TCRA, nawaombea msamaha Wasafi TV

TCRA, nawaombea msamaha Wasafi TV

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
324
Reaction score
649
TCRA NINAUNGANA KUWAOMBEA RADHI WASAFI TV.

Na Elius Ndabila
0768239284

Leo TCRA wametoa mvua ya miezi sita kwa Wasafi TV kwa kile kinachosemekana ni kurusha maudhui kinyume cha sheria.

Niwapongeze TCRA kwa kusimamia sheria hizi kwa uangalifu na nidhamu kubwa. Tunajua kuwa sheria ni msumeno, na hii inathibitishwa na adhabu hizi ambazo wamekuwa wakizitoa TCRA.

Nimejaribu kuiona ile picha ya huyo Msanii. Lakini sitaki kuzungumzia hii picha, nataka kuzungumzia hii adhabu.

Wasafi TV kupitia chombo chao hiki wameajiri watu wengi ambao maisha yao yanategemea pale. Kuwafungia miezi sita ni kuhatarisha maisha ya hawa watu. Lakini Wasafi Tv wanayomatangazo mbalimbali ya watu ambao wanakiamini chombo hicho kuwa ni munyororo tosha kwenye kuongeza wateja ktk biashara zao. Kuwafungia miezi sita ni kushusha biashara za watu ambako serikali inategemea kupata kodi.

Lakini ipo video inayoonyesha Wasafi Tv waliomba msamaha siku ileile. Sheria zetu zina option, ninaomba TCRA waangalie option nyingine ili kupunguza ukubwa wa adhabu hii ambayo imetokana na kosa la mpuuzi mmoja aliyeamua kuruhusu maudhui ambayo si sahihi kwa mjibu wa sheria zetu.

Ninaomba TCRA waangalie upya adhabu waliyotoa ili kuweza kuwasaidia watu hawa. Lakini pia ninashauri sheria zetu ziweze kutazamwa upya ili yanapotokea makosa kama haya aadhibiwe mtu na isiwe taasisi. Kwa mfano hapa angeadhibiwa huyu msanii na Wafanyakazi wa Wasafi TV ambao siku hiyo waliruhusu picha hizo kurushwa.

TCRA ni walezi, ninawaomba leo mvae sura ya ulezi ya kuonya, kushauri na kuhurumia. Picha hii imetudhalilisha wote, lakini ngoja tufanye exception kwa kumpa adhabu huyu Msanii na ikiwezekana kuwatoza faini ya fedha Wasafi TV na si kufungia chombo.
 
Wasafi walishapigwa onyo na faini kwa mambo hayo hayo "kipindi cha woman matters", wakaja wakafungiwa week moja kwa sababu ya mambo hayo hayo "inshu ya babalevo" sahivi wamerudia Tena kosa.

Siwachukii wasafi ila hiyo adhabu ni msamaha tosha, walistahili zaidi ya adhabu hiyo waliopewa

Note: watu wanatumia zaidi ya miaka >2 chuoni kusomea uandishi wa habari kwa hiyo uandishi wa habari sio kazi rahisi kiasi hicho
 
Pamoja na mambo mengine wao wanaangalia makusanyo na kinda maslahi ya cha tawala. Mengine mbwembwe
 
Hii ingekuwa chanzo cha mapato
Tupo uchumi wa kati aiseh
 
Hapo linatengenezwa tatizo ili mzee baba apate umaarufu wa kisiasa si umeona umaarufu wake umeshuka.
 
Unajua ni kampuni ngapi zimefungwa completely chini ya utawala huu,tena zingine kwa kukomolewa tu,hao unaowaombea msamaha ndio walikuwa mavuvuzela wa majizi ya kura,kwa kuwa wamefanya kosa nashauri adhabu iwe kubwa zaidi na sio kupunguziwa
 
Hizi sheria katili zilipitishwa na kushangiliwa na wabunge wa CCM tena kwa kuwabeza sana wapinzani kwa vijembe na kebehi.

Huu ni muda muafaka wa kila mtanzania kupokea na kula matunda ya mitano tena.

"Leo mnakaa kimya kwasababu haliwahusu na tunaoumizwa ni sisi, kesho wakimalizana na sisi watawageukia nyie" By Tundu
 
Maoni yangu napendekeza WCB wafungue hata mwaka mzima. Wana promote mambo ya kijinga kijinga sana na kuona wao ni werevu kuliko media yoyote.
 
Adhabu iongezwe ili iwe funzo kwa wapiga ksmpeni wengine wa SISIEEM wasibweteke saanaa kuona kama kupiga kwao kampeni ndo wanaweza fanya loloootee lile wakaachwa,wapigwe tuu kifungo hamna namna.

Lakini pia maudhui chafu kabisa za kipuuzi hazina haja ya kuzi intertain kabiisaa kabsa
 
Wasafi wao si kijani kindakindaki wanajiona wanaweza fanya lolote
Acha waadhibiwe kwa sasa hawana umuhimu wangoje chaguzi ukaribie watatumika tena

Ova
 
Back
Top Bottom