiuza kwa wanaohitaji hiyo namba.

Hizi namba zinanunuliwa na watu wengi haswa hao matapeli lakini hata ambao sio matapeli wanapotaka kuficha identity zao.
Kwa mujibu wa hawa vijana hizi namba huuzwa kati ya 30,000 - 50,000/-

Wengine wanaonunua namba hizi ni wageni wanaoishi hapa Tanzania hasa hawa wanaotoka nchi za Kiafrika.

2. Watu wengi hawana muda wa kujiridhisha namba ambazo zimesajiliwa kwa majina yao ( Namba ya Kitambulisho cha Taifa) , wengi wanatembea mjini hapa lakini kitambulisho chake kimetumika kusajili namba nyingi bila wao kujua na hawataki kujua.

3. Mfumo wa TCRA wa kuwasilisha malalamiko na mitandao ya simu sio rafiki sana. Maana inabidi mara nyingi uanzishe kesi polisi, na kama mjuavyo Watanganyika na masuala ya polisi. Wengi huamua kuacha tu huku wakisubiri tukio lingine la utapeli.

4. Watu wengi hatuna muda wa kutaka kujiridhisha kuhusu mtu tunayetaka kumtumia pesa, inawezekana una ahadi ya kumtumia pesa mtu, yaani ukipokea meseji ya hivi huchukui muda kutaka kuthibitisha. Ni vyema tuwe tunathibitisha.

View attachment 2239057View attachment 2239057

Swali ni je kwa nini system ya mitandao ya simu isikatae kusajili tena namba iliyosajiliwa na kuwa active? Au kwanini tcra au kampuni za simu zisifute namba zilizojirudia usajili ibaki namba moja ya mteja kisha mteja atakapoona mabadiliko yoyote asiyoyaelewa basi aende kwa wakala ku-claim namba yake? Hii nafkiri itakomesha. System bado haijatumika vizuri.

Unless otherwise makampuni ya simu yanashirikiana na hao matapeli kwenye kutapeli wananchi.
 
Sijaisoma mada yote, lakini narudia tena kusema, cha ajabu siku hizi matapeli wanatumia namba za TTCL (Kampuni ya Serikali) kupiga na kutuma ujumbe mfupi.
 
Jengo lao kubwa maofisi mengi lakini hamna wanachokifanya.
 
Kupitia ''search engine'' jina la Paulo Maembe likatokea mara kadhaa, nikaanza kumtafuta kwenye mitandao, baada ya siku chache nikapata mpaka namba halisi ya simu na mahali anapoishi.

Baada ya mazungumzo nikagundua kuwa namba yake imesajiliwa mara kadhaa na yeye mwenyewe hajui. Kwa wepesi tuliweza kuthibitisha mpaka kijana aliyemsajilia line ya simu ambaye kwa makusudi alisajili namba za ziada kwa sababu hizi za utapeli.
Kuna mapungufu mengi ya kitaalamu na ubunifu TCRA ni kama vile hawapo,
 
Nchi yetu na nyingi za ulimwengu wa tatu zina tatizo kubwa la kuruhusu jambo lililo kinyume na sheria ama uhuni tu kuendelea kwa muda huku taasisi zenye kazi ya kuzuia uhuni huo kukaa kimya.

Unaweza kusema huwezi kutapeliwa, lakini hiyo haina maana kuwa kinachoendelea kiendelee tu.

Nakumbuka tarehe 9 Mei 2022 majira ya saa 2.50 usiku nilipopokea ilikuwa simu ya ndugu yangu lakini alitumia namba ya mtu mwingine akiomba kiasi fulani cha pesa ili afanyiwe kipimo siku ya pili asubuhi (huyu alikuwa mgonjwa amelazwa katika hospitali fulani), katika mazungumzo nilimuuliza hiyo pesa nitume kwenye namba hii? akasema ndio.

Uzuri nilikuwa na hicho kiasi hivyo skupoteza muda, nikafanya muamala. Nikapiga kumueleza kuwa nimeshafanya muamala, naye akathibitisha kupokea.

Dakika chache baadaye ikaingia meseji kutoka namba 0733 584 129 iliyosomeka ''Nitumie tu kwenye namba hii 0716 135 528 Jina ni PAULO MAEMBE''

Hapa nikatafakari sana, kutapeliwa ni rahisi sana kwa sababu ya ''coincidence'', yaani kama ningekuwa sijatuma ile hela kwa ndugu yangu kulikuwa na nafasi kubwa sana kwa mimi kutuma ile hela kwa sababu ya mfuatano wa matukio na uharaka wa pesa husika.

Kwa kuwa nilikuwa na muda na kwa kuwa ni jambo rahisi kufanya uchunguzi mdogo, nikaamua kuanza kumtafuta huyu mtu anayeitwa Paulo Maembe.

Katika ulimwengu wa kidijitali, kupata taarifa ni jambo rahisi sana. Na wengi wetu tunaacha ''digital prints'' kwenye mitandao ya kijamii.

Kupitia ''search engine'' jina la Paulo Maembe likatokea mara kadhaa, nikaanza kumtafuta kwenye mitandao, baada ya siku chache nikapata mpaka namba halisi ya simu na mahali anapoishi.

Baada ya mazungumzo nikagundua kuwa namba yake imesajiliwa mara kadhaa na yeye mwenyewe hajui. Kwa wepesi tuliweza kuthibitisha mpaka kijana aliyemsajilia line ya simu ambaye kwa makusudi alisajili namba za ziada kwa sababu hizi za utapeli.

Zoezi la yeye kuthibitiisha namba zake likafanyika na hatimaye ile namba ya utapeli ikawa ipo ''deactivated''.

Mambo machache niliyogundua kuhusiana na huu utapeli wa ''tuma kwenye namba hii''

1. Vijana wengi wanaosajili namba nje ya ofisi husika za mitandao ya simu, huwa wanasajili namba nyingi unapoenda kusajili.

Wakati wanakwambia network inasumbua huku ukiwa umeshaweka finger print jua amesajili namba ya kwanza, anapokwambia embu turudie jua hapo inasajiliwa namba ya pili. Baada ya hapo anakupa namba moja huku ukiwa umebakisha namba nyingine mezani kwake ambayo yeye ataiuza kwa wanaohitaji hiyo namba.

Hizi namba zinanunuliwa na watu wengi haswa hao matapeli lakini hata ambao sio matapeli wanapotaka kuficha identity zao.
Kwa mujibu wa hawa vijana hizi namba huuzwa kati ya 30,000 - 50,000/-

Wengine wanaonunua namba hizi ni wageni wanaoishi hapa Tanzania hasa hawa wanaotoka nchi za Kiafrika.

2. Watu wengi hawana muda wa kujiridhisha namba ambazo zimesajiliwa kwa majina yao ( Namba ya Kitambulisho cha Taifa) , wengi wanatembea mjini hapa lakini kitambulisho chake kimetumika kusajili namba nyingi bila wao kujua na hawataki kujua.

3. Mfumo wa TCRA wa kuwasilisha malalamiko na mitandao ya simu sio rafiki sana. Maana inabidi mara nyingi uanzishe kesi polisi, na kama mjuavyo Watanganyika na masuala ya polisi. Wengi huamua kuacha tu huku wakisubiri tukio lingine la utapeli.

4. Watu wengi hatuna muda wa kutaka kujiridhisha kuhusu mtu tunayetaka kumtumia pesa, inawezekana una ahadi ya kumtumia pesa mtu, yaani ukipokea meseji ya hivi huchukui muda kutaka kuthibitisha. Ni vyema tuwe tunathibitisha.

View attachment 2239057View attachment 2239057
kweli kabisa mkuu
 
Mara ya kwanza tuli register kwa kitambulisho, then wakasema biometrics, tukapiga foleni ku register. Lakini utapeli unaendelea. Next tutaambiwa ku register na retinal scan. Hizi taasisi kama TCRA naona mambo yamewashinda kabisa.
 
Tangu mhandisi James Kilaba aondolewe Pala TCRA, mambo yameenda hovyo sana, yaani TCRA imekuwa kama ttcl, ni utapeli mtupu
 
Ukifuatilia utaona hizi sms zinakufikia sana pale either ukiwa na hela kwenye simu au ukiwa umefanya miamala kadhaa which means mitandao ya simu kuna watu wasio waaminifu wanauza taarifa za wateja.
Kuna ukweli kwa hili
 
Nawatukanaga wakikata nawapigia Tena mpk wazime simu shenzi kabisa
 
Back
Top Bottom