Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vyombo vya habari nchini katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu kuvipatia vyama vya siasa nafasi sawa katika kuripotiwa habari bila upendeleo ili kuondoa malalamiko.
Meneja wa Kitengo cha Utangazaji TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka ameyasema haya leo katika Mkutano wa Misa Tanzania na Wadau (MISA-TAN - Wadau Summit 2025) uliofanyika jijini Dodoma, Mhandisi Kisaka amesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kufanya kazi kwa usawa, haki na uadilifu, hasa wakati wa kuripoti habari za vyama vya siasa.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema, kuvipatia haki sawa vyama vya siasa itasaidia kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa sahihi na zinazowawezesha kufanya uamuzi wa busara hususani wa kuchagua viongozi wanaowataka na sio kukipatia chama kimoja muda mrefu wa kujieleza na kuvinyima vingine, kwani ni kosa kisheria na hatua za kinidhani zitachukuliwa.
Meneja wa Kitengo cha Utangazaji TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka ameyasema haya leo katika Mkutano wa Misa Tanzania na Wadau (MISA-TAN - Wadau Summit 2025) uliofanyika jijini Dodoma, Mhandisi Kisaka amesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kufanya kazi kwa usawa, haki na uadilifu, hasa wakati wa kuripoti habari za vyama vya siasa.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema, kuvipatia haki sawa vyama vya siasa itasaidia kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa sahihi na zinazowawezesha kufanya uamuzi wa busara hususani wa kuchagua viongozi wanaowataka na sio kukipatia chama kimoja muda mrefu wa kujieleza na kuvinyima vingine, kwani ni kosa kisheria na hatua za kinidhani zitachukuliwa.