Teak Wood Tree - Loan

Teak Wood Tree - Loan

Poa mkuu na kutumia kwa inbox number ya huyo sister, i hope atakuwa na contacts za huyo mteja.
 
Hii ni fursa nzuri sana,ila ni kuomba Mungu wasije wakabadilikia njiani,maana kupanda mitiki kwa mwaka 2014 maana yake mkopo ni 2017 kitu ambacho si kibaya na wala si muda mwingi iwapo hawatabadili masharti yao!je wadau mnaweza kunipa mwanga miteak inastawi zaidi katika maneo au hali ya hewa ya namna gani?na kwa Morogoro ni ukanda upi inaweza kustawi zaidi?

Mkuu 1800, mitiki inastawi sana katika mikoa ya pwani,tanga na morogoro. Mikoa ambayo inajoto kiasi na mvua za wastani kulingana na ukweli kwamba mitiki huvumilia sana ukame na inatunza maji mengi sana.
Pia ni miti ambayo hukua kwa kasi ya ajabu kama utazingatia hatua za awali kuandaa shamba lako kwa kulitifua na trekta ili kuruhusu mizizi kupenya kwa urahisi. Ukizingatia hilo na ukadhibiti uchafuzi ufanywao na mifugo hasa ng'ombe pia moto, utastaajabu jinsi inavyokimbia katika ukuaji.
Ni mti ambao unavumilia sana ukame na nzuri zaidi huendelea kuchipua hata kama umekatwa na kubaki kisiki.
Nawasihi
 
Last edited by a moderator:
Issue ya ng'ombe na moto unadhibiti vp mkuu?
Tayari nishakutumia.

Utadhibiti ng'ombe kwa kuweka ulinzi hasa ukipata mtu aliyeoa na kuhusu moto ni kwa kupalilia mara kwa mara na kutengeneza barabara kuzunguka shamba. Pia ni mhimu sana kujenga mahusiano mazuri na wananchi wa eneo husika ili kuhakikisha ulinzi mbadala kwa waharifu wengine zaidi hasa wafugaji ambao ni sugu kwa uchafuzi huku mashambani. Mathalani kuingiza ng'ombe shambani, kukatakata miti kusiko na mpango etc.
Kadharika, miti ikishakuwa mikubwa zaidi unaweza kufuga mifugo michache kwajili ya malisho ili kusaidia zoezi la upaliliaji kadri watakavyokuwa wakila nyasi ndani ya shamba. Unaweza ukaona sasa ni jinsi gani ambavyo unaweza kulimudu shamba la miti kwani kadri ikuwavyo gharama za kutunza zinazidi kuwa chini zaidi.
 
Mkuu hii kitu inawezekana kama utakuwa na tittle deed ya shamba lako plus an operating business.
Pia kama shamba lako ni large scale basi nenda pale sua kuna mhadhiri anaconnection na shirika flani marafiki wa mazingira kutoka canada wanatoa mkopo mrefu na mnono kwelikweli kiasi kwamba utamu wa kupanda miti utaufaidi mpaka siku ya mavuno ya mitiki hakika utakuwa umekinai.
Kesho ntajongea CRDB nikajihakikishie mwenyewe then nilete mrejesho kamili hapa jukwaani.

large scale nikuanzia hekaringapi?..
 
Wakuu mi nina hekta 15 Hale-Tanga;- natafuta mnunuzi, sijui wanapatikana wapi? Miti yangu ina miaka 17. If you can direct me please!
 
Mkuu kindege534 nitumie namba yako PM. Ningependa kujua ulichoandika ni hekta 15 kwa maana ya ekari 37.5? Au umeandika hekta kimakosa kumbe ni ekari15?
Kama ina umri huo basi mi nakuja na wateja hapo Hale.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu vp ngombe/mbuzi wanakula majani ya mitiki napenda kufahamu. Pili kwa maeneo ya segera hii miti inastawi? asanteni
 
Wakuu vp ng'ombe/mbuzi wanakula majani ya mitiki napenda kufahamu. Pili kwa maeneo ya segera hii miti inastawi? asanteni
 
Back
Top Bottom