Tegeta Escrow: TANESCO yashindwa kesi dhidi ya IPTL. Yaamriwa kulipa zaidi ya Sh. Bilioni 320!

Mkuu 10% sio haba hapa Mwenye nchi akigawana na washikaji na walamba asali wenzake.

Ukiongeza mengine kama holidays, shopping, na nyumba za bure Dubai utaona kwanini wanasaini hii mikataba na kuwafungulia watu kesi za uhaini.
 
Wanashindwaje kesi waliyojishtaki wenyewe? Hapo wameshinda kesi, we chizi nini?
 
mhhh.. kazi ipo hii nchi ukiijulia kutajirika ni kufumba na kufungua macho tu
tunajila wenyewe hao wazungu na wageni ni mitego tu ila wasuka deals na walaji ni wazee wetu wakubwa na tunaamka nao kila siku nchini mwetu yamekosa uzalendo na aibu kabisa hivi kweli ukaitie short nchi yako masikini billion zaidi ya 320 hata mshipa wa aibu hauna...!

wazee wetu mmekosa uzalendo kwa kiasi kikubwa mno mnatukosea sana vijana nyie.!

vijana tunapambana sana mazingira magumu mno kwa nchi yetu hii tuoneeni huruma basi japo kidogo haya maisha magumu mnayasababisha ni nyinyi maana loss kama hiyo ya karibu billion 350 hapo hakuna mitaji kwa vijana ya kutosha wala wanawake wala hospitali za kutosha wala ajira za kutosha mnafanya tujenge chuki na serikali yetu inakera na kuumiza sana.
 
Anaye umia ni mwanachi wa kawaida kwa kuingezewa kodi na tozo
 
Walevi wa Madaraka pamoja na chawa watakwambia ni uzushi naniupotoshaji wa kiwango cha mlima everest.
 
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.
ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

My take.
Muda si mrefu tutasikia Tanzania yashindwa kesi na DP world yatakiwa kulipa trillioni 15.

Njia mpya iliyobuniwa na wakubwa ndani ya serikali kuchota kodi za walala hoi, unasaini mkataba wa kijinga ambao ni kichaa tu anayeweza kuuvumilia alafu ukiulizwa unasema tumeshindwa kesi tulipeni tu.
 
Nafikiri naye anahusika naanza kupata wasiwasi miaka saba nyuma mambo haya hayakuwepo!
 
Mikataba inavunjwa kwa maagizo ya wanasiasa halafu utarajie mawakili washinde kesi?
 
Ni sawa tu na huu mkataba wa kijinga kati ya bandari na dp world.tutakuja kupigwa zaidi ya hii ya tanesco
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…