TCRA kufunga simu zisizosajiliwa ni mpango wa serikali kuwabana wale wanaotumia simu kusambaza habari za uzushi au fake news

TCRA kufunga simu zisizosajiliwa ni mpango wa serikali kuwabana wale wanaotumia simu kusambaza habari za uzushi au fake news

Habari za uzushi za kutekwa kwa mdhibiti mkuu wa fedha za serikali wa zamani Profesa Assad zimezusha taharuki kubwa.

Na mpaka ilipoibuka video mitandaoni ambapo Profesa Assad anaonekana yupo salama na mwenye afya njema, watu wengi waliingiwa na hofu kubwa.

Ifikapo tarehe 31 Desemba mwaka huu serikali kupitia mamlaka ya mawasiliano TCRA itazifunga simu zote ambazo zitakuwa hazijasajiliwa.

Ili kuweza kusajiliwa inambidi mhusika kutoa alama za vidole na baada ya hapo kuweza kufuatiliwa na kubaini ni yupi mtumiaji sahihi wa kampuni ipi ya simu.

Hivyo basi, kuanzia tarehe 1 Januari mwaka 2020 mtu yeyote ambae atatumia simu yake ya mkononi atakuwa ni yule tu ambae amesajiliwa na TCRA.

Je, huo ndo utakuwa mwisho wa habari za uzushi mitandaoni?

Au ndo utakuwa mwanzo wa kuwadhibiti wale wote ambao wanatumia simu zisizosajiliwa?
Watatumia za Nje na kufanya Roaming,
Pili watu wana maarifa sana
 
Watu wataendelea kutumia WhatsApp, maana kufungwa kwa laini haku affect WhatsApp, wifi zipo, ila tatizo wale wa vijijini sasa
 
Mitandao ya kijamii inayohitaji member kujisajili kwa kutumia majina na email badala ya namba ya simu kama Jamii Forum hakuna namna mtu anaweza akambaini mhusika endapo huyo mtu atatumia majina bandia na email bandia. Hakuna.

Wenye uwezo wa kukubaini kwa mukhtadha huo ni Google tu kule Marekani, hawa wengine hamna kitu ni mbwembwe tu na vitisho kibao vya nyoka mfu.

Mitandao, kwa mtizamo huo, inayodai member kujisajili kwa namba ya simu ni za kuepuka kwa gharama yoyote, namba za simu ndo inabeba the potential risk to be tracked.
 
Habari za uzushi za kutekwa kwa mdhibiti mkuu wa fedha za serikali wa zamani Profesa Assad zimezusha taharuki kubwa.

Na mpaka ilipoibuka video mitandaoni ambapo Profesa Assad anaonekana yupo salama na mwenye afya njema, watu wengi waliingiwa na hofu kubwa.

Ifikapo tarehe 31 Desemba mwaka huu serikali kupitia mamlaka ya mawasiliano TCRA itazifunga simu zote ambazo zitakuwa hazijasajiliwa.

Ili kuweza kusajiliwa inambidi mhusika kutoa alama za vidole na baada ya hapo kuweza kufuatiliwa na kubaini ni yupi mtumiaji sahihi wa kampuni ipi ya simu.

Hivyo basi, kuanzia tarehe 1 Januari mwaka 2020 mtu yeyote ambae atatumia simu yake ya mkononi atakuwa ni yule tu ambae amesajiliwa na TCRA.

Je, huo ndo utakuwa mwisho wa habari za uzushi mitandaoni?

Au ndo utakuwa mwanzo wa kuwadhibiti wale wote ambao wanatumia simu zisizosajiliwa?

Mkuu Richard JPM kaongeza siku hadi tarehe 20 January 2020, tutaheshimiana tu hapa kwenye mtandao. Haiwezekani watu kila siku kazi yao ni kupotosha tu na kueneza majungu.
 
Watatumia za Nje na kufanya Roaming,
Pili watu wana maarifa sana

Mkuu, nina imani kwamba unaelewa kinachoendelea.

Ni kweli watu wana maarifa sana, lakini dola inapoamua kulifanyia kazi jambo fulani hali huwa si hivyo unavyofikiri.
 
Back
Top Bottom