TCRA yaipiga faini ya Tsh. bilioni 11.89 Kampuni ya Intaneti ya Raha Limited kwa kuendesha shughuli zake bila kuwa na kibali

TCRA yaipiga faini ya Tsh. bilioni 11.89 Kampuni ya Intaneti ya Raha Limited kwa kuendesha shughuli zake bila kuwa na kibali

Ukiwa mfanyabiashara hakuna jambo linakera kama kupigwa faini ambayo haiendani na uhalisia na mtaji au mapato ya biashara yako.

Mamlaka ziwaangalie wafanyabiashara. Wasitumike kama kitega uchumi.

Sheria zipo. Zinapokiukwa waangalie na uhalisia sio kuweka kizingiti kwa wafanyabiashara.

Uchumi utakuwa kwa kujali wafanyabiashara. Isifikie kipindi waonewe kwa misingi ya sheria kandamizi au maamuzi ya kuumiza.

Serikali iangalie hili. Isije kupelekea kuua biashara binafsi bila kujua ni kuua uchumi wa nchi.
 
UPUUZI MTUPU! Kampuni thamani yake haifiki hata bilioni moja halafu faini yake ni bilioni 11? 😳😳😳😳
Itakuwa ni typo tu ya mleta mada. Ukijumlisha pesa zote haifiki hata 50m
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Walikuwa wapi kuwapa hiyo fine mwezi March. Biashara za kuviziana ni sawa na uchawi
 
Swali ni kwann ulifanya kazi bila kibali ndoshida inaanzia hapo, yaani utajitetea vipi kwamfano aiseee? Tena hiyo ndgo ukiangalia na formula zake kwa usahihi unaweza kukuta unatakiwa kulipa T na sio B

Wasingeiba hayo masafa je tcra wangepata Hizo billions?
 
hawa wanaadhibiwa sababu wamejirock down na kupunguza wafanyakazi sababu ya madhara ya corona. sasa sielewi TCRA ilitegemea wafanyeje wakati wateja wamewakimbia sababu ya corona.

Yeah na wamepunguza wafanyakazi sana
 
hawa wanaadhibiwa sababu wamejirock down na kupunguza wafanyakazi sababu ya madhara ya corona. sasa sielewi TCRA ilitegemea wafanyeje wakati wateja wamewakimbia sababu ya corona.
Acha uongo! Wakati wa corona ndiyo Kampuni zinazotoa huduma za mawasiliano wamepata faida zaidi na zaidi kwa kuwa bandwith zimetumika zaidi kwa sababu kampuni nyingi zilikuwa zinafanya kazi toka home! Sawa na Pharmacy. Kama hujui nyamaza.
 
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeipiga Faini ya Sh.bilioni 11.89 Kampuni ya Raha Limited watoa huduma ya Internet kwa makosa mbalimbali ikiwemo kutumia masafa ya mawasiliano ya Radio katika wigo 1452-1482 MHZ bila kuwa na leseni halali kutoka TCRA tangu 24 Machi 2020.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi James Kilaba amesema TCRA ilitoa leseni ya matumizi ya huduma za mawasiliano kimkoa, Leseni ya miundombinu ya mawasiliano, Leseni ya Kitaifa ya matumizi ya mawasiliano ya kieletroniki, leseni ya kufunga na kutengeneza vifaa vya Mawasiliano na Leseni ya matumizi ya namba kwa muda tofauti tofauti.

Mhandisi Kilaba amesema kampuni ya Raha baada ya kupata leseni walitakiwa kufanya mambo mbalimbali ikiwa kujenga,kusimika, kutunza ,kutumia na kusimamia miundombinu ya mikoa ya Dar es Salaam,Arusha na Tanga ifikapo Februari 2020 na Kilimanjaro ifikapo Septemba 2021 pamoja na kuandaa na kuwasiliasha mpango wa kuendeleza rasilimali Watu kwa Mamlaka hiyo.

Amesema kuwa katika kufanya kazi waliweza kuchukua masafa ya mawasiliano ya Radio mkoani Mtwara bila kubali na kupigwa faini sh.Bilioni 11.85.

Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Kilaba amesema kampuni Raha wanatakiwa kulipa faini sh.milioni 10 kwa kujenga Miundombinu ya mfumo wa mawasiliano kuendesha na kutoa huduma za mawasiliano mkoani Mtwara bila ya kuwa na Leseni kutoka TCRA, Kulipaa Faini ya Tsh. milioni 5 kwa kutotimiza masharti ya Leseni baada ya kushindwa kutoa huduma mkoani Kagera Agasti 2019.

Aidha amesema kampuni hiyo inatakiwa kulipa Tsh.milioni 5 kushindwa kuwasilisha taarifa za ukaguzi wa mahesabu ya ndani ya miezi sita kuanzia mwaka wa hesabu na sh.milioni tano zingine ni kushindwa kuwasilisha mpango mkakati wa kuendeleza rasilimali Watu huku faini nyingi Tsh. milioni 10 kushindwa kutimiza masharti ya leseni hususani kushindwa kuomba upya kwa muda uliopangwa.

"Masafa ni rasilimali ya Taifa haikopwi wala haiibwi na mtu yeyote."Amesema Kilaba.

Chanzo: Isaamichuzi blog
Tunahangaika kutafuta pesa za kampeni na vilevile ni hela ya kisukuma uchumi wa kufikia uchumi wa Kati kutoka B2 na Sasa hapo tumefondoka mpaka B1.
 
UPUUZI MTUPU! Kampuni thamani yake haifiki hata bilioni moja halafu faini yake ni bilioni 11? [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
Nadhani kuna kitu nyuma ya pazia voda tigo airtel halotel wana husika
 
Back
Top Bottom