BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA)imeiamuru ZamaMpya TV Online kulipa faini Shilingi Milioni Mbili (2,000,000) ndani ya siku 21 kufuatia kuchapisha hisiyo na midhania ya habari.
Taarifa hiyo ilihusu maudhui ya Selemani Msindi (Afande Sele) ambayo yanatuhumiwa kuwa ya uchochezi kuhusiana na Tozo mpya za kielektroniki zilizotangazwa na Serikali hivi karibuni kuanza kutozwa kwa njia ya benki.
Aidha ZamaMpya TV itakuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha miezi mitatu huku pia wakitoa onyo kwa kituo hicho na kuwataka kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na kuwa watawajibika kwa kila maudhui yatakayochapishwa kinyume na taratibu.
Taarifa hiyo ilihusu maudhui ya Selemani Msindi (Afande Sele) ambayo yanatuhumiwa kuwa ya uchochezi kuhusiana na Tozo mpya za kielektroniki zilizotangazwa na Serikali hivi karibuni kuanza kutozwa kwa njia ya benki.
Aidha ZamaMpya TV itakuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha miezi mitatu huku pia wakitoa onyo kwa kituo hicho na kuwataka kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na kuwa watawajibika kwa kila maudhui yatakayochapishwa kinyume na taratibu.