TCRA kama bado mna Meno yenu Makali natumaini hiki nilichokisikia leo kutoka Wasafi FM mtawaadhibu upesi

ID yako tu imetosha Kunithibitishia kuwa Uhalisia wako ndiyo huo huo kwani hata neno lao tu lenyewe la TCRA ni la Kizungu vile vile. Hopeless!!!!
Mkuu unaweza kubandika hyo sauti ya huo wimbo???
 
Kwenye ile katuni ya AKILI inayorushwa na TIBISII Wani kuna kale kabinti ka kike ka Akili(samahani kama ndio jina lake halisi) kwenye gauni lake la upinde wa shingoni mbona ule upinde wa kuzunguka gauni lake zile rangi ni kama zile rangi za bendera ya LGBT???
 
Sasa wadau wanazungumzia Bongo , wewe unasema za mbele. Huko mbele wameshahalalisha mpaka ndoa za jinsia moja. Tatizo ni hapa Bongo.
Kasome tena thread mwenye uzi amezungumzia nyimbo za kizungu zenye matusi ambazo zinapigwa kwenye vyombo vya bongo.

"TCRA Mzukulu ninawataarifu kuwa leo Jioni kati ya Saa 12 na dakika 31 hadi na dakika 33 Disk Joker ( DJ ) aitwae Delvic ( kama nimelikosea mnaolijua mtalirekebisha ) aliupiga Wimbo wa Kizungu ambao ndani ya huo Wimbo mara mbili nikalisikia Tusi Kubwa sana ashakum si Matusi la Mother Fucker na nikaanza Kujiuliza je, huyo DJ alikuwa amepitiwa au labda anatutukana Sisi Wasikilizaji wake?"
 
Ila kwa kweli ngoma kama hizo zenye hayo maneno yaitwayo "matusi" kwa kawaida zikichezwa redioni hayo maneno huwa wanayaminya kwa sababu si mazzuri. Mfano kuna jumamosi moja mchana hapo Uhuru fm ile "Hit 'em Up" ya 2Pac ilikuwa inachezwa, t ena kama ilivyo. Ni aibu kwa kweli hasa kama ikiwa mko kwenye daladala na mchanganyiko wa watu.

Hii inaonesha kuna tatizo kubwa kwenye uongozi wa hivi vituo hasa kwenye sera yao ya muziki upi uchezwe redioni na pia ni uthibitisho kuwa hawa watoto wanaokuwa Radio Dj's siku hizi wengi ni Zero Brain. Dj Kama Bonny Luv au Dj JD, wasingeweza kufanya upuuzi huu kwa radio. Hawa ma_Dj watoto wanapaswa wapewe darasa.
 
Ndio maana nikasema tatizo ni Bongo, kwamba kweli ni ngoma za huko mbele inawezekana kwao ziko saaa, lakini kibongo haziko poa kuchezwa redioni bila kuhaririwa hayo jamaa anayosema ni matusi.
 
Ndio maana nikasema tatizo ni Bongo, kwamba kweli ni ngoma za huko mbele inawezekana kwao ziko saaa, lakini kibongo haziko poa kuchezwa redioni bila kuhaririwa hayo jamaa anayosema ni matusi.
Mkuu Kindly note that, ngoma moja kukubaliwa kupigwa hapa Marekani kusifanye hata huko bongo hizo ngoma zipigwe hata kama sheria na kanuniza nchi haziruhusu, kwa hyo kama hapa Atlanta G, ni sa01:56 basi hata huko pia kuwa ni sa01:56 mkuu??? Nadhani mleta uzi angewaandikia Tcra email kuwaataarifu hyo situation, Hapa marekani ushoga umehararishwa bahadhi ya majimbo na sio majimbo yote.
 
Sasa wadau wanazungumzia Bongo , wewe unasema za mbele. Huko mbele wameshahalalisha mpaka ndoa za jinsia moja. Tatizo ni hapa Bongo.
Ila bado wanauwezo wa kufungia vituo vya ndani kucheza nyimbo zilizo nje na mahadiri yetu ata kama niza nje kama china walivyo fungia vituo vyao kucheza nyimbo za lady gaga
 
Mimi nimevutiwa na hilo neno "kabinti ka kike".
 
Mimi naona kama wote tunaongea lugha moja hapa. Kwamba hizo nyimbo inawezekana ziko poa kuchezwa huko lakini kwa hapa Bongo ili kuzicheza redioni ni vyema zifanyiwe uhariri kuondoa/kuminya hayo maneno. Hilo la ushoga nimelileta kuonesha ule utofauti tu, kuwa wao wameruhusu ndoa za jinsia moja ila sisi huku hapana.
 
Hili hii situation isitokee na TISIARAEI wachukue hatua gani mkuu na huyu mleta mada tumwambie nn hii hyo taarifa iwafikie hao TISIARAEI
 
Ila bado wanauwezo wa kufungia vituo vya ndani kucheza nyimbo zilizo nje na mahadiri yetu ata kama niza nje kama china walivyo fungia vituo vyao kucheza nyimbo za lady gaga
Hapa una maana kuwa kwa sasa sheria imewaruhusu hawa wadau wa redio kupiga nyimbo zozote hata zenye lugha mbaya!? Yaani hakuna sheria inayowakataza!?
 
Hapa una maana kuwa kwa sasa sheria imewaruhusu hawa wadau wa redio kupiga nyimbo zozote hata zenye lugha mbaya!? Yaani hakuna sheria inayowakataza!?
Kwani kwani kuna sheria mpya imetungwa tofauti na ile sheria ya awali???
 
Mimi ndo mwenyekiti wa TCRA awachukuliwi hatua yoyote

Unasemaje ss
 
Unashtaki kwenye genge la wahuni, usitegemee kitu.
 
Kamuulize aliyekubebea Mimba yako Miezi Kenda ya Kukuleta hapa Ulimwenguni atakuwa na Jawabu Mujarab kabisa la Kukujibu na zuri kuliko.
Maneno kama haya ndo huaribu content nzima ya ulichokusudia kutueleza...
 
Hapa una maana kuwa kwa sasa sheria imewaruhusu hawa wadau wa redio kupiga nyimbo zozote hata zenye lugha mbaya!? Yaani hakuna sheria inayowakataza!?
Naweza sema hvyo ndio maana wanazipiga ata za watanzania had pale watakapo ambiwa nyimbo flan imefungiwa ndio wanapo acha kuicheza kwenye vituo vyao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…